AN-NUUR 
Na.177 Shaaban  1419, Novemba 27 - Desemba 3, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Uongozi Masjid Qadiria waitwa Polisi kuhojiwa
 
  • Waituhumu nchi kuendeshwa Kikristo
  • Wasema wimbo wa Taifa, dua ya Bunge ni maandiko ya Kikristo
UONGOZI Masjid Qadiria uliopo Mburahati Mzambarauni ulipelekewa barua ya kuitwa kituo cha Polisi Magomeni Novemba 17, mwaka huu, kufuatia kufanyika muhadhara msikitini hapo. Kutokana na kutokuwepo uongozi wa kudumu msikitini hapo waumini kadhaa walijitolea kwenda kituo cha Polisi Magomeni tarehe Novemba 18, mwaka huu ili kuitikia wito. 

Katika mahojiano yaliyofanyika kituoni hapo ilidaiwa kwamba kuna muhadhara wa kashfa unaokashifu dini nyingine katika msikiti huo na pia muhadhara huo unachanganya dini na siasa. 

Waumini walikanusha madai hayo na kusema kwamba muhadhara huo unatangaza dini ya Kiislamu kwa kusoma vitabu vinne vya Allah (s.w.). 

Kuhusu kuchanganya dini na siasa waumini hao waliiomba Polisi kabla ya yote iwathibitishie kama nchi hii ni ya Kikristo au la kwa sababu wimbo wa Taifa ni wimbo wa Kikristo uliomo katika kitabu cha Kikristo kiitwacho "Chuo kidogo cha sala na nyimbo, wimbo huo umo katika ukurasa wa 86 katika kitabu hicho", walidai huku wakionyesha hicho kitabu, na kuongeza kwamba, pia dua ya kuliombea Bungeni dua ya Kikristo ambayo imo katika ukurasa wa 12 wa kitabu hicho hicho. 

Kutokana na hali hiyo mashtaka yalibadilishwa likaja shtaka la kufanya muhadhara bila kibali. Waumini hao waliachiwa huru kwa sharti kwamba wakitoka kuendelea na muhadhara watafute kibali hata kama ni msikitini kutokana na sababu za kiusalama. 



Wakazi wa Mbagala Msalabani kuishitaki Tume ya Jiji 

BAADHI ya wakazi wa eneo la Mbagala Msalabani huenda wakaishitaki Tume ya Jiji kwa madai ya kuwaingilia katika makazi yao na kuweka alama za kubomolewa nyumba bila ridhaa zao; na makubaliano. 

Kutokana na maelezo kamili ya baadhi ya wahusika wa maeneo hayo wakazi hao wanatakiwa kuhama makazi hayo kwa sababu imedaiwa ni mali ya Kanisa Katoliki (Catholic Secretariat) jambo ambalo wakazi hao wanalipinga. 

Wamesema kuwa, kuwepo kwa Msalaba katika eneo lao sio sababu ya kuwa si eneo lao, na kuwa ni mali ya "Catholic Secretariat", kwani Msalaba huo umekuwepo tangu mwaka 1932, zama za Wajerumani. Baadae eneo lilirudishwa kwa serikali katika miaka ya 1960. 

Baada ya Uhuru Serikali ililirudisha eneo hilo na kwamba wakazi hao walikuwa wanapatumia kama bustani. Wakazi hao wa sasa wanasema kuwa wao wapo hapo kwa muda mrefu . 

Wamesema kwamba Kanisa limeanza kufuatilia eneo hilo tangu mwaka 1994 na kuanza kazi ya upimaji wa viwanja hivyo. walipohojiwa ni kwa nini wanachukua hatua ya kuishtaki Tume ya Jiji muda huu na si tokea mwanzo wa mgogoro huo walisema kuwa mwanzo walikutana na uongozi na kuahidiwa kupatiwa fidia, lakini cha ajabu ni kwamba mpaka hii leo hawajapewa chochote wala viwanja. 

"Tumeandikiwa barua ya kutuamuru kuondoka, katika eneo hili bila ya kuonyeshwa wapi pa kwenda", walisema. 

Aidha, walidai kwamba waliambiwa wafuatilie malipo pamoja na viwanja kwa Mkurugenzi wa Jiji wa Kanda ya Temeke lakini kila wakifuatilia anasema ana kazi nyingi. 

Pia wakazi hao wamedai kwamba walifika kwa Afisa Ardhi Wilaya Temeke ambaye aliwajibu kuwa yeye hana nakala ya kuwaamuru waondoke na kuwaambia waende Makao Makuu ya Jiji wamuone alie waandikia barua hiyo. 

Eneo hilo lenye mgogoro linakaliwa na Waislamu watupu na kuna madrasa na miti ya Matunda (miembe, midizi n.k.). 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 

Tahariri
Hii siyo Demokrasia ni fedheha

Urambo wamlilia Profesa Lipumba
Na Mwandishi Wetu

Sheikh aridhia Waislamu kubatizwa
Na Rajab Rajab, Morogoro

Zanaki kupiga marufuku Hijab?

Uongozi Masjid Qadiria waitwa Polisi kuhojiwa

Wakazi wa Mbagala Msalabani kuishitaki Tume ya Jiji

Wasemavyo wanaharakati

Akhera ipo, makafiri ni wakadhibishaji
Na Abubakar Marwilo

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo ni mgumu
Na Elia Batendi

Aina ya maudhi yaliyoharamishwa juu ya Muislamu

PAROLE:   Rais kasusa au hana ubavu?
Na Bisura Waziri Nyello

Serikali ikithamini kilimo
Na Abdallah Ahmad Seif

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 3
Na Ustaadh Kupa Pazi Said

Madrasa Arrijalu Muswallin Damba

Ijue Madrasat Fauzia - Kibondo

Waislamu  Kondoa waanza kupokea misaada ya ujenzi wa Msikiti, Madrasa
Na Abu Zubeir, Dodoma

Waislamu Dodoma wasali sala ya Ghaib kwa marehemu Kilima na mkewe

Songea kujenga shule ya sekondari

Wanafunzi wa Bihawana Dodoma wamshukuru Alhaj Ismail Dawood

Mashindano ya kusoma Qur’an yafanyika Kondoa

Waislamu wautazame upya mfumo wao wa elimu

Ujenzi wa Chuo cha Kiislamu Shamsiya Bereko wakwama

Kesi ya kushambulia kituo yaahirishwa tena

Polisi waondolewa kimya kimya Mwembechai

Msikiti wa Kiwanja cha Ndege wapania kujenga shule

Sayansi na Teknolojia
[Kwenye Kompyuta RAM ni kitu gani?]

Mafundisho ya Quran

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Madini ya chuma]

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita