|
Mashairi
AN-NUUR mjumbe mwema
AN-NUUR yako miali, baidi inafikia,
Wasomaji mbalimbali, nuru waifurahia,
Imekuwa ni muhali, ulivyo kukuchukia,
Ndugu umeniungia, An-Nuur mjumbe mwema.
Wewe ni mjumbe mwema, kwenye kheri waitia,
Wamekwitika kauma, kwako twakutanikia,
Mfano wa itiswama, tunapo pa kushikia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Umeutoa uwanja, nasi tukauingia,
Humo tunakuta hoja, fahamu zenye kutia,
Unajengeka umoja, na imani kutwingia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Awali sikuwajua, hata nao kwangu pia,
Kurasa tumefunua, ndani tukakutania,
Humo tukayavumbua, mengi ya kutufalia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Jicho halijawaona, wao wamenandikia,
Korogwe si mbali sana, bali sijapafikia,
Huko amepatikana, ndugu wa kunililia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Mwingine yuko Kigoma, na huko napasikia,
Nimepata ndugu mwema, dini ndio kaingia,
Baruaye nimesoma, An-Nuur kanikutia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Mpanda siachi kutaja, nimewahi kuingia,
Yuko kakangu wa haja, jichoni sijamtia,
Tumejuana pamoja, gazetini kupitia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Na Tabora pia wako, ndiko nilikoanzia,
Nawajua walioko, ndugu walojaa nia,
Huja kwangu maandiko, salamu kunitumia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Hata wa Darisalama, kuliko na Tanzania,
Gazeti wanolisoma, na nakishi kulitia,
Wapo wanipao hima, na tungo kuzipitia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Na Mwanza wamenijua, shule nilikopitia,
AN-NUUR meniinua, salamu nazipokea,
Na nasaha nachukua, na dua kuitikia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Bali na hapa jirani, si mbali kupafikia,
Ni Mwadui mgodini, Maganzo unapitia,
Nimepata ikhiwani, AN-NUUR likiwa “via”,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
AN-NUUR ifanye kazi, usije ukalegea,
Kazi zako twazienzi, na dua twakuombea,
Metutoa usingizi, mbele tunaelekea,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
AN-NUUR kama jahazi, mawimbi watukatia,
Hodari wako ujuzi, “kona” unazipatia,
Kukudhuru hawawezi, Mola atakukingia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
AN-NUUR yaseme wazi, yakiukayo sharia,
Madhalimu uwakhizi, waipendao dunia,
Japo wanayo mavazi, uchi wapate bakia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
AN-NUUR siyamalizi, hapa ninasimamia,
Ya kwako mambo azizi, thamani yamezidia,
Wa witiri mwenye enzi, azidi kukupa njia,
Ndugu umeniungia, AN-NUUR mjumbe mwema.
Jihad R. Saballa,
S.L.P. 347,
Shinyanga.
Ilaniwe Marekani
Laden anahimiza, “Sratwa” Mustaqima,
Ile inayo-ongoza, kwenye mwisho Akrama,
Iweje mwamgombeza, na kumvisha shutuma?
Hastahiki lawama, ilaniwe Marekani.
Mtu akitetea haki, gaidi mnasema!
Wangapi mabaramaki, na mliwafata nyuma?
Walianzisha mikiki, dunia ikatetema,
Laden hana lawama, ilaniwe Marekani.
Kutekeleza za Mungu, sheria ziwe za Toma!
Mwanzo wa huu ukungu, amanikuwa kilema,
Hayapungui majungu, kisha huzidi dhulma,
Laden hana lawama, ilaniwe Marekani.
Mwapuuza maagizo, Mola aliyoyasema,
Mnafata makatazo, mfano watu wa zama,
Huu ukubwa uozo, mwatukosesha ghanima,
Laden hana lawama, ilaniwe Marekani.
Wana hila Marekani, dunia wameiduma,
Nyote mko ujingani, kwa hizo zao ndarama,
Mjue huko mbeleni, adhabu yawaandama,
Laden hana lawama, ilaniwe Marekani.
Siko nanyi mie aka, mi’kando nimesimama,
Maaluni Amerika, siwashiriki daima,
Mimi namcha Rabuka, natii anavyosema,
Laden hana lawama, ilaaniwe Marekani.
Hapa nimegota tasa, namba yenye heshima,
Nafata mila ya Musa, na huyo Ibrahima,
Na Muhammadi hasa, Utume ndiye hatima,
Laden hana lawama, ilaniwe Marekani.
Na Bin Laden,
Magori Chriss (Chifu Jaji)
S.L.P. 61402,
Dar es Salaam.
|
YALIYOMO
Tahariri
Hii siyo Demokrasia ni fedheha
Urambo wamlilia Profesa Lipumba
Na Mwandishi Wetu
Sheikh aridhia Waislamu
kubatizwa
Na Rajab Rajab, Morogoro
Zanaki kupiga marufuku Hijab?
Uongozi Masjid Qadiria waitwa Polisi
kuhojiwa
Wakazi wa Mbagala Msalabani
kuishitaki Tume ya Jiji
Wasemavyo wanaharakati
Akhera ipo, makafiri ni wakadhibishaji
Na Abubakar Marwilo
Mdahalo kati ya Waislamu na
Wakristo ni mgumu
Na Elia Batendi
Aina ya maudhi yaliyoharamishwa
juu ya Muislamu
PAROLE: Rais kasusa
au hana ubavu?
Na Bisura Waziri Nyello
Serikali ikithamini kilimo
Na Abdallah Ahmad Seif
Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto
wadogo - 3
Na Ustaadh Kupa Pazi Said
Madrasa Arrijalu Muswallin Damba
Ijue Madrasat Fauzia - Kibondo
Waislamu Kondoa waanza
kupokea misaada ya ujenzi wa Msikiti, Madrasa
Na Abu Zubeir, Dodoma
Waislamu Dodoma wasali sala ya
Ghaib kwa marehemu Kilima na mkewe
Songea kujenga shule ya sekondari
Wanafunzi wa Bihawana Dodoma
wamshukuru Alhaj Ismail Dawood
Mashindano ya kusoma Qur’an yafanyika
Kondoa
Waislamu wautazame upya mfumo
wao wa elimu
Ujenzi wa Chuo cha Kiislamu
Shamsiya Bereko wakwama
Kesi ya kushambulia kituo yaahirishwa
tena
Polisi waondolewa kimya
kimya Mwembechai
Msikiti wa Kiwanja cha Ndege
wapania kujenga shule
Sayansi na Teknolojia
[Kwenye Kompyuta RAM ni kitu gani?]
Mafundisho ya Quran
Masomo ya Dini ya Kiislamu
Barua za Wasomaji
Mashairi
Chakula na lishe
[Madini ya chuma]
|