AN-NUUR
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
Mafundisho ya Qur’an

Hakuna kulazimishwa kuingia katika dini


 


Aya ya 256 - 257

Ingawa neno lililotumika hapa ni Twaghuut kwa uchache lakini inapewa tafsiri ya wingi kwasababu mtu yoyote ambaye anamkanusha Allah na kuamua kuishi kwa kufuata mfumo wowote wa masiah usio Uislamu basi anakuwa mtumwa si wa Twaghuut mmoja bali Matwaghuut kadhaa wenye maumbile na hali tofuati. Kinara wa Matwaghuut ni Ibilisi ambaye humuandalia mtu huyu namna kwa namna za udanganyifu wenye mvuto wa aina yake.

Mbali na Ibilisi, Twaghuut mwingine aliyefichika kwa wegni na nafsi yake mwenyewe binadamu. Nafsi ya binadamu humfanya kuwa mtumwa na matamanio na matashi na kumuongoza kwenye kila aina ya upotofu na njia zilizokwenda upogo. Matwaghuut wengvine ni mke au mume, watoto, jamaa zake, kabila au familia, marafiki au taifa. Aidha Matwaghuu wengine ni viongozi wa kisiasa au kidini na hata serikali yake.

Wote hawa ni Matwaghuut kwa mtu mmoja huyu na kila mmoja anamvutia kwenye yale anayoyatamani yeye wakati huyu mtu anabaki kuwa mtumwa anayejidanganya kuwa ataweza kuwaridhisha wote. Ni kwasababu kama hizo Allah alisema kuwa iwapo tutawatii wengi waliomo ardhini watatupoteza aliposema:

"Na kama ukwatii wengi katika hawa waliomo ulimwenguni watakupoteza na njia ya Allah. Hawafuati ila dhana tu, na hawakuwa ila ni wenye kuzua (tu basi).(6:116).

Kinyume na hivyo anaeleza tena:

"Sema: "Hii ndiyo njia yangu, ninaita (ninalingania) kwa Allah kwa ujuzi wa kweli - mimi na wanaonifuata......(12:108).

Kwa hiyo bado tunatilia mkazo kuwa njia ya Allah (Nuru) ni moja tu ambaye aliilingania Mtume (s.a.w.) na sasa inalinganiwa wa Waislamu wa kweli siyo wale wafuasi wa Matwaghuut waliojivika vilemba na kujipachika madaraka bila ya haki.
 

Juu

YALIYOMO


TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi

Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Na Mwandishi Wetu

Wanakijiji wawapiga Polisi Olesiva
Na Mwandishi wetu, Arusha

Waislamu washinda kesi Same
Na Mwandishi Wetu, Same

Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah inahujumiwa 
Na Mwandishi Wetu

KOSOVA: Bosnia nyingine

Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin

Historia ya damu za mashujaa Afghanistan

Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata viongozi wapya
Na Suleiman Simba, Kigoma

Muhadhara wanguruma Masjid Hijaz
Na Said Shariff

Waislamu waitumie Misikiti ipasavyo
Na Ashraf Yusuph, Moshi

Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza wengi
Na Mwandishi Wetu

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 3
Na Muhibu Said

Wanawake wa Kiislamu washiriki maonyesho ya kilimo
Na Habiba Swedi

Wanawake wa Kiislamu washauriwa kupigania haki zao
Na Habiba Swedi, Arusha

Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii
Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Na Mwandishi Wetu

Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga Mungu?
Mahfudhi M. Mahfudhi

MAONI: Porojo za Ngatara -2

Zanzibar na  biashara ya utumwa
Na J. Hussein

Marekani ishitakiwe
Na Abubakar Msham

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3

Mafundisho ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe
 
 
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita