|
|
|
Haja ya kusimamisha maadili ya Kiislamu Tangu Waislamu wasahau wajibu wao wa kuuongoza ulimwengu huu na badala yake kujiingiza kwenye migogoro na mapambano ya wenyewe kwa wenyewe, dunia imekuwa ikiongozwa na mifumo ya kibeberu ya mrengo wa kikristo na kiyahudi (kiliberali) au ile iliyodaiwa kuwa ni ya kikomunist na kijamaa. Kutokana na mifumo hiyo ya kitwaghuti wanaadamu wameachwa taabani kiuchumi, kisiasa, kijamii na kimaadili Mifumo hiyo ya kibeberu imeweka sura mbaya sana duniani. Imeweka matabaka ya walionacho na wasionacho. Dunia imejaa uchoyo na uroho, chuki na mauaji, udhalimu na unafiki. Historia ya dunia iliyotawaliwa na mifumo hiyo ya kibeberu inatuonyesha kuwa imesababisha madhila makubwa duniani. Mifumo hiyo ya kibeberu ndiyo iliyoanzisha, kusimamia na kuendesha biashara ya utumwa. Mifumo hiyo ndiyo iliyopora uhuru wa nchi na watu na kuwatawala kwa nguvu. Mifumo hiyo ndiyo iliyoanzisha na kuchochea vita na mauaji. Mifumo hiyo ndiyo iliyoanzisha vita kuu ya kwanza na ya pili ya dunia. Mifumo hiyo ndiyo iliyomporomosha Mwanaadamu kutoka kwenye utu na kumrudisha chini kuliko hata wanyama. Wanaadamu wanaadhibiwa na urongo walioufuma wao wenyewe. Wanaendelea kudhurika, kutaabika na kudhalilika, kuliko kunufaika, kustawisha na kuboresha maisha yao. Kwa nini iendelee kuwepo na kupandikizwa katika vichwa vya vizazi vipya? Mfumo wa maisha ya Kiislamu ndio mtatuzi wa madhila haya, lengo lake si kuwalazimisha watu wote wawe waislamu, bali kuboresha hali za wanaadamu kimaaadili, kiuchumi, kisiasa na kijamii. Kuweka na kusimamia Uadilifu, haki na maendeleo ya kivitu na kiroho katika maisha yao. Ni kutokana na lengo hili la Uislamu, Waislamu wanatakiwa wafanye jitihada na harakati mbali mbali kwa mali na nafsi zao kuhakikisha kuwa dola na Serikali zinaendeshwa kwa kufuata sharia ya Allah (s.w.). "Enyi mlioamini! Shikeni hadhari yenu (juu ya maadui zenu. Msikhadaike). Tokeni (kwenda vitani) makundi moja moja au tokeni nyote pamoja."(4:71) Na mna nini hampigani katika njia ya Mwenyezi Mungu na (katika kuwaokoa) wale waliodhaifu katika wanaume na wanawake na watoto- ambao husema: "Mola wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na tujaalie tuwe tuna mlinzi anaeyetoka kwako na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anayetoka kwako. (4:75) Kwa hakika Lengo la Uislamu ni kuona kuwa ulimwengu mzima unakombolewa toka mikononi mwa Makafiri na unakuwa Jamhuri ya Kiislamu (World Islamic Republic): Yeye ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uongofu na Dini iliyo ya Haki, ili ishinde na kuwa juu ya dini zote. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Shahidi.(48:28) |
Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia wasiwasi AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA
WANAFUNZI WA KIKATOLIKI
Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa
Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia alivyosilimu Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani
Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania
dini yake
'Waislamu wenye sisa kali'
MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu
- 2
Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane
Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya
Z'bar
Da’awa Handeni yashika kasi
Kongamano la vijana wa
Kiislamu Masjid Nuur Dar
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|