AN-NUUR
Na.156 Rabi' Awal 1419, Julai 4 - 9, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Wakwama kujenga msikiti kwa miaka 30

WANAFUNZI Waislamu wa Shule ya Sekondari ya Same wamekwama kujengea msikiti wao katika eneo la shule kwa miaka thelathini sasa.

Awali mwaka 1968 wanafunzi Waislamu wa Shule ya Sekondri ya Same waliamua kujijengea msikiti hapo shuleni ili kurahisisha ufanyaji wa ibada. Matarajio na malengo ya awali yalikuwa kwamba wanafunzi wangejitolea kufanya kazi zote za ujenzi kwa mikono yao kama utengenezaji wa matofali.

Katika barua yao Na.9/3/99 ya Septemba 12, 1968, wanafunzi hao Waislamu waliwaomba Waislamu wa mji wa Same kuchanga fedha za kununulia vifaa vya kujengea msikiti huo.

Hata hivyo toka wakati huo mpaka leo msikiti huo haujajengwa.

Wizara ya Elimu kupitia barua yake No. EDS.A1/63/90 ya Mei 14, 1968 na EDS/A1/68/99 ya Septemba 18, 1971 ilitoa ruhusa na kuhimiza ujenzi wa msikti huo. Hata hivyo mpaka leo haijulikani kulitokea nini kwani mpaka leo msikiti huo haujajengwa.

Waislamu wa Same ambao walitarajiwa kutoa msaada mkubwa kwa msikiti huo wa Shule ya Sekondari Same wanyewe wamekwama kujenga msikiti mkuu wa mji huo na mpaka leo wanaswalia gofu la toka wakati wa Mkoloni ambalo laweza kuanguka wakati wowote.

Katika hali hiyo ya kukwama Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Gladness Mziray ameamua kulipa shukrani kwa kura alizopewa kwa kusaidia ujenzi wa Msikiti huo wa Same. Mbunge huyo Mhe.Gladness amekuwa akiwasiliana na wafanya biashara wakubwa jijini Dar es Salaam kuwaomba wachangie ujenzi wa msikiti huo.

Katika barua yake No. NWA/SAME/2/3/98 ya Machi 2, 1998 amemwomba Mkurugenzi wa Kampuni ya Farai Ginnery (DSM) na Marafiki zake watoe mchango kusaidia ujenzi wa msikiti huo.

Mwandishi wa habari hizi hakuweza kujua mara moja iwapo kinachokwamisha ujenzi wa misikiti hiyo ni Waislamu wa Same kukosa fedha au ni ajizi tu na kutokuthamini misikiti huku wakijali zaidi maslahi yao binafsi.

Juu 
 

YALIYOMO
 
TAHARIRI 

Maoni yetu:Tusianze kuulizana tena shida yenu nini 

Agizo la Rais Mkapa lapuuzwa:Wazee wa miaka 80 wateseka Gerezani

Wanawake wasema hawatarudi nyuma mpaka dhulma iondoke

Serikali kuzuia mahubiri ya Waislamu, kuvamia Msikiti, kukamata, kudhalilisha na kuua Wananchi ni kuvunja Katiba na Sheria za Nchi

Kujua lugha ya Kiarabu sio kuujua Mwongozo wa Allah
Na Sadick M. Sadick"

Serikali isidhani kuwa Waislamu wa Tanzania wamelala usingizi

Intifada ndio jibu (2)
Na Sheikh Pandukizi Dilunga

Kusema ukweli ni sehemu ya uadilifu
A.S. Chachika

Mafumbo ya imani yabakie ndani ya Makanisa
Na J. Hussein

Majibu kwa Kamara Kusupa

Tamko la Wanawake wa Kiislamu mkoa wa Morogoro kuhusu kadhia ya Mwembechai

Asiye na elimu kwa mujibu wa Biblia
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

TAMTA yaadhimisha miaka 36
Na Masoud Mohamed Said, Tanga

Muumini aliyeachiwa aeleza jinsi Waislamu wanavyoteswa Segerea
Na Muhibu Said

Wakwama kujenga msikiti kwa miaka 30

Habari za Madrasa

Barua 

Mashairi 

Lishe : Mtoto anyonye maziwa ya mama miaka miwili 
Na Dk. Ali. A. Mzige
  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita