|
MASHAIRI
Uzawa wa Mtume Muhammad (s.a.w.)
Bismillahi Karima, mwanzoni nalitamka,
Jina lake Muadhama, Mola aliyetukuka,
Mwenye wingi wa neema, na huruma kadhalika,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Sikuye ya kuzaliwa, Muhammad imefika,
Kote inashangiliwa, Dunia inachemka,
Mtume tuloletewa, uzaziwe twakumbuka,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Kumi mbili iligota, wenye ndovu ule mwaka,
Ni mwezi mfungo sita, kazaliwa kule Makka,
Nuru yake ikimeta, kama taa akiwaka,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Ni Mtume Muhammad, mjumbe asiye shaka,
Ametumwa na Wadudi, umma uje nasihika,
Naye kafanya juhudi, Uislamu wawika,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Muhammad nuru njema, katushushia Rabuka,
Tena kwetu ni Rehema, hana wa kufananika,
Mtume mwenye hekima, na sifa za kutosheka,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Muhammad hakuacha, Islamu kumeguka,
Waziwazi hakuficha, kutupa mwanga haraka,
Katufundisha kumcha, Rabi anayepasika,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Muhammad kiigizo, tumwige pasi kuchoka,
Ametuletea nguzo, tano zinahesabika,
Halali na makatazo, humo hayakufichika,
Umefikatwakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Kumbukumbu nzuri kwake, ni ibada kuzishika,
Wanaume Wanawake, tuzingatie mipaka,
Mipaka tusiivuke, Mwenyezi akaudhika,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Tama twaomba Rabia, mjaze nyingi baraka,
Maswahaba wake pia, wape ya kunufaika,
Nasi tuongoze njia, ya kwenda pa kuongoka,
Umefika twakumbuka, uzawa wa Muhammad.
Kassim Miraji,
S.L.Posta 25578,
DARE SALAAM.
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia
wasiwasi
AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA
WANAFUNZI WA KIKATOLIKI
Na Mwandishi wetu, Morogoro
Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa
Na Mwandishi wetu
AN-NUUR kwenye Internet
Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia
alivyosilimu
Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani
Na. Kassim Juma
Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania
dini yake
Na. Ali Njuki
MAKALA: Zanzibar na tamasha la filamu
Na Said Mzee
'Waislamu wenye sisa kali'
Na. Ustaadh A. S. Fundi
MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu
- 2
Ustaadh Khamis Suleyman Nassoro, Usangi, Mwanga -
Kilimanjaro
Pongezi hizi za nini?
Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane
Na Paskal Msemakweli
BARUA YA WAZI KWA WABUNGE
Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya
Z'bar
Na Mwandishi Wetu
Da’awa Handeni yashika kasi
Na Ibn Muhammad
Kongamano la vijana wa
Kiislamu Masjid Nuur Dar
Na Mwandishi Wetu
Mafunzo ya Quran
Barua za wasomaji
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
Habari za Madrasa
Masomo
Chakula na Lishe
|