AN-NUUR
Na.159 Rabi' Awal 1419, Julai 24 - 30, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani

Na. Kassim Juma

Wito umetolewa kwa baadhi ya waalimu wa madrasa Jijini kuacha tabia ya kuwatuma wanafunzi wao kuzunguka mitaa mbali mbali kwa lengo la kuomba pesa zinazodaiwa kuwa za ujenzi na uendelezaji wa madrasa hizo.

Wito huo umetolewa na Waislamu kadhaa waliofika ofisi za gazeti hili wiki hii kueleza hisia zao kuhusiana na hali iliyoshamiri hivi sasa Jijini.

Akizungumza kwa uchungu baada ya kuwaona watoto kadhaa wa madrasa wakiwa wamebeba visanduku wakipita mitaani katikati yaJiji,Ustaadh Mahmoud mkazi wa Ilala amesema tabia hiyo sio nzuri na inaaibisha Uislamu.

Aidha Ustaadh huyo amesema kwamba amefadhaishwa mno kuwaona watoto wenye umri kati ya miaka minane (8) na 15 wakiranda mitaani huku wakiwa wamebeba visanduku vichwani.

Ameongeza kusema kuwa visanduku hivyo vilivyofungwa kwa kufuli vina matundu juu yake ambayo wachangiaji hutumbukiza pesa kupitia humo.

Imeelezwa kuwa baada ya makusanyo ya pesa ya siku nzima, visanduku hivyo hupelekwa kwa waalimu ambao imedaiwa kuwa ndiyo wenye funguo za kufuli hizo.

Katika waraka ambao ameuandika kuelezea jambo hili na ambao nakala yake aliiwasilishwa gazeti hili, Ustaadh Mahmoud ameileza hali hiyo kuwa ni ya kuudhalilisha Uislamu na kwamba hadhani kama wazazi wa watoto hao wanafahamu lolote.

"Parents bring their children to madrassa to have them educated and teachers accept them for that purpose", ameandika ustaadh huyo kwa lugha ya Kingereza akiwa na maana kwamba wazazi huwapeleka watoto wao madrassa ili wakapate elimu na walimu huwapokea watoto hao kwa lengo hilo.

Akizungumzia taabu wanazozipata watoto hao katika zoezi hilo la ukusanyaji wa pesa, ustaadh Mahmoud amezitaja kuwa ni pamoja na kutembea umbali mrefu juani kupitia maduka mengi iwezekanavyo.

Amesema kuwa watoto wanafanya kazi hiyo nzito huku wakiwa na njaa, kiu na uchovu hali ambazo ameeleza huathiri afya zao, masomo na tabia kwa ujumla.

Ustaadh Mahmoud amesema katika utafiti wake kuhusu jambo hili amegundua kwamba pamoja na ugumu wa zoezi hilo makusanyo hayo huambulia kiasi kidogo sana cha pesa ambacho hakizidi shilingi 1500 kwa siku.

Ustaadh Mahmoud amewataka Waislamu hususan wale wenye wasaa wa mali kuchangia ili kuboresha madrasa sambamba na kuwawezesha waalimu kuendesha maisha yao.

"Waalimu wanabuni mbinu hizi ili kuwawezesha kuhudumia vyema madrasa zao, tusimamishe hali hii kwa kupeleka michango na sadaqa zetu kila mara, amesisitiza Ustadh huyo.

Aidha ameiomba Juwakuta itayarishe orodha ya madrassa zote Jijini ili watakaokuwa tayari kutoa sadaqa na michango wasipate ugumu na ili iweze kufika kwa walengwa kwa urahisi.

Vile vile amekitaka chombo hicho kiwe na utaratibu wa kutembelea madrasa mara kwa mara ili kujua maendeleo yaliyofikiwa na matatizo yanayozikumba.

Juu 
 

YALIYOMO
 
 

TAHARIRI 

Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia wasiwasi 

AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA WANAFUNZI WA KIKATOLIKI 
Na Mwandishi wetu, Morogoro 

Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa 
Na Mwandishi wetu 

AN-NUUR  kwenye Internet 

Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia alivyosilimu 

Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani 
Na. Kassim Juma 

Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania dini yake 
Na. Ali Njuki 
 
MAKALA: Zanzibar na tamasha la filamu
Na Said Mzee

'Waislamu wenye sisa kali'
Na. Ustaadh A. S. Fundi 

MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu - 2
Ustaadh Khamis Suleyman Nassoro, Usangi, Mwanga - Kilimanjaro

Pongezi hizi za nini?

Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane 
Na Paskal Msemakweli

BARUA YA WAZI KWA WABUNGE

Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya Z'bar
Na Mwandishi Wetu

Da’awa Handeni yashika kasi
Na Ibn Muhammad

Kongamano la vijana wa Kiislamu Masjid Nuur Dar
Na Mwandishi Wetu

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)

Habari za Madrasa 

Masomo 

Chakula na Lishe 
 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita