|
Na. 049 Jumatano Mei 24 - 30, 2000 |
|
|
|
|
|
S.L.P. 72045, Simu: 0811 - 600145, Dar es Salaam KERO katika Elimu ziondolewe haraka
KERO mbali mbali zinazoikabili sekta ya elimu nchini zinahitaji juhudi za makusudi za Serikali na wananchi ili kuziondoa vinginevyo taifa litaangamia. Imeripotiwa wiki hii kwamba elimu katika mkoa wa Pwani ni duni ambapo shule kadhaa za msingi hazijawahi kutoa wanafunzi wanaofaulu kwenda sekondari za serikali kwa karibu miaka 20 tangu zilipoanzishwa. Aidha, imeelezwa kuwa matokeo hayo yanachangiwa na mazingira duni watoto wanaposomea, walimu kukosa mishahara yao kwa zaidi ya miezi sita, na walimu hao kuishi katika nyumba ambazo hazina mwanga. Kama kwamba hayo hayatoshi, tunaambiwa kwamba hivi sasa kuna walimu zaidi ya 1500 ambao hawajalipwa mishahara yao tangu waajiriwe mwaka jana. Sambamba na hali hiyo kero sasa zinapanda kutoka shule za msingi na sekondari na kufika katika vyuo vikuu. Wiki hii baadhi ya wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, sehemu ya Mlimani, wamekuwa wakifanyia mitihani yao ya kumaliza mwaka na wengine kuhitimu shahada za katika bwalo la chakula. Hali hii inatokana na hatua ya Serikali kuongoza idadi ya wanafunzi chuoni hapo kila mwaka, wakati miundo mbinu haiongezeki kwa idadi sawa na ongezeko la wanafunzi. Mpaka sasa baadhi ya wanafunzi wa Kitivo cha Uhandisi wamesimamishwa masomo baada ya ugomvi kati yao na wanafunzi wenzao wa Kitivo cha Sheria. Inadaiwa kuwa sakata hilo linatokana na hatua ya wanafunzi wa Kitivo cha Sheria kutumia madarasa ya Kitivo cha Uhandisi. Tukiutazama mwendo huu kwa makini na bila ya mapenzi ya vyama vya siasa, tutaona kwamba taifa letu linaelekea pabaya, ambapo kero katika sekta ya elimu zinaongezeka kila kukicha. Kwa hiyo, tunaiomba serikali na wananchi kwa ujumla kuziondoa kero mbali mbali katika elimu. |
YALIYOMO
TAHARIRI
Chuo Kikuu Dar wafanya mitihani katika Bwalo la chakula Udini wa CCM utaisambaratisha nchi -Tambwe ‘Kutoweka’ kanda ya Kakobe: CCM yatuhumiwa Maalim Seif awaambia Wazanzibari: Wenye mamlaka ya kumuweka mtu Ikulu ni wananchi Mkapa afurahia maendeleo Pwani ‘Zawadi’ ya Uchaguzi yatishia kusambaratisha taasisi ya Kiislam Tanga Serikali yakemea mwanamke kudhalilishwa Ushauri Nasaha
MAKALA
Makala
Kalamu ya Mwandishi
MAKALA
Makala
Makala
RIWAYA
Lishe
|
|
|
|
|