AN-NUUR
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
MAONI

Porojo za Ngatara -2


 


Hivi karibuni vyombo vya habari vimepasha kwamba kijana mmoja wa Kiislamu alikamatwa na polisi huko mjini Korogwe na kufunguliwa mashtaka kwa kuandika katika baiskeli yake kuwa Yesu si Mungu. Ni nini tafsiri ya kitendo hiki? Tafsiri yake ni kuwa kwa mujibu wa serikali (jeshi la polisi ni idara nyeti na muhimu katika serikali) Yesu ni Mungu! Bila shaka msimamo huu ni wa kutia mashaka makubwa kwa serikali inayojitangaza kuwa haiongozwi na dini yoyote. Msimamo huu wa serikali umetiliwa nguvu na yaliyojiri katika mhadhara mkubwa ulioendeshwa hivi karibuni Jijini na Mwinjilisti wa Kijerumani Rainhard Bonke ambao pia ulihudhuriwa na baadhi ya watu mashuhuri wakiwamo Makamu wa Rais Dk. Omari Ali Juma, mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Lt. Yusuph Makamba na mke wa Waziri Mkuu Bibi Esther Sumaye. Katika mhadhara huo tulibwagizwa kwa mapana na marefu kuwa Yesu ni Mungu wa Tanzania

Sio tu kwamba tangazo hili lilionekana kutokuwa na walakini wowote, bali lilipata baraka zote za serikali pale serikali ilipousifia mhadhara huo na kuutaja kama unaofaa kuigwa.

Sasa ni nini tunachokisoma kutoka kwenye mifano kama hii? Ni dhahiri kuwa kwa mtu yeyote ambaye atajishughulisha kutafakari na atokee kuwa na bahati ya kutoathiriwa na mafumbo ya imani, atafikia hitimisho kuwa kinachotokea ni kujaribu kulazimisha hatua kwa hatua - kwa kutumia dola, izoeleke na kukubalika hadharani kuwa Yesu ni Mungu na kwa wale ambao hawakubaliani na swala hilo walazimike kuwaonyesha msimamo huo sirini na mafichoni tu.

Tujaalie, kama Bwana Ngatara anavyoamini kuwa Tanzania ni kisiwa cha amani na kuwa serikali ya Tanzania haijifungamanishi na dini yoyote - iwe wazi wazi au kwa siri. Aidha tujaalie kuwa kila Mtanzania ana uhuru kamili wa kuamini na kuabudu kupitia dini anayotaka. Pamoja na kujaalia hayo yote bado Bwana Ngatara anatokea kuwa na ufinyu mkubwa wa utambuzi kwa kule kudai kwake kuwa ni mambo haya yanayoiwezesha Tanzania kubakia ni ‘kisiwa cha amani ndani ya bara linalokabiliwa na misuguano na migongano ya hatari ya kila aina?! Kwanza ni muhimu Bwana Ngatara akatambua kuwa msisitizo kwenye kauli yake unatoa picha potofu kuwa ni bara hili pekee ambalo kwa kiasi kikubwa linakabiliwa na migogoro na migongano. Ukweli wenyewe ni kwamba migogoro na migongano iko katika mabara takriban yote. Kwa mfano tu, Ulaya inakabiliwa na migogoro hivi sasa huko Ireland ya Kaskazini, Serbia-Kosovo, Belaruss,Ukraine, Hispania, na Cyprus. 

Huko Amerika ya Kusini wapiganaji wa Shinning Path wanaleta dhahama katika nchi za Peru, Colombia na Bolivia wakati kule Amerika ya Kaskazini wapiganaji wa Zapatista wanacharushana na serikali ya Mexico. Huko Asia nako ukiondoa mashariki ya kati bado kuna Syrilanka, Afghanistan, Jammu - Kashmir, Burma, Cambodia, Indonesia - Timor Mashariki, na bila ya kusahau hali ya kivita isiyokwisha kati ya Korea Kusini na Korea Kaskazini.

Pili, tukirejea barani Afrika ni mgogoro au mgongano hivi sasa upi ambao asili yake ni sera inayotoa kipaumble katika dini? Bila shaka Bwana Ngatara na wenzake kwa kuwa wamekaririshwa hivyo na kwa kuwa hawana uwezo wa kujua mchele ni upi na pumba ni zipi katika yale wanayoyasikia watakimbilia kuitaja migogoro inayoendelea hivi sasa kule Algeria na Sudan.

Chanzo cha mgogoro wa Algeria kinajulikana vema. Chama cha Kiislamu cha FIS kilipata ushindi kwenye uchaguzi na ushindi huo ukaporwa na Madhalimu. Kwa kuwa ni haramu kwa Muislamu Muumini kudhulumu au kukubali kudhulumiwa, basi FIS ikawapasa kufanya kile walichopaswa kufanya. Walichokifanya FIS na wanachoendelea hakitofautiani na kinachotokea hivi sasa nchini Togo. Hivi majuzi muungano wa vyama vya upinzani nchini humo umeanzisha mapambano ya silaha dhidi ya serikali ya Rais Gyadema ambaye na chama chake walidhulumu ushindi katika uchaguzi mkuu uliopita. Suala la Sudan naloliko wazi. Mgogoro kati ya waasi wa kusini mwa nchi hiyo na serikali umeanza mara tu baada ya uhuru katika miaka ya hamsini. Mgogoro huo katika sura yake ya kileo umeanzishwa na John Garang na waasi wenzake mnamo mwaka 1983 kabla kabisa ya kuingia madarakani kwa serikali ya Kiislamu inayoingoza nchi hiyo hivi sasa chini ya Generali Hassan El Bashr. Sasa katika mnyumbulisho huu suala la dini linaanzia wapi? 
 


Insha Allah tutaendelea katika toleo lijalo.


 




Juu

YALIYOMO

TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi

Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Na Mwandishi Wetu

Wanakijiji wawapiga Polisi Olesiva
Na Mwandishi wetu, Arusha

Waislamu washinda kesi Same
Na Mwandishi Wetu, Same

Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah inahujumiwa 
Na Mwandishi Wetu

KOSOVA: Bosnia nyingine

Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin

Historia ya damu za mashujaa Afghanistan

Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata viongozi wapya
Na Suleiman Simba, Kigoma

Muhadhara wanguruma Masjid Hijaz
Na Said Shariff

Waislamu waitumie Misikiti ipasavyo
Na Ashraf Yusuph, Moshi

Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza wengi
Na Mwandishi Wetu

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 3
Na Muhibu Said

Wanawake wa Kiislamu washiriki maonyesho ya kilimo
Na Habiba Swedi

Wanawake wa Kiislamu washauriwa kupigania haki zao
Na Habiba Swedi, Arusha

Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii
Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Na Mwandishi Wetu

Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga Mungu?
Mahfudhi M. Mahfudhi

MAONI: Porojo za Ngatara -2

Zanzibar na  biashara ya utumwa
Na J. Hussein

Marekani ishitakiwe
Na Abubakar Msham

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3

Mafundisho ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe
 
 
 
 
 
 
 
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita