|
|
|
Wasiwasi wazidi kutanda Moro
Na Mwandishi Wetu, Morogoro Agizo la Ofisi ya Elimu ya Manispaa ya Morogoro linalowaagiza walimu wakuu wa Shule za Msingi watume majina ya wanafunzi Wakatoliki wa darasa la saba, limeendelea kuibua wasiwasi na hisia tofauti miongoni mwa wananchi nchini. Wananchi wengi wamekuwa wakihoji ni kwanini ofisi hiyo ya elimu iagize majina ya wanafunzi wa dhehebu moja. Nini lengo na kwanini agizo hilo litolewe katika kipindi hiki ambacho wanafunzi wa darasa la saba wanakaribia kufanya mitihani yao ya mwisho. Mzazi mmoja mwenye mtoto anayesoma Shule ya Msingi Mtawala alisema lau kama agizo au ombi hilo lingetoka kwa padri au askofu kusingekuwa na sababu ya kuwa na wasiwasi; lakini akasema kwamba inapokuwa ni ofisi ya elimu ambayo huhudumia wanafunzi wote bila kujali dini zao, inajenga dhana mbaya. Mzazi mwingine ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini alishtuka kuiona nakala ya barua hiyo ambayo nakala zake zimesambazwa karibu maeneo yote mjini hapa. Mzazi huyo ambaye mtoto wake anasoma Shule ya Msingi Misufini amesema kwamba japo mtoto wake anafanya vizuri sana katika masomo lakini ashaanza kuwa na wasiwasi. Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba zoezi hili si mara ya kwanza kufanyika, bali hufanyika kila mwaka inapofika nyakati kama hizi. Waalimu Wakuu wengi waliohojiwa na gazeti hili walikataa majina yao na hata shule zao kutajwa gazetini walikiri kuwepo kwa agizo hilo lakini wakadai kwamba hawajui majina hayo yanaagizwa kwa lengo gani. Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Mlimani (Forest juu) alidai kutokujua jambo hilo na akashtuka sana alipooneshwa nakala ya barua hiyo. Hata hivyo mwalimu mkuu wa shule nyingine iliyopo katika Manispaa hii alimwonyesha Mwandishi wa habari hizi barua hiyo ndani ya faili(file) lake. Alipoulizwa kwamba majina hayo yametakiwa kwa lengo gani alijibu kwamba hajui na yeye alichofanya ni kutekeleza agizo la mwajiri wake. Baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba katika shule za msingi Msamvu, Mafiga, Mtawala, Misufini na Mlimani waliohojiwa juu ya jambo hili walikiri kuwepo kwa zoezi hilo. Katika baadhi ya shule wamesema Mwalimu amekuwa akiita majina na kuuliza dini ya kila mmoja ambapo wale wakatoliki majina yao yamekuwa yakiandikwa. Baadhi ya wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka jana ambao walihojiwa na mwandishi wa habari hizi walikiri kwamba waliwahi kufanyiwa zoezi hilo. Kutokana na hali ya mtafaruku ambayo inaendelea katika Manispaa ya Morogoro juhudi za kuwaona wahusika kuzungumzia suala hili zimekuwa zikikwama kwa namna moja au nyingine. Katika miaka ya hivi karibuni kimetolewa kitabu ambacho kimeeleza kwamba yapo mahusiano ya Karibu sana baina ya Kanisa Katoliki na Serikali ambayo hufanya matendo, msimamo na uamuzi wa Viongozi wa Serikali ufanane na mwelekeo wa Kanisa. Ni hivi karibuni pia Baraza kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu limehoji kuwepo kwa habari kwamba Kanisa hilo lina Tume ya Majeshi ya Vita. Kutokana na hali hiyo Wananchi wamefikia kudai
kwamba upo ushirika usioeleweka baina ya Serikali na Kanisa hilo.
|
Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia wasiwasi AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA
WANAFUNZI WA KIKATOLIKI
Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa
Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia alivyosilimu Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani
Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania
dini yake
'Waislamu wenye sisa kali'
MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu
- 2
Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane
Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya
Z'bar
Da’awa Handeni yashika kasi
Kongamano la vijana wa
Kiislamu Masjid Nuur Dar
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|