|
|
|
Serikali ijibu tuhuma hizi Wiki iliyopita gazeti hili liliripoti juu ya hali ya wasiwasi iliyojitokeza mjini Morogoro baada ya wananchi kuona nakala ya barua inayowaagiza wakuu wa shule za msingi kupeleka majina ya wanafunzi Wakatoliki kwa Mkurugenzi wa Elimu. Wasiwasi wa wananchi hao umejengeka juu ya dhana kwamba huenda agizo hilo likawa linahusiana kwa namna moja au nyingine na mitihani ya darasa la saba inayotarajiwa kufanywa hivi karibuni. Kabla ya tukio hili Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu lilikuwa limemwandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kuhoji kuwepo taarifa kwamba Kanisa Katoliki lina Tume ya Mageshi ya vita, mpaka leo Mhe. Waziri Bw. Ali Ameri hajajaaliwa kupata fursa ya kujibu. Lakini jingine ni kwamba agizo hili la Mkurugenzi wa Elimu kwa waalimu wakuu (ambalo limetekelezwa bila kuhoji) linakuja wakati ndio kwanza Waislamu wanarejea kutoka maziarani (Makaburini) kuwazika wenzao waliopigwa risasi pale Mwembechai baada ya Paroko wa Kanisa Katoliki kuikemea na kuiagiza Serikali iwachukulie hatua wale aliodai kwamba wanamtukana Yesu. Aidha agizo hilo limekuja huku wananchi wakishuhudia Kadinali Pengo kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki nchini akipewa ulinzi, na itifaki ya kiserikali katika ziara zake mikoani. Yote haya kwa ujumla wake yanakuja katika mazingira ambayo tayari yapo malalamiko toka kwa Waislamu kwamba wamedhulumiwa na kunyimwa haki zao; lakini pia yanatokea katika mazingira ambayo tayari utafiti na machapisho ya wataalamu mbali mbali kama yale ya Dk. John Sivalon yanaonyesha kwamba Kanisa Katoliki lina hadhi ya pekee katika serikali kiasi kwamba wakati mwingine ni vigumu kutofautisha lipi ni la kanisa na lipi ni la Serikali. Hayapo mengi ya kusema juu ya hali hii; lakini labda kukumbusha tu kwamba vikao rasmi vya chama vilikaa na vyombo vya habari kuzua zogo Waziri mmoja ambaye ni Marehemu sasa alipotoa dokezo kwamba mfumo wa elimu uchunguzwe kuona ni kwanini sehemu moja ya jamii inaonekana kuwa nyuma. Aliitwa mdini na kuandamwa. Wakati wakiyatafakari yote haya, wanasubiri ufafanuzi, maelezo, majibu na kauli ya serikali. Wakati wamekumbwa na wasiwasi juu ya hatma ya watoto wao walio katika shule za msingi, tunarejea kauli yetu kwamba Waislamu wameuliwa na wauaji wapo mtaani hawajakamatwa. Watoto, wazee na mama zao wameteswa na kudhalilishwa, wahusika hawajafikishwa mahakamani au kuwajibishwa. Maadhali Serikali yetu imedai kwamba haina dini haimdhulumu wala kumuonea mtu na kwamba ni Serikali ya Uwazi na Ukweli inayofuata sheria. Sifa zote hizi zinalazimisha kuwepo kwa Tume ya uc hunguzi juu ya madai ya Waislamu na wale waliowaua Waislamu wakamatwe wafikishwe mahakamani. |
Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia wasiwasi AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA
WANAFUNZI WA KIKATOLIKI
Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa
Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia alivyosilimu Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani
Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania
dini yake
'Waislamu wenye sisa kali'
MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu
- 2
Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane
Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya
Z'bar
Da’awa Handeni yashika kasi
Kongamano la vijana wa
Kiislamu Masjid Nuur Dar
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|