|
|
| Wanawake
Arusha watakiwa kutafuta elimu
Na Habiba Swedi, Arusha MWALIMU wa akina mama katika Madrasatul-Hidaya ya mjini hapa (Arusha), Ustadha Maryam Salim Ally, amewashauri Wanawake wa Kiislamu nchini kutafuta elimu ili kupata radhi ya Mwenyezi Mungu Aliyasema haya alipokuwa katika mahojiano ya ana kwa ana na mwandishi wa habari hizi alipomtembelea katika madrasatul-Hidaya, iliyopo kijijini Ererai kata ya Sombetini, Wilaya ya Arusha mjini. Aliendelea kusema kuwa, akinamama wa Kiislamu, wanayasahau majukumu yao kutokana na ukosefu wa elimu ya dini yao. Katika kutoa ushauri huo, Ustadha Maryamu amesema kwamba ni kwa njia ya elimu tu, ndipo akina mama wataweza kujenga mioyo ya dini na hivyo kulea familia katika maadili mazuri ya dini ya Kiislamu. Amefafanua kwamba, hata kama mama anahangaika na utafutaji riziki kwa familia yake, na kwamba utafutaji huo ni mgumu, bado mama huyo anashauriwa kutenga japo saa moja ya kujielimisha.Ustadha Maryamu aliongeza kuwa, hata Mtume Muhammad (s.a.w.) zama zake, alitoa da’awa huku akihangaika kutafuta riziki. Aliasa kuwa; riziki ya mja inatolewa na Mwenyezi Mungu, na lau kama inapatikana kwa taabu tena kidogo kidogo, mama asikate tamaa. "Ajibidiishe kuitafuta riziki hiyo huku akimwamini mola wake kuwa atamfungulia, na imani hii itamjia mama huyu, endapo tu ana elimu ya dini", alisema Ustadha Maryam. Alimalizia kwa kuzidi kutoa ushauri kuwa; elimu ya dini yake, itamfanya
mama wa Kiislamu, kukabiliana na madhila yote yaliyopo katika jamii, na
hatoyumbishwa juu ya jambo lolote; kwani ndani ya Qur’ani kunapatikana
kila kitu, akiwa na maana kuwa, Qur’ani ni mwongozo na akaongeza kuwa ufafanuzi
unapatikana pia katika hadithi za Mtume (s.a.w.).
Tamsa Tanga yapata viongozi wapya Na Masoud Mohamed JUMUIYA ya wanafunzi wa Kiislamu Tanzanhia (TAMSA) mkoa wa Tanga imepata uongozi mpya baada ya ule wa zamani kumaliza muda wake mwezi uliopita. Uongozi huo ulipatikana katika mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika tarehe 28 Julai kwenye Shule ya Sekondari ya Jumuiya. Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa kwa kina ni pamoja na uimarishaji wa somo la maarifa ya Kiislamu na mavazi ya heshima (hijaab) mashuleni. Kutokana na kukosekana kwa ushirikiano kutoka BAKWATA; TAMSA imeazimia kufikia malengo yake kwa kushirikiana na Jumuiya ya Waalimu wa Kiislamu Tanga (JUWAKITA) badala yake. Akitoa nasaha zake amiri wa JUWAKITA; Ustadh Khamis Hussein Shemtoi, alipongeza taratibu za kudumisha vikao vya kikatiba vya TAMSA. Hili alisema linaendana na agizo la Qur’an (3:159) ambalo linahimiza "Shuura". Pia aliwataka viongozi wapya wa TAMSA kuwa wasimamizi wazuri wa wenzao kuhakikisha wanasoma na kufaulu vizuri. Waliochaguliwa ni: (1) Ustadh Sudi Ahmed (Shule ya Popatlal) - Mwenyekiti (2) Ustadh Chambuso R. Ramadhani (Jumuiya Sec.) M/kiti Msaidizi (3) Ustadh Ali Abbasi (Popatlal) - Mweka Hazina (4)Ustadh Athman Ibrahim (Usagara) - Katibu Mkuu (5) Ustadh Ali Seif) (6) Ustadh Kaimu Mwanjia) (Si wanafunzi) - Makatibu watendaji.
|
Waislamu hawatokubali kusingiziwa
mambo
Serikali ya Sudan yadhamiria kuleta
amani ya kudumu
Mwalimu alaumiwa kuwashawishi watoto
waingie ulokole
Wanawake Arusha watakiwa
kutafuta elimu
Tamsa Tanga yapata viongozi
wapya
Mjue Dr. Abuu Ameena Philips: Mwanaharakati aliyewasilimisha askari 3000 wa Amerika Barua ya Ofisa Elimu ina agenda nyuma
yake
Nabii Isa Mwana wa Maryamu ni Yesu huyo huyo!! Kuanzishwa ‘Islamic Club’ ni ajenda ya siri inayoweza kuhatarisha amani Tanzania Agenda ya siri
Hatua ya Rais kutengua uteuzi wa
Parole ni ya kizalendo
Serikali iwahurumie raia wake
Wanawake Waislamu Wilayani
Masasi waanzisha Jumuiya
Kuhifadhika kwa mwanamke ni kuhifadhika
kwa jamii
Waislamu wekezeni kwenye
kheri -Mwinyi
Biashara ya ufuska yavamia
Z’bar Polisi uchwara’ wanufaika
Asimamishwa uongozi kwa kutoa
fat’wa ya Hitma
Aqswa waazimia kufuata Qur’an
na Sunna
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|