AN-NUUR
Na.161 Rabiul Thani 1419, Agosti 7-13, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Wanawake Waislamu Wilayani Masasi waanzisha Jumuiya

Na Yousouf S. Kayungilo, Masasi 

WANAWAKE wa Kiislamu mjini Masasi wameanzisha jumuiya yao kwa lengo la kukutana pamoja na kujifunza ili kuzijua kikamilifu haki zao zilizobainishwa na Allah (SWT) katika Qur’an kupitia Mtume (s.a.w.) na kuepuka propaganda za ki-taghoot zinazoenezwa ulimwengu mzima kwa kivuli cha maazimio ya mkutano wa Beijing kuhusu haki za wanawake na kudai usawa. 

Aidha, wanawake hao wametoa wito kwa wanawake Waislamu kote nchini kushikamana na mwongozo sahihi wa Uislamu na kuepuka propaganda hizo zenye lengo la kuwakufurisha wanawake wa Kiislamu. 

Katika tamko lao baada ya masomo yao ya jioni wamehoji kwa kusema hao wanaojiita watetezi wa usawa na haki za wanawake mbona matatizo yakiwapata wanawake wa Kiislamu hawainua midomo yao kusema chochote? Na kuongeza kuwa haki za wanawake wa Kiislamu zimebainishwa vizuri katika Qur’an na Sunah sahihi ya Mtume (s.a.w.), hivyo kamwe hawakubali kuyumbishwa, na kwamba ni jukumu la wanawake wote nchini kushikamana na mwongozo huo kikamilifu ili kuzijua haki zazo. 

Aidha, wamesema, wanawake wengi kwa kupuuza kwao mwongozo wa Uislamu, wamekuwa wakiishi kinyume kabisa na Uislamu, kama kutembea uchi, kushiriki maonyesho ya urembo, kujiuza miili yao kwenye mabaa, madanguruo, n.k. Sasa jukumu lao ni kuzinduka na kujielimisha kama Qur’an na Hadithi za Mtume (s.a.w.) zinavyosisitiza; wamesisitiza wanawake hao. 

Wanawake hao wa mjini Masasi wametoa pongezi zao kwa vikundi vya akina mama Waislamu wa Songea, Iringa, Morogoro, Dar es Salaam, Tanga, Dodoma na Mwanza kwa jitihada zao za kumkomboa mwanamke wa Kiislamu, na wametoa wito kwa wanawake wa Kiislamu wa mikoa mingine kuiga mfano huo. Pia wamepongeza juhudi za viongozi wa Al-Azizu Islamic Centre kwa ushauri wao mzuri ambao umefanikisha kuanzishwa kwa jumuiya yao nchini ya Taasisi ya Al-Azizu Islamic Centre. 

Jumuiya hiyo ya akinamama wa Kiislamu Masasi imewasihi Masheikh wetu kuwa wasiziminye ndimi zao kwa kubainisha sheria ya Allah (SWT) na kumfumbia macho adui wa Allah anayepinga kutekelezwa sharia yake katika jamii. Aidha, wamesema, Masheikh wetu wasitoe msisitizo wao mkubwa katika kuwatii masheikh, mawalii na masharifu tu wakati wanaiacha jamii ya Kiislamu inateketea kwa kukosa nafasi katika nyanja muhimu. 

Wakisisitiza nasaha yao wamesema, Masheikh wauweke Uislamu mbele ya kitu kingine chochote, wasijiweke vifua mbele kuwa vigingi vya kuzuia kusimama kwa Uislamu, wafahamu wao ni binadamu, mauti yapo mlangoni kuwapeleka akhera, huko hakuna zaidi ila pepo na moto, hakuna yeyote atakayenufaika na cheo chake, ila ucha Mungu wake. Hivyo ni bora kwao historia iwakumbuke kama watetezi wa Uislamu kuliko historia kuwakumbuka kama vikwazo vya maendeleo ya Uislamu. 

Aidha, wamesema wana muunga mkono Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Sheikh Omar Bafadhil kwa msimamo mzuri aliouonyesha wa kutetea haki za Uislamu na Waislamu, na kuwataka masheikh wote wa mikoa kuiga mfano huo mwema wa kutokuwa na woga katika kusema ukweli. 

Mwisho wametoa wito kwa mashirika ya Kiislamu ya ndani na nje ya nchi na wafadhili binafsi kuwasaidia ili kuimarisha umoja wao, pamoja na shughuli za ki-da’wa pia wana mipango ya kujishughulisha na shughuli za kijamii ili kujiletea maendeleo yao kama kushona, kufuma, n.k. hivyo wenye nia ya kuwasaidia mashine za kushonea, kufuma, kudarizi, n.k.Wanawakaribisha.si. 

Waliochaguliwa kuiongoza jumuiya hiyo nikama ifuatavyo:- 

Mwenyekiti -Bi. Halima Hassan, M/Kiti Msaidizi - Bi. Shadida Suleiman, Katibu -Bi. Asiya Hassan, Katibu Msaidizi - Bi Amina Maiwa, *Mtunza Hazina - Bi. Fadina Awadh, Mtunza Hazina Msaidizi - Bi. Rahma Millanzi. 

 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI  

Waislamu hawatokubali kusingiziwa mambo 
Na Mwandishi wetu 

Serikali ya Sudan yadhamiria kuleta amani ya kudumu 
Na Mwandishi Wetu 

Mwalimu alaumiwa kuwashawishi watoto waingie ulokole 
Na Badru Kimwaga 

Wanawake Arusha watakiwa kutafuta elimu 
Na Habiba Swedi, Arusha 

Tamsa Tanga yapata viongozi wapya 
Na Masoud Mohamed 

Mjue Dr. Abuu Ameena Philips: Mwanaharakati aliyewasilimisha askari 3000 wa Amerika 

Duniani kwa ufupi 

Barua ya Ofisa Elimu ina agenda nyuma yake 
Na Mussa Ally Morogoro 

Nabii Isa Mwana wa Maryamu ni Yesu huyo huyo!! 

Kuanzishwa ‘Islamic Club’ ni ajenda ya siri inayoweza kuhatarisha amani Tanzania 

Agenda ya siri 
Na. Hassan Kimangale 

Hatua ya Rais kutengua uteuzi wa Parole ni ya kizalendo 
Na J. R. Msuya 

Serikali iwahurumie raia wake 
Na BADRU KIMWAGA  

Wanawake  Waislamu  Wilayani Masasi waanzisha Jumuiya 
Na Yousouf  S. Kayungilo, Masasi 

Kuhifadhika kwa mwanamke ni kuhifadhika kwa jamii 
Na Zuhra Tajiri 

Waislamu  wekezeni kwenye kheri -Mwinyi 
Na Mwandishi Wetu, Tanga 

Biashara ya ufuska yavamia Z’bar Polisi uchwara’ wanufaika 
Na Rajab Rajab 

Asimamishwa uongozi kwa kutoa fat’wa ya Hitma 
Na Nadhiru Ishengoma Wetu , Kahama 

Aqswa waazimia kufuata Qur’an na Sunna 
Na Mwandishi Wetu 

Mafunzo ya Quran  

Barua za wasomaji  

Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)  

Masomo  

Chakula na Lishe  
  

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita