AN-NUUR
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
KOSOVA: Bosnia nyingine

MIAKA michache iliyopita vyombo vya habari vilitanda habari za kuuliwa, kuteswa na kuvunjwa kwa haki za binadamu, kunyanyaswa Waislamu huko Bosnia ndani ya Ulaya iliyostaarabika.

Wakati machungu, majeraha na makovu ya Waislamu bado hayajakauka; Kosova imegeuzwa kuwa Bosnia nyingine; Waislamu wanachinjwa na makazi yao kuangamizwa kwa kutamka kwao Shahada.

Warsebia wanaopiga miji na vijiji vya Waislamu huko Kosova kwa mabomu wakiua Waislamu wasio na hatia kwa maelfu hawana haki yoyote juu ya eneo hilo kama ambavyo Wacroats na Waserbia kwa pamoja hawakuwa na haki juu ya Waislamu wa Bosnia.

Halikadhalika, kama ambavyo Wayahudi wasivyo na haki juu ya Wapalestina na Wahindu juu ya wananchi wa Kashmir.

Kosova ina watu wapatao milioni 2.2 ambapo asilimia 90 ni wa asili ya Albania Wakatoliki wakiwa asilimia 5 na waliosalia wakiwa Waislamu.

Waserbia wapatao asimilia 10 ya wananchi wa Kosovo wakisaidiwa na Waserbia wa Serbia (Yugoslavia) wanataka kuwadhibiti Waislamu na ikiwezekana kuwasafisha wote.

Mbinu zinazotumika ni kupiga mabomu miji na vijiji ili watu wakimbie. Kuchoma moto nyumba ili waliokimbia baada ya mabomu wasirejee, kuwaua wanaume mbele ya macho ya wanawake na watoto ili watakaposilimua unyama huo, asitamani yeyote kurejea Kosova. Kuwanajisi wanawake mbele ya wanaume na watoto. Ili yote hayo yasijulikane hivyo kutolaaniwa vyombo vya habari na wanadiplomasia wamekuwa kana kwamba wanazuiwa katika kusema ukweli juu ya mauaji hayo ya kuangamiza.

Historia fupi ya Kosova:

1300 BC: Wahenga wa Waalbania wajulikanao kama Illyraina walihamia Balkans.

Karne ya sita AD: Makundi mbalimbali ya Waslav na Wahenga wa Waserbia walihamia Balkans.

1180 AD: Stefan Nemanj aliunda taifa la awali la Muugano la Waserbia.

1389: Waserbia walishindwa na jeshi la Waislamu wa Uturuki (Ottoman). Kuanzia hapo Waseribia wakajenga chuki kali dhidi ya Waturuki na Waislamu.

1459: Kosova ikawa jimbo katika ‘Ottoman Empire’

1912-13: Vita vya Balkan. Waserbia wakashinda katika maeneo mengi ya Serbia.

1939: Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Waalbania wa Kosovo wakaasi dhidi ya utawala wa Serbia.

1946: Muungano wa nguvu za Urusi, Ufaransa na Uingereza iliunganisha kwa nguvu Kosovo na Serbia. Kosovo ikabaki chini ya utawala wa Kikomunisti wa Serbia.

1974: Mamlaka haba yalitolewa kwa Kosovo.

Milosevic akiwa kiongozi wa chama cha Kikomunisti cha Serbia aliingia madarakani kwa kutumia kampeni za chuki dhidi ya Waalbania.

1990: Milosevic alifuta mamlaka ya watu wa Kosovo, na kuwatenza nguvu chini ya utawala wa kijeshi na kuvunja haki zao zote za kiraia.

Juni 25, 1991: Slovenia na Croatia yalikuwa majimbo ya awali kujitangazia uhuru toka Yugoslavia.

Oktoba, 1991: Kosova ilijitangazia uhuru.

1992: Macedonai na Bosnia nazo zikajitangazia uhuru toka Yugoslavia.

1992: Waserbia wakaanza mauaji ya maangamizi dhidi ya Waislamu wa Bosnia.

Agosti, 1992: Yakagunduliwa makambi ya kuwatesea na kuwabaka Waislamu.

Julai, 1995: Majeshi ya Serbia yakakamata mji wa Srebrenica maelfu ya Waislamu wanaume na vijana wakauliwa. Umoja wa Mataifa haukuingilia.

Novemba, 1995: Baada ya Waislamu kuelekea kushinda NATO ikaingilia kati na kulazimisha mkataba wa Dayton (The Dayton Accords).

1995: Dk. Ibrahimu Rugova kwa kutumia demokrasia ya kura alichaguliwa kuwa Rais wa Kosovo. Marekani ikapinga na kutaka asitambuliwe.

1997: Jeshi la ukombozi wa Kosova (Kosova Liberation Army - KLA ) likaanzishwa.

1998: Waserbia wakaanza kuwachinja watoto na wanawake katika kijiji cha Dremica ikifuatiwa na mauaji ya kuangamiza sawa na yale ya Bosnia.
 

Juu

YALIYOMO

TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi

Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Na Mwandishi Wetu

Wanakijiji wawapiga Polisi Olesiva
Na Mwandishi wetu, Arusha

Waislamu washinda kesi Same
Na Mwandishi Wetu, Same

Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah inahujumiwa 
Na Mwandishi Wetu

KOSOVA: Bosnia nyingine

Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin

Historia ya damu za mashujaa Afghanistan

Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata viongozi wapya
Na Suleiman Simba, Kigoma

Muhadhara wanguruma Masjid Hijaz
Na Said Shariff

Waislamu waitumie Misikiti ipasavyo
Na Ashraf Yusuph, Moshi

Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza wengi
Na Mwandishi Wetu

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 3
Na Muhibu Said

Wanawake wa Kiislamu washiriki maonyesho ya kilimo
Na Habiba Swedi

Wanawake wa Kiislamu washauriwa kupigania haki zao
Na Habiba Swedi, Arusha

Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii
Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Na Mwandishi Wetu

Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga Mungu?
Mahfudhi M. Mahfudhi

MAONI: Porojo za Ngatara -2

Zanzibar na  biashara ya utumwa
Na J. Hussein

Marekani ishitakiwe
Na Abubakar Msham

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3

Mafundisho ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe
 
 
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita