|
|
|
Mama Chuki asema Waziri hakusema kweli Na Mwandishi Wetu MADAI ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Mh. Ali Ameir aliyoyatoa bungeni hivi karibuni kwamba mwanafunzi Chuki Athumani alikamatwa na makaratasi ya uchochezi yamekanushwa. Akiongea na mwandishi wa habari hizi hospitalini Mwanafunzi huyo alisema kwamba amefadhaishwa na kusikitishwa sana na taarifa hizo za Waziri. Alisema siku ya tukio alikuwa akitoka nyumbani kwao kwenda kwa ndugu zake Magomeni Kagera, alichoshtukia ni risasi inampiga na kuanguka chini na akaongeza kusema kwamba hakuwa na kipande chochote cha karatasi. Aidha mama yake naye amekanusha kwamba amewahi kumwambia Mh. Waziri Ali Ameir kwamba mtoto wake hatarudi tena shuleni alikokuwa. Mama huyo katika hali ya huzuni ameeleza kuwa pamoja na yote yaliyomkuta mwanawe inasikitisha kwamba bado haachwi akapata utulivu bali anazidi kusingiziwa mambo. Ameendelea kusema kwamba inavyoelekea shutuma hizi mpya zinalenga kuwaweka mbali hata wale ambao wangetaka kumsaidia mwanawe. "Wakisikia kwamba anatuhumiwa kwa uchochezi wajiweke mbali kuepuka matatizo", amesema kwa masikitiko mama huyo. Aliongeza kusema Mama Chuki kwamba kilichotokea ni a siku mwanawe alipofunguliwa pingu maafisa wa Wizara walimhoji endapo walimu wake Chuki wanakuja kumuona ambapo aliwajibu hapana. Ikawa imejengwa hoja kwamba waalimu hao hawamtakii kheri mtoto Chuki. Lakini mama Chuki anasema kwamba haoni ni vipi waalimu wake walaumiwe kutomtembelea mwanafunzi wao wakati ule ambapo hata yeye mwenyewe mama mzazi alikuwa haruhusiwi kumwona ila kwa kibali maalumu na siku akiwa hana kibali hicho huzuiwa au hughasiwa. Mama huyo amesisitiza kwamba sio kweli kuwa amemweleza
Waziri wa Mambo ya Ndani au mtu yeyote kwamba eti mwanawe hatasoma tena
katika shule ya sekondari ya Al-haramain kwa sababu inafundisha mambo ya
uchochezi au kashfa.
|
Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia wasiwasi AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA
WANAFUNZI WA KIKATOLIKI
Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa
Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia alivyosilimu Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani
Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania
dini yake
'Waislamu wenye sisa kali'
MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu
- 2
Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane
Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya
Z'bar
Da’awa Handeni yashika kasi
Kongamano la vijana wa
Kiislamu Masjid Nuur Dar
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|