AN-NUUR 
Na.177 Shaaban  1419, Novemba 27 - Desemba 3, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Historia: Form IV 

Uendeshaji wa Serikali ya Kiislamu wakati wa Makhalifa 

Ngome na kambi za jeshi zilijengwa katika sehemu mbali mbali, majengo ya ofisi na ya kukaa wafanyakazi mikoani na wilayani zilijengwa, Baitul mal yalijengwa majengo madhubuti, majela pia yalijengwa. Pamoja na majengo haya mabarabara na madaraja nayo yalijengwa. Visima na vituo kadhaa baina ya Makka na Madina vilijengwa. miji nayo ilianzishwa. Maarufu ni Basra, Kufa, Fustat na Mosal.40 

14. Ulinzi na usalama 

Katika Dola ya Kiislamu wakati wa ukhalifa wa Makhalifa wanne ulinzi uliimarishwa kwa kiwango kikubwa. Wakati wa Mtume (s.a.w.) hakukua na kambi za kwa ajili ya Jeshi. Kila mtu alikuwa askari na vita ilipofika Waislamu walijitokeza wakapewa mafunzo na kwenda vitani. Ni kweli pia kuwa katika dola ya Kiislamu kila muumin ni askari wa Allah na wakati wowote anapotakiwa ni lazima ajitoe kupigania Dini ya Mwenyezi Mungu: 

"Enyi mlioamini Je! Nikujulisheni Biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo? Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na piganieni dini ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu... (61:10 - 11). 

Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waislamu nafsi zao na mali zao ili nae awape pepo. Wanapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu wanauwa na wanauwawa... (9:111). 

Ni dhahiri Muislamu ni askari wa Mwenyezi Mungu. Pamoja na hivi tangu wakati wa Khalifa wa pili Umar liliundwa jeshi kama yalivyo majeshi ya kileo. Khalifa ndie aliyekuwa mkuu wa majeshi aliteua kamanda wa jeshi na makamanda wa mikoa na wilaya. Ndani ya jeshi kulikuwa na vyeo mbali mbali. Kama vile "Arief" aliyekuwa mkuu wa askari kumi. Qaid au Lieutenent alikuwa mkuu wa askari mia moja. Wanawake walishiriki kwenye vita kazi zao zilikuwa kutoa huduma kuwahudumia majeruhi kwa kufunga vidonda, n.k. na mara chache walishiriki katika mapigano. 

Askari walikuwa wa farasi na wa miguu. Askari wa farasi walitumia silaha za mikuki, majambia. Walivaa kofia za chuma na vazi la chuma. Askari wa miguu walivaa joho linalovuka magoti kwenda chini, suruali na viatu. 41 Silaha zao zilikuwa mikuki, midogo midogo, majambia, pinde, mshale na ngao. Kila askari alikuwa akinunua vifaa vyake na wale wasioweza walinunuliwa na serikali. Vifaa vingine vilivyotumika wakati huo ni Manjaniq, 42 Dababa 43 na Zaboor.44 

Idara ya ulinzi ilipoanzishwa askari wote waliorodheshwa na utaratibu wa mshahara na posho ulianza kutumika kwa askari wa kudumu, wakujitolea na wale waliopigana vita vya awali kama Badr, Uhud, n.k., walipewa posho. 

Kiulinzi nchi iligawiwa kwenye maeneo ya kiulinzi, makao makuu ya maeneo hayo yakawa Madina, Kufa, Basra, Mosul, Fustat, Damaskas, Hems. Jordan na palistine.45 Katika sehemu zote hizi kambi zilijengwa kwa ajili ya askari. Mashamba ya mifugo yalipanuliwa kwa matumizi ya farasi na ngamia wa vita. 

Pamoja na askari wa farasi na wa miguu jeshi la maji lilianza wakati wa ukhalifa wa uthman. Vita vya kwanza vya majini vilipiganwa na Muawiya alipoivamia Cyprus mnamo mwaka wa 28 A.H. Makao makuu ya jeshi la maji yalikuwa Alexandria Misri. Wanamaji wa Kiislamu walisaidia kuimarisha ulinzi wa dola ya Kiislamu. 

Usalama wa Taifa na ujasusi 

Idara hii nayo ilikuzwa. Ilianza tangu wakati wa Mtume (s.a.w.) na kuendelezwa wakati wa makhalifa wanne. Walitumika wanajeshi na wasio wanajeshi katika kazi ya kupata habari ndani na nje ya Dola na hasa kujua mwenendo wa adui. Wapo Machief kwa mfano Syria waliochagua wana usalama wao kuchunguza mwenendo wa Warumi. Wapalestine lilikuwepo kundi la Wayahudi lililojulikana kwa jina la Samara, lililojizatiti katika upelelezi. Khalifa Umar aliweka wapelelezi ndani ya jeshi ili apate habari zote. Hivyo idara hii nayo ilisaidia sana katika ulinzi na usalama wa Dola wa kiislamu. 

Hivi ndivyo serikali ya Kiislamu ilivyoendeshwa - kwa ufupi Serikali ya Kiislamu iliyoendeshwa kwa muda wa miaka 40 kuanzia kwa Mtume (s.a.w.) hadi makhalifa wake wanne iliweka misingi ya uendeshaji wa serikali zote za leo Duniani. Pamoja na kubadili misingi lakini mambo mengi yameazimwa kutoka katika misingi ya Serikali ya Kiislamu 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 

Tahariri
Hii siyo Demokrasia ni fedheha

Urambo wamlilia Profesa Lipumba
Na Mwandishi Wetu

Sheikh aridhia Waislamu kubatizwa
Na Rajab Rajab, Morogoro

Zanaki kupiga marufuku Hijab?

Uongozi Masjid Qadiria waitwa Polisi kuhojiwa

Wakazi wa Mbagala Msalabani kuishitaki Tume ya Jiji

Wasemavyo wanaharakati

Akhera ipo, makafiri ni wakadhibishaji
Na Abubakar Marwilo

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo ni mgumu
Na Elia Batendi

Aina ya maudhi yaliyoharamishwa juu ya Muislamu

PAROLE:   Rais kasusa au hana ubavu?
Na Bisura Waziri Nyello

Serikali ikithamini kilimo
Na Abdallah Ahmad Seif

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 3
Na Ustaadh Kupa Pazi Said

Madrasa Arrijalu Muswallin Damba

Ijue Madrasat Fauzia - Kibondo

Waislamu  Kondoa waanza kupokea misaada ya ujenzi wa Msikiti, Madrasa
Na Abu Zubeir, Dodoma

Waislamu Dodoma wasali sala ya Ghaib kwa marehemu Kilima na mkewe

Songea kujenga shule ya sekondari

Wanafunzi wa Bihawana Dodoma wamshukuru Alhaj Ismail Dawood

Mashindano ya kusoma Qur’an yafanyika Kondoa

Waislamu wautazame upya mfumo wao wa elimu

Ujenzi wa Chuo cha Kiislamu Shamsiya Bereko wakwama

Kesi ya kushambulia kituo yaahirishwa tena

Polisi waondolewa kimya kimya Mwembechai

Msikiti wa Kiwanja cha Ndege wapania kujenga shule

Sayansi na Teknolojia
[Kwenye Kompyuta RAM ni kitu gani?]

Mafundisho ya Quran

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Madini ya chuma]

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita