|
|
|
Na Badru Kimwaga WAZAZI kadhaa wa watoto wasomao masomo ya ziada (tuisheni ) kwa mwalimu mmoja huko Mburahati, wamemlalamikia mwalimu huyo kutokana na tabia yake ya kuwashawishi watoto hao kubadili dini au dhehebu kumfuata mwalimu huyo ambaye ni Mlokole. Wakiongea na gazeti hili Jijini juzi, wazazi hao kwa nyakati tofauti wamesema kuwa mwalimu huyo anayejulikana kwa jina moja tu la Dan, anayefundisha kwa sasa katika kanisa la Assemble of God la Mburahati Barafu, huwa akiwalazimisha watoto hao ambao husoma shule za msingi kubadili dini zao kutoka Uislamu hadi Ukristo au kutoka dhehebu jingine na kuwa Mlokole kwa maneno ya ushawishi. Mmoja wa mzazi ambaye mtoto wake alikumbwa na vishawishi vya mwalimu huyo na kubadili dhehebu, Bwana Andrew Thomas, amesema kuwa mwalimu huyo ambaye hajulikani anafundisha shule gani Jijini, alimfanya mwanae Catherine mwenye umri wa miaka kumi na tatu aliye darasa la 6 kubadili dhehebu kutoka Roman . Catholic (RC) na kuwa mfuasi wa Assemble of God, maarufu kwa jina la Walokole. Amesema kuwa yeye kama mzazi wa mtoto huyo amechukizwa na tabia ya mwalimu huyo ambaye mara ya kwanza alikuwa anafundisha tuisheni katika maeneo ya karibu na Uwanja wa KIFA, kando ya Baa ijulikanayo kwa jina la Fontane, iliyoko huko Mburahati. Mzazi huyo na mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Mama Sikitu alidai pia hata mtoto wake Bakari Mohamed anayefundishwa na mwalimu huyo, alishawahi kumuelezea jinsi Mwl. huyo anapomaliza kufundisha masomo ya tuisheni, huanza kuwapa sera za Okoka uokolewe na damu ya Yesu, ambapo ni kinyume na makubaliano ya ufundishaji wa tuisheni hizo. Hata hivyo uchunguzi wa gazeti hili kwa muda wa wiki moja uliweza kung’amua kuwa huyo anayedaiwa kuwa Mwalimu (yaani Dan, haijulikani kama ni Dunstan au Daniel) hana taaluma ya ualimu, isipokuwa ni mhitimu wa elimu ya sekondari . Mwaka 1995 na 96 alikuwa anafundisha wanafunzi wa sekondari huku akisubiri matokeo ya mtihani wake wa Kidato cha Sita. Baada ya Majibu kutoka na matokeo kuwa mabaya wanafunzi hao walimkimbia. Inasemekana baada ya matokeo hayo alianza kufundisha wanafunzi wa shule za msingi, baada ya wale wa sekondari kumkimbia na ndipo alipoanza kuwarai watotowaingie dini au madhehebu yake, . Mwandishi wa habari hizi alifika eneo linalodaiwa kutumiwa kwa "Tuisheni"
hiyo, hata hivyo hakuweza kuwasiliana na mwalimu huyo kwa kile kilichoelezwa
na wahusika wa mahala hapo kwamba huwa hapatikani nyakati za mchana
|
Waislamu hawatokubali kusingiziwa
mambo
Serikali ya Sudan yadhamiria kuleta
amani ya kudumu
Mwalimu alaumiwa kuwashawishi watoto
waingie ulokole
Wanawake Arusha watakiwa
kutafuta elimu
Tamsa Tanga yapata viongozi
wapya
Mjue Dr. Abuu Ameena Philips: Mwanaharakati aliyewasilimisha askari 3000 wa Amerika Barua ya Ofisa Elimu ina agenda nyuma
yake
Nabii Isa Mwana wa Maryamu ni Yesu huyo huyo!! Kuanzishwa ‘Islamic Club’ ni ajenda ya siri inayoweza kuhatarisha amani Tanzania Agenda ya siri
Hatua ya Rais kutengua uteuzi wa
Parole ni ya kizalendo
Serikali iwahurumie raia wake
Wanawake Waislamu Wilayani
Masasi waanzisha Jumuiya
Kuhifadhika kwa mwanamke ni kuhifadhika
kwa jamii
Waislamu wekezeni kwenye
kheri -Mwinyi
Biashara ya ufuska yavamia
Z’bar Polisi uchwara’ wanufaika
Asimamishwa uongozi kwa kutoa
fat’wa ya Hitma
Aqswa waazimia kufuata Qur’an
na Sunna
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|