AN-NUUR
Na.161 Rabiul Thani 1419, Agosti 7-13, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Duniani kwa ufupi
  

Qur’an katika lugha ya Kipanjapi 

New Delh, India 

TAFSIRI mpya ya Qur’an tukufu kwa lugha ya Kipanjapi imezinduliwa nchini India, Juni 28, mwaka huu. 

Tafsiri hiyo yenye kurasa 1240 ilizinduliwa na Rais wa Jamaat Islami, Maulana Sirajul Hassan katika sherehe fupi iliyohudhuriwa na watu kadhaa mashuhuri wa mjini Malerkota mkoani Punjap. 

Kwa mujibu wa ripoti kutoka nchini India, kazi ya kutafsiri Qur’an katika lugha hiyo iliwachukua wafasiri miaka mitano kuweza kuikamilisha. 

Tafsiri hiyo mpya ya Qur’an itafahamika kwa jina la Qur’an Majeed Anuwad Te Sankhep Teeka Sahiit. 

Miongoni mwa waliopewa nakala za mwanzo (Complimentary) za tafsiri hiyo ni bwana Surjeeta Singh Barnala, waziri wa kilimo na ushirika wa India. 
 

Semina kuhusu uongozi wa Kiislamu 

Kuala, Lumpur. 

Chuo Kikuu cha Kiislamu nchini Malaysia, kitaandaa semina ya siku kumi kuhusu uongozi wa Kiislamu. 

Lengo la Semina hiyo itakayaoanza Agosti 15 mwaka huu, imeelezwa kuwa ni kutoa mafunzo ya uongozi na uendeshaji wa kazi ya Da’awah. 

Miongoni mwa waalikwa wa semina hiyo ni pamoja na wafanyabiashara na wanaharakati wa Kiislamu sehemu mbalimbali. 

Mwenyekiti wa semina hiyo atakuwa Prof. Dk. Hassan Omar Kasule. 
 
 

Mkutano wa Kiislamu 

Teheran, Iran. 

Mkutano mkubwa utakaojadili umoja miongoni mwa Waislamu duniani, utafanyika mjini Teheran nchini Iran kuanzia Julai 10 hadi 12 mwakani. 

Katika mkutano huo zitawasilishwa mada mbali mbali ambazo zote zitalenga kwenye umoja na mshikamano wa Waiislamu duniani kote. 

Baadhi ya mada hizo zimetajwa kuwa ni pamoja na kanuni za msingi za Uislamu, ufufuo, hadhi na utu wa mwanaadamu, mageuzi ya kijamii na utatuzi wa migogoro. 

Islamic Volice. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI  

Waislamu hawatokubali kusingiziwa mambo 
Na Mwandishi wetu 

Serikali ya Sudan yadhamiria kuleta amani ya kudumu 
Na Mwandishi Wetu 

Mwalimu alaumiwa kuwashawishi watoto waingie ulokole 
Na Badru Kimwaga 

Wanawake Arusha watakiwa kutafuta elimu 
Na Habiba Swedi, Arusha 

Tamsa Tanga yapata viongozi wapya 
Na Masoud Mohamed 

Mjue Dr. Abuu Ameena Philips: Mwanaharakati aliyewasilimisha askari 3000 wa Amerika 

Duniani kwa ufupi 

Barua ya Ofisa Elimu ina agenda nyuma yake 
Na Mussa Ally Morogoro 

Nabii Isa Mwana wa Maryamu ni Yesu huyo huyo!! 

Kuanzishwa ‘Islamic Club’ ni ajenda ya siri inayoweza kuhatarisha amani Tanzania 

Agenda ya siri 
Na. Hassan Kimangale 

Hatua ya Rais kutengua uteuzi wa Parole ni ya kizalendo 
Na J. R. Msuya 

Serikali iwahurumie raia wake 
Na BADRU KIMWAGA  

Wanawake  Waislamu  Wilayani Masasi waanzisha Jumuiya 
Na Yousouf  S. Kayungilo, Masasi 

Kuhifadhika kwa mwanamke ni kuhifadhika kwa jamii 
Na Zuhra Tajiri 

Waislamu  wekezeni kwenye kheri -Mwinyi 
Na Mwandishi Wetu, Tanga 

Biashara ya ufuska yavamia Z’bar Polisi uchwara’ wanufaika 
Na Rajab Rajab 

Asimamishwa uongozi kwa kutoa fat’wa ya Hitma 
Na Nadhiru Ishengoma Wetu , Kahama 

Aqswa waazimia kufuata Qur’an na Sunna 
Na Mwandishi Wetu 

Mafunzo ya Quran  

Barua za wasomaji  

Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)  

Masomo  

Chakula na Lishe  
  

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita