|
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998 |
|
Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Kiislamu; Tanzania Islamic Centre (T.I.C) yenye makao makuu Magomeni Mapipa Jijini imewasaidia kwa kuwasafirisha vijana saba waliobahatika kupata nafasi za masomo nchini China. Akiongea kwenye tafrija fupi ya kuwaaga vijana hao iliyofanyika katika ofisi za Tanzania Muslim Hajj Trust mtaa wa Kipata, Katibu Mkuu wa kitengo cha Zakkah Sheikh Jabri alisema kwamba TIC kupitia kitengo chake cha Zakkah kimeamua kuchukua jukumu la kuwapitia Waislamu mbalimbali baada ya serikali kushindwa kuwasafirisha vijana hao. Alisema gharama ya kuwasafirisha vijana hao kwenda masomoni nchini China ni takriban dola za Kimarekani mia nane na sitini na tano (865) kwa kila mmoja. Akitoa shukrani zake kwa niaba ya wazazi wa vijana hao, Mzee Ally Omar Ally alisema ni mara nyingi nafasi kama hizi pengine hutokea lakini kutokana na hali ngumu ya kimaisha nafasi hizo huishia kwa watu ambao sio waliokusudiwa kwa hiyo amewataka Waislamu kuunga mkono kitengo hicho cha Zakkah ili vijana wao wakwamuke na udhalili. Naye Mwenyekiti wa kitengo cha Zakkah, Sheikh Nurudin Hussein akitoa nasaha zake kwa vijana hao aliwaasa wasije wakafanya mambo yaliyo kinyume na maadili ya dini yao wawapo huko ugenini, kwani kufanya hivyo ni sawa na kuudhalilisha Uislamu. Alisema Uislamu ni dini ya heshima na nidhamu na kwamba Waislamu ndio wanaowatuma kwenda huko na matarajio yao kwamba watavuna mavuno mazui kama walivyotarajia. Akipokea nasaha hizo, mmoja wa vijana hao kwa niaba ya wenzake, aliahidi kulinda heshima na maadili ya Uislamu na kwamba wanajua kwamba wao ni tegemeo kubwa kwa Waislamu kutokana na ujuzi watakaoupata huko. Vijana hao ambao wanakwenda kuchukua kozi tatu tofauti katika kiwango cha juu cha Chuo Kikuu ni Mohamed Mwinyimvua, Ligile Mahamoud Vumilia na Shaabani Ally Likonda wanakwenda kuchukua mafunzo ya udaktari kwa kipindi cha miaka sita. Wengine ni Haruna Said Luguluke, Kenguka Mohamed Kenguka pamoja na Omari Ally ambao watachukua sayansi ya kompyuta (computer) kwa kipindi cha miaka mitano. Mwingine ni Mbaraka Mohamed anayekwenda kuchukua sayansi ya mazingira naye pia kwa muda wa miaka mitano. Vijana hao wameondoka kwa ndege ya Gulf Air Agosti 25, 1998 kupitia Muscut hatimaye Shaghai nchini China. Wakati huo huo Mkurugenzi wa Mult Travel Agency, Bw. Rajan ametoa punguzo maalum kwa wasafiri wa kwenda Umra. Akiongea katika hafla hiyo amesema gharama za kwenda na kurudi zitakuwa
dola za Kimarekani 450 pia amesema gharama hizo ni nje ya gharama nyingine
za kawaida.
|
TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Wanakijiji wawapiga Polisi
Olesiva
Waislamu washinda kesi Same
Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah
inahujumiwa
Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin Historia ya damu za mashujaa Afghanistan Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata
viongozi wapya
Muhadhara wanguruma Masjid
Hijaz
Waislamu waitumie Misikiti
ipasavyo
Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza
wengi
Hoja za kutofautisha Yesu na Issa
ni udhaifu, ni uzushi mtupu! - 3
Wanawake wa Kiislamu washiriki
maonyesho ya kilimo
Wanawake wa Kiislamu washauriwa
kupigania haki zao
Africa Muslims Agency: Inavyohudumia
jamii
Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga
Mungu?
Zanzibar na biashara ya utumwa
Marekani ishitakiwe
MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3
|
Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua kwa: webmaster@islamtanzania.org