AN-NUUR
Na.161 Rabiul Thani 1419, Agosti 7-13, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Serikali ya Sudan yadhamiria kuleta amani ya kudumu 

Na Mwandishi Wetu 

Serikali ya Sudan imesema kwamba ni nia yake kufanya kila iwezalo kuleta amani ya kudumu Kusini mwa Sudan. Aidha imesema kwamba inasikitishwa sana na hali mbaya ya njaa na huduma nyingine za kijamii inayowakabili wananchi katika baadhi ya maeneo Kusini mwa Sudan. 

Akiongea na waandishi wa habari ofisini mwake Agosti 5, Balozi wa Sudan nchini Bw. Kuol Alor amesema kwamba hali ya watu katika baadhi ya maeneo Kusini mwa Sudan ni ya kutisha. Amesema baadhi ya watu wanakufa kwa ajili ya njaa. Hali hii mbaya amesema ni matokeo ya vita vinavyoendelea kati ya majeshi ya serikali na waasi wa SPLA. 

Ni kwa kuzingatia hali hiyo Balozi Kuol Alor amesema kwamba ufumbuzi wa tatizo hilo hauwezi kupatikana kama hakuna usimamishwaji wa vita katika eneo lote na wakudumu. 

Kwa kuzingatia wajibu wake kwa wananchi wake; serikali ya Sudan; imetoa tangazo la kusimamisha vita na kuitaka SPLA nayo ifanye hivyo hivyo ili kuwanusuru wananchi wa Sudan wanaoteseka. Amesema kwamba kusimamisha vita kwa wakati huu mazungumzo ya amani yakiendelea huko Ethiopia ni kutilia nguvu azma yake na umakini wake katika mazungumzo hayo ili kuleta amani ya kudumu. 

Ujumbe wa Serikali ya Sudan katika mazungumzo hayo unaongozwa na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Dk. Mustafa Othman Ismail wakati ule wa SPLA unaongozwa na mmoja wa makamanda wake wa ngazi za juu kabisa. 

Wakati juhudi za mazungumzo ya amani yakiendelea katika nyakati tofauti toka serikali ya Hassan El Bashir kushika madaraka; juhudi pia zimekuwa zikifanyika kuandaa katiba mpya. Bw. Alor alisema kwamba katiba hiyo ilijadiliwa na wananchi wa Sudan waliondani na hata wale wanaoishi nje ya Sudan na kisha kupigiwa kura ambapo ilipitishwa kwa 96.7% ya kura na kusainiwa na Rais Juni 30, 1998. 

Kwa mujibu wa katiba hiyo Balozi Kuol Alor amesema kwamba wananchi wa Kusini wana haki ya kuamua baada kipindi cha mpito cha mika minne, kuamua ama kubaki kama sehemu ya Sudan au kujitenga. Na kwamba uamuzi huo utafikiwa kwa njia ya kura ya maoni (referandum). 

Akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua endapo kuna nguvu kutoka nje zinazochangia kudumu kwa vita hivyo; Balozi Alor alisema kwamba ni wazi kama kusingekuwa na nguvu kutoka nje SPLA isingeweza kudumu katika vita hivyo. Hata hivyo hakuitaja nchi yoyote wala jinsi nchi za nje zinavyohusika. 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI  

Waislamu hawatokubali kusingiziwa mambo 
Na Mwandishi wetu 

Serikali ya Sudan yadhamiria kuleta amani ya kudumu 
Na Mwandishi Wetu 

Mwalimu alaumiwa kuwashawishi watoto waingie ulokole 
Na Badru Kimwaga 

Wanawake Arusha watakiwa kutafuta elimu 
Na Habiba Swedi, Arusha 

Tamsa Tanga yapata viongozi wapya 
Na Masoud Mohamed 

Mjue Dr. Abuu Ameena Philips: Mwanaharakati aliyewasilimisha askari 3000 wa Amerika 

Duniani kwa ufupi 

Barua ya Ofisa Elimu ina agenda nyuma yake 
Na Mussa Ally Morogoro 

Nabii Isa Mwana wa Maryamu ni Yesu huyo huyo!! 

Kuanzishwa ‘Islamic Club’ ni ajenda ya siri inayoweza kuhatarisha amani Tanzania 

Agenda ya siri 
Na. Hassan Kimangale 

Hatua ya Rais kutengua uteuzi wa Parole ni ya kizalendo 
Na J. R. Msuya 

Serikali iwahurumie raia wake 
Na BADRU KIMWAGA  

Wanawake  Waislamu  Wilayani Masasi waanzisha Jumuiya 
Na Yousouf  S. Kayungilo, Masasi 

Kuhifadhika kwa mwanamke ni kuhifadhika kwa jamii 
Na Zuhra Tajiri 

Waislamu  wekezeni kwenye kheri -Mwinyi 
Na Mwandishi Wetu, Tanga 

Biashara ya ufuska yavamia Z’bar Polisi uchwara’ wanufaika 
Na Rajab Rajab 

Asimamishwa uongozi kwa kutoa fat’wa ya Hitma 
Na Nadhiru Ishengoma Wetu , Kahama 

Aqswa waazimia kufuata Qur’an na Sunna 
Na Mwandishi Wetu 

Mafunzo ya Quran  

Barua za wasomaji  

Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)  

Masomo  

Chakula na Lishe  
  

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita