AN-NUUR
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
Historia ya damu za mashujaa Afghanistan


Wakati iliyokuwa Jamhuri ya Muungano wa kisovieti (USSR), ikivamia Afghanistan, Akhtar Khan, aliyekuwa mkuu wa idara ya usalama ya Pakistan (ISI), alitoa ushauri kwa Rais Zia Ul Haq ulioitaka Pakistan kusaidia vita vya msituni, vilivyokuwa vikiendeshwa na makundi ya Mujahidiin dhidi ya majeshi hayo ya uvamizi na vibaraka wake nchini Afghanistan. 

Kufuatia ushauri huo makachero wa Serikali ya Pakistan walianza kupenyezwa ndani ya urusi ambao kwa kusaidiana na vikosi vya mujahidiin, walifanya hujuma kadhaa dhidi ya vituo vya kijeshi sambamba na kushambulia miji ya Urusi iliyopo mpakani na Afghanistan. Aidha Pakistan chini ya Generali Zia iliendesha mafunzo ya kijeshi kwa wapiganaji wa kiislamu waliojitolea kuingia msituni kupambana na madhalimu hao wa kirusi wakisaidiana na vibaraka wao. 

Hata hivyo wakati Mashambulizi dhidi ya adui yakiendelea kushika kasi, Nchini Pakistan msiba mkubwa ulitokea. Ilikuwa yule yule mfadhili wa Wapiganaji hao, Rais Zia Ul Haq na mshauri wake wa mambo ya usalama bwana Akhtar Khan, walioripotiwa kufariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea wakati kiongozi huyo akiwa katika ziara ya kikazi ndani ya Pakistan.

" Ndege ya Jeshi la Anga la Pakistan C-130 ikiwa imemchukua Rais Generali Zia na baadhi ya maafisa wa ngazi za juu wa jeshi ililipuka angani na kuua wote waliokuwemo", amendika Brigedia Muhammad Yousaf mmoja wa washiriki wa vita vya Afghanistan katika kitabu chake Afghanistan’s untold story.

Ulikuwa msiba mkubwa kwa makundi ya Mujahiidin hawa wachanga, wasio na uzoefu wowote wa vita, kulinganisha na nguvu ya kutisha iliyokuwa mkabala nao.

Mauaji ya Generali Zia yalipangwa na majasusi wa CIA na KGB kwa kumtumia bwana Aslam Beg, mtu aliyekuja kushika uongozi mara tu baada ya kifo cha Rais Zia Ul Haq.

Ili kuukanganya Ulimwengu, mauaji hayo yaliwajumuisha waambata wawili wa kijeshi wa Marekani ambao walikufa sambamba na Generali Zia katika mlipuko huo.

Kutoka Marekani Maafisa wa FBI walitumwa "kuchunguza" sababu na chanzo cha mlipuko huo wa ndege uliosababisha pamoja na watu wengine, waambata wake wa kijeshi kupoteza maisha!

Hata hivyo, pengine kwa kuwa na taarifa rasmi ya kadhia hiyo FBI haikujishughulisha kabisa na kuwahoji walioshuhudia tukio hilo.

" Wingu lililozingira mauaji hayo lilitokana na ukweli kwamba Marekani ilikuwa na mkakati tangu awali wa kudhibiti Mujahidiin wasiweze kusimamisha serikali ya kiislamu nchini Afghanistan ingawa ilijitia kuwa nao bega kwa bega kuwafurusha warusi", anafafanua Brigedia Yousaf katika moja ya kurasa za kitabu chake.

Kuuawa kwa Generali Zia kulikuwa ni hitimisho la njama kadhaa zilizofanywa dhidi ya kiongozi huyo. Njama ya mwanzo ilipangwa na Mkuu wa majeshi wa Urusi wakati huo, ambaye aliona kuwa kazi ya kudhibiti Mujahidiin ingechukuwa muda mrefu iwapo ngome yao kuu( Pakistan) haitasambaratishwa.

Mkuu huyo alisuka njama kuipindua serikali ya Rais Zia Ul Haq kutokea Urusi. Alituma makachero nchini Pakistan kutega mabomu katika maduka, ndege za abiria, kuyauzia silaha ki magendo makabila yaliyokuwa yakiishi mpakani mwa nchi hizo mbili na kuchochea migawanyiko, kero zote hizo zililenga kuwaghadhibisha Wananchi wa Pakistan dhidi ya serikali ya Generali Zia hatimaye ipinduliwe. Harakati hizi hazikufanikiwa.

Kifo cha Rais Zia Ul Haq kilitoa ishara ya mapambano magumu na ya muda mrefu mbeleni yaliyokuwa yakiwakabili Mujahidiin, kwani kuchanganyikiwa kwao kulikotokana na kifo hicho kulitoa mwanya kwa Majeshi ya adui yakiwa na zana nzito nzito huku yakipata msaada wa Najibullah na vibaraka wenzake waliokuwa wakiiongoza nchi hiyo, kujichimbia barabara ndani ya Afghanistan.

Wataalamu wa masuala ya kijeshi walilielezea jaribio la Mujahidiin kutaka kupambana na Taifa hilo kubwa likiwa limejikita sawa sawa ndani ya Afghanistan, kwamba ni kichekesho cha karne hii, na isingechukuwa hata miezi mitatu kabla hawajasagiliwa mbali. 

Katika hali hiyo ya ukiwa Idara ya usalama ya ISI ikipigana nyuma ya Mujahidina, ilibeba jukumu la usafirishaji na usambazaji wa silaha na misaada mingine ya fedha na chakula kwa wapiganaji (logistics). Misaada hiyo ilitoka kwa Wahisani mbali mbali ikiwemo serikali ya Saudi Arabia.

Pasipo uratibu wa upiganaji, mipango wala mbinu madhubuti, Mujahidiin hawa wachanga walitumia silaha kufanya mashambulizi ya kushtukiza katika ngome za majeshi ya adui. Hata hivyo mashambulizi yao yalijibiwa vikali na adui kiasi cha kusababisha hasara kubwa ya mali na maisha ya watu. Mtihani mwingine uliojitokeza katika kipindi hiki kigumu, ni ule wa migogoro ya viongozi wa makundi ya wapiganaji. badala ya kusonga mbele kumkabili adui, viongozi wa makundi walianza kunyoosheana vidole hadi kufikia kuyapambanisha makundi yao katika vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Nusra ilijitokeza pale makundi hayo yalipoketi na kurejea Qur’an, hatua iliyopelekea kuundwa shuura iliyounganisha makundi saba ya Mujahidiin yaliyokuwa msituni wakati huo. 
 


Itaendelea toleo lijalo


 


Juu

YALIYOMO


TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi

Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Na Mwandishi Wetu

Wanakijiji wawapiga Polisi Olesiva
Na Mwandishi wetu, Arusha

Waislamu washinda kesi Same
Na Mwandishi Wetu, Same

Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah inahujumiwa 
Na Mwandishi Wetu

KOSOVA: Bosnia nyingine

Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin

Historia ya damu za mashujaa Afghanistan

Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata viongozi wapya
Na Suleiman Simba, Kigoma

Muhadhara wanguruma Masjid Hijaz
Na Said Shariff

Waislamu waitumie Misikiti ipasavyo
Na Ashraf Yusuph, Moshi

Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza wengi
Na Mwandishi Wetu

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 3
Na Muhibu Said

Wanawake wa Kiislamu washiriki maonyesho ya kilimo
Na Habiba Swedi

Wanawake wa Kiislamu washauriwa kupigania haki zao
Na Habiba Swedi, Arusha

Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii
Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Na Mwandishi Wetu

Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga Mungu?
Mahfudhi M. Mahfudhi

MAONI: Porojo za Ngatara -2

Zanzibar na  biashara ya utumwa
Na J. Hussein

Marekani ishitakiwe
Na Abubakar Msham

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3

Mafundisho ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe
 
 
 
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita