NASAHA
Na. 050 Jumatano Mei 31 - Juni 5, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Tahariri 
S.L.P. 72045, Simu: 0811 - 600145, Dar es Salaam
 

Tahadhari ya Warioba juu ya rushwa isipuuzwe 

Jaji Joseph Sinde Warioba akiongea katika Chuo Kikuu cha Dar es Saaam hivi karibuni aliItuhumu serikali kwa kuzembea katika suala zima la kupambana na rushwa iliyokithiri hapa nchini.

Alisema kuwa hatua zinazochukuliwa na serikali katika vita vyake dhidi ya rushwa ni za shabaha ya mbali na matokeo yake ni rushwa kupamba moto katika jamii ya Watanzania na akaonya kuwa nguvu za kupambana na rushwa zisipoelekezwa kwenye kuwasafisha viongozi wa juu nchi itabakia katika nadharia na propaganda zisizokwisha juu ya kupambana na rushwa.

Kauli hiyo ya Jaji Warioba imekuja wakati ambapo jamii ya Watanzania imeathiriwa vibaya na rushwa kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya Taifa hili.

Tanzania hivi sasa inaongoza kwa kuwa ya tatu kwa rushwa miongoni mwa nchi za Kiafrika na ya saba katika dunia.

Athari ya kukithiri huko kwa rushwa inaonekana waziwazi katika nyanja mbali mbali za maisha ya Watanzania ambapo huduma mbali mbali kama vile za afya, elimu, ajira na sekta nyinginezo hutolewa kwa rushwa.

Kauli ya Jaji Warioba kuwa wengi wa viongozi huingia madarakani kwa kutoa rushwa katika chaguzi mbalimbali kuanzie zile za udiwani, uwakilishi na hata ubunge, inaibua hisia zaidi za wananchi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, ya kupatikana viongozi bomu na wasio waadilifu na wenye kula rushwa ambao hawataweza kupambana na rushwa kwa vitendo zaidi ya maneno.

Ni jukumu na wajibu wa wananchi kuitilia maanani tahadhari ya Jaji Warioba juu ya kuwa macho na wale wenye kuingia madarakani kwa kutoa rushwa.
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Tahadhari ya Warioba juu ya rushwa isipuuzwe

Mkapa afanya ziara Pwani

CCM ‘inaweweseka’ - Sheikh

Zanzibar wadai kuyumbishwa na Bara

Serikali yatoa muelekeo wa Bajeti na kutangaza njaa

Habari za ndani
Wapinzani kusimamisha mgombea Urais mmoja 

SMZ haishughulikii mikarafuu -Maalim Seif

Mwalimu Mkuu Msimbazi Mseto atishia kujiuzulu 

Hizi ni 'arobaini' za mapandikizi

Waislamu Mbeya wamsusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA 

Masheikh wa BAKWATA waongoza sherehe za kuwasimika makamanda wa vijana wa CCM 

Wakristo waishitukia CCM

MAKALA
Dini na siasa haviwezi kutenganishwa

Makala 
Mikutano ya Prof. Lipumba 'yaendelea' baada ya kuondoka 

MPASHO NASAHA
MATATA! MATATA!

Kalamu ya Mwandishi 
Wapinzani epukeni patupu 

MAKALA
CCM na sera za maendeleo (6)

Habari za Kimataifaza Kimataifa

Lishe 
Supu na umuhimu wake mwilini

BARUA

MASHAIRI

RIWAYA
Mapinduzi ya fikra - 4 

MICHEZO

  • Uchaguzi Yanga Julai
  • BATA yahimiza usajili michezo
  • 'Simba SC, Singida United baba mmoja mama mbali mbali' 
  • Tarimba akalia Kuti Kavu Yanga
  • Ambari, Mwakipesile wajitosa kugombea DRFA

  •  


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita