AN-NUUR
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii

Na Mwandishi Wetu

AFRICA Muslims Agency (AMA) ni shirika la kutoa huduma kwa jamii lisilo la Kiserikali (NGO) ambalo limesajiliwa nchini toka mwaka 1987.

Shirika hili ni mwanachama hai wa Baraza la Maendeleo ya Jamii Tanzania (TACOSODE) na kamati ya kitaifa inayotoa misaada wakati wa maafa (TANDRED).

Shughuli za AMA zina lenga kuboresha huduma za jamii na maendeleo kupitia miradi yake ya elimu, afya na misaada ya kibinadamu.

Awali, shirika hili lilianzishwa kama taasisi ya kuwasaidia Waislamu wa Malawi mwaka 1982, baada ya madaktari fulani kutoka Kuwait kuitembelea nchi hiyo na kushuhudia hali mbaya iliyokuwa ikiwakabili Waislamu. 

Baada ya kufanya kazi kwa miaka miwili kwa jina la Malawi Muslim Agency, shirika hilo lilipanua malengo yake na kuitazama Afrika kwa ujumla. Jina lilibadilika na kuwa Africa Muslims Agency ambapo hivi sasa lina ofisi na matawi 40 katika nchi mbalimbali za Afrika.

Kwa Tanzania, ofisi kuu ipo Jijini Dar es Salaam eneo la Tabata wakati matawi ya ofisi hiyo yapo Moshi, Tanga, Zanzibar, Morogoro, Mwanza na Mtwara.

AMA ina idara nne ambazo ni elimu, afya, huduma za jamii na programu za dharura.

Chini ya idara ya elimu kuna shule za sekondari za Alfarooq (Dar es Salaam), Kaloleni (Moshi) na Kitaya (Mtwara). Aidha, kwa mwaka 1999 zinatarajiwa kufunguliwa sekondari nyingine kadhaa ambazo ni Alkheir Centre (Mkwakwani Tanga) na An-nuur Centre (Pongwe, Tanga).

Alkheir itakuwa kwa ajili ya wasichana na wanawake watu wazima (mafunzo ya ufundi) wakati ile ya Pongwe itakuwa kwa wavulana. Shule nyingine itafunguliwa Mji Mpya Morogoro.

Pamoja na shule hizo, vipo vituo 5 vya kutoa mafunzo ya ufundi kwa akina mama. Aidha, imefunguliwa "College" ijulikanayo kama Al-Shariah College huko Zanzibar ambayo imefungamanishwa na Chuo Kikuuu cha Madina. Lengo ni kuifanya Al-Shariah kuwa Chuo Kikuu kamili katika miaka michache ijayo.

Chini ya idara ya afya kuna zahanati kadhaa zinazofanya kazi wakati nyingine zipo mbioni kufunguliwa.

Zanahati zinazofanya kazi ni pamoja na Al-Molhem Medical Centre (Tanga) Kaloleni Health Centre na Prince Saud Medical Centre.

Juhudi zinafanyika katika kuziendeleza zahanati na vituo hivyo vya afya kufuata maadili mema ambapo wanawake wana sehemu za kupatiwa huduma tofauti na wanaume huduma zikiwa sawa kwa wote.

Kituo cha Prince Saud ambacho kipo katika eneo la shule ya Al-Farooq kitafanya kazi kwa masaa 24 kikiwa na huduma za kawaida na "Ultra Sound Clinic" na huduma za "Marternity" na MSH.

Idara hii muhimu ya afya ikiongozwa na Dk Rashed E. Hamed inaendesha kambi za matibabu ya macho bure ambapo upasuaji hufanyika na miwani kutolewa bure.

Kufikia mwisho wa mwaka huu 1998 AMA inatarajia kuwa na vituo 10 vya afya.

Kwa upande wa huduma za jamii, AMA inaendesha vituo kadhaa vya kulelea yatima vyenye watoto wapatao 250. Watoto hao hupewa chakula, malazi, mavazi,matibabu na zaidi husomeshwa hadi mwisho wa uwezo wao (sekondari au Chuo Kikuu).

Pamoja na watoto wanaokaa katika nyumba rasmi za kulelea yatima wapo watoto zaidi ya 100 ambao husaidiwa chakula na mavazi wakiwa katika familia zao.

Chini ya kitengo hiki hutolewa pia misaada ya chakula na nguo katika maeneo yenye shida ya njaa na wakati wa maafa.

Aidha, husaidia kuchimba visima vya maji katika maeneo yenye shida ya maji na zaidi ya visima 600 vishachimbwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Pamoja na shughuli zote hizi, Africa Muslims Agency huwasadia waumini kujenga Misikiti. Misikiti ipatayo 50 nchini.

Wakati wa maafa kwa kushirikiana na TANDREC, AMA hushiriki kikamilifu kutoa misaada na huduma zinazohitajika kuokoa maisha ya watu.
 

Juu

YALIYOMO


TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi

Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Na Mwandishi Wetu

Wanakijiji wawapiga Polisi Olesiva
Na Mwandishi wetu, Arusha

Waislamu washinda kesi Same
Na Mwandishi Wetu, Same

Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah inahujumiwa 
Na Mwandishi Wetu

KOSOVA: Bosnia nyingine

Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin

Historia ya damu za mashujaa Afghanistan

Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata viongozi wapya
Na Suleiman Simba, Kigoma

Muhadhara wanguruma Masjid Hijaz
Na Said Shariff

Waislamu waitumie Misikiti ipasavyo
Na Ashraf Yusuph, Moshi

Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza wengi
Na Mwandishi Wetu

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 3
Na Muhibu Said

Wanawake wa Kiislamu washiriki maonyesho ya kilimo
Na Habiba Swedi

Wanawake wa Kiislamu washauriwa kupigania haki zao
Na Habiba Swedi, Arusha

Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii
Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Na Mwandishi Wetu

Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga Mungu?
Mahfudhi M. Mahfudhi

MAONI: Porojo za Ngatara -2

Zanzibar na  biashara ya utumwa
Na J. Hussein

Marekani ishitakiwe
Na Abubakar Msham

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3

Mafundisho ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe
 
 
 
 
 
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita