NASAHA
Na. 049 Jumatano Mei 24 - 30, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Lishe

Unachotakiwa kufanya kabla ya kuweka chakula kwenye jokofu



CHAMOS, H.J

Kila kitu kina mipangilio yake. Na kwa kila chenye mipangilio ni muhali kukosa matayarisho. Ili uwezo kupata mafanikio unayotarajia, huna budi kujiandaa vyema. Iwapo unahitaji kuhifadhi vyakula vyako kwenye jokofu, ufuatao ni muhtasari wa matayarisho. Unapokuwa tayari na vyakula mezani, ndio kwanza unataka kupanga kwenye jokofu ni vyema ukazingatia yafuatayo.

Kwanza gawanya vyakula katika makundi tofauti. Bila shaka vyakula vyako vitakuwa si vya aina moja bali ni aina mbalimbali. Kila chakula kina ladha na harufu totauti. Kuna vyenye mafuta na visivyokuwa navyo. Hivyo basi ni lazima vyakula vyako uvitenganishe sawasawa. Mathalani, nyama, samaki, dagaa kuwa kundi moja. Mboga za majani na matunda, maziwa, maji ya matunda na vyakula vya makopo. Kundi la mwisho ni viungo vibichi kama vile vitunguu saumu, tangawizi n.k. 

Kuna vyakula vinaweza kufyonza harufu ya vyakula vingine mfano maziwa iwapo vitachanganywa. Ndio maana tunasisitiza kutenganisha. Ama baada ya kutenganisha, vyakula visafishwe kulingana na makundi yake. Jaribu kutotumia maji mara mbili. Mfano maji yaliyooshea matunda kuoshea mboga za majani, si katika mpangilio unaofaa. Kila kundi lijitegemee. Vyakula visafishwe kwa uangalifu mkubwa kwa kuzingatia kuwa, baada ya kuhifadhiwa hakitaoshwa tena, bali kupikwa au kuliwa moja kwa moja.

Baada ya kusafisha vyakula viweke katika kiasi kinachowekeka. Mfano huwezi kuweka mguu mzima wa ng’ombe bila kukatakata. Zoezi hili lifanyike bila kuchanganya makundi yaliyokwisha tengwa. Utakapo katakata vizuri, itasaidia kuhifadhi vyakula vingi zaidi kuliko kuweka shagalabagala katika ukubwa au udogo usio na uwiano. Kwa vyakula ambavyo vitapikwa tena, vikatwekatwe kwa saizi itakayotumika wakati wa mapishi. Kama nilivyowahi kueleza huko nyuma, vyakula vilivyotolewa kwenye jokofu huharibika haraka. Hivyo basi ni vizuri kuandaa kabisa ili chakula kisibaki nje muda mrefu kabla ya kupikwa.

Kwa mboga za majani itategemea na aina. Mathalani mchicha ni bora ‘uchambuliwe’ kwanza na kuwekwa kwa kiasi unachotaka (kumbuka kukatakata mchicha au mboga za majani baada ya kuosha). Ama mboga mboga zingine kama bamia, karoti, njegere, biringanya n.k. vinaweza kuwekwa bila ya kukatakata. Kumbuka kuwa kukatakata kuna kifanya chakula kiweze kupoteza virutubisho haraka zaidi kuliko vile ambavyo havijakatwa. Na kuzuia kwake kunahitaji uangalifu mkubwa. Kwa sababu hiyo ni vyema kukatakata vyakula vile tu ambavyo vinaulazima huo na si kila chakula.

Hatua inayofuata ni kufungasha (packing). Vyakula ambavyo tayari vimekatwa katwa na vipo katika makundi vipakiwe kwenye vyombo, mifuko au vifaa vyovyote vilivyotayarishwa kayari kwa kazi hiyo. Iwapo unahitaji chakula chako kidumu muda mrefu zaidi, ndivyo itakavyokuhitaji ufungashe vizuri zaidi. Vyakula vinaweza kudumu hata miezi 6-12 kulingana na uhifadhi wako. Fungasha kulingana na makundi ambayo tayari umeyapanga. Vifurushi viwe katika ujazo ambao utatumika kwa chakula hicho kitakapohitajika. Kuna aina nyingi za vifaa vitumikavyo kufungashia vyakula. Cha msingi ni kuwa kifaa hicho kisiweze kutoboka na kioneshe chakula kilichopo ndani yake. Hii itakurahisishia kuona unachohitaji badala ya kupekuapekua. Harufu za vyakula zinaweza kusafiri kutoka chakula kimoja hadi kingine. Ili kuzuia hili, fungasha kwa uangalifu ili kuzuia harufu kusambaa. Vifuko vya kuwekea vyakula ni vizuri iwapo vitakuwa vya rangi tofauti tofauti. Hii husaidia kutofautisha vyakula kwa urahisi.

Mara baada ya kufungasha, panga vyakula vyako vizuri kulingana na muda wa kuhifadhi. Vitakavyo tumiwa muda mfupi vikae chini kwenye baridi ya kati. Iwapo jokofu lako lina milango miwili pamoja na vichumba viwili, tumia chumba kimoja kwa ajili ya vyakula vitavyotumika karibuni na kingine kwa ajili ya vyakula vitavyotumika baadaye sana. Mlango wa chumba chenye vyakula vya muda mrefu, usifunguliwe mara kwa mara. Kumbuka kupanga kulingana na makundi uliyotenganisha.
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
KERO katika Elimu ziondolewe haraka

Chuo Kikuu Dar wafanya mitihani katika Bwalo la chakula

Udini wa CCM utaisambaratisha nchi -Tambwe

‘Kutoweka’ kanda ya Kakobe: CCM yatuhumiwa

Maalim Seif awaambia Wazanzibari: Wenye mamlaka ya kumuweka mtu Ikulu ni wananchi

Mkapa afurahia maendeleo Pwani

Wapinzani wajiimarisha Moro

‘Zawadi’ ya Uchaguzi yatishia kusambaratisha taasisi ya Kiislam Tanga

Serikali yakemea mwanamke kudhalilishwa

Ushauri Nasaha
Umuhimu wa kushirikiana na majirani katika malezi ya watoto

MAKALA
Afande Mahita, wananchi hatutaki Dola ya kipolisi

Makala
CCM hawawezi kuondoa umasikini, ndio tegemeo lao

Kalamu ya Mwandishi
Makubaliano kwa vitendo Z'bar

MAKALA
CCM na sera za maendeleo (5)

Makala
Wanawake na maendeleo: Je ni wimbo wa kuchaguliwa?

Makala
CCM inatawala badala ya kuongoza

Habari za Kimataifa

RIWAYA
Mapinduzi ya fikra -4

Lishe
Unachotakiwa kufanya kabla ya kuweka chakula kwenye jokofu

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Raza kufungua mashindano ya Wavu Zanzibar
  • Real Madrid yaota Ubingwa  leo
  • Kajumulo asema Yanga timu ya Wananchi

  •  


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita