|
|
| Tamko
la Wanawake wa Kiislamu mkoa wa Morogoro kuhusu kadhia ya Mwembechai
Sisi wanawake wa Kiislamu wa Morogoro tunalaani matumizi ya mabavu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na hususan kitendo cha askari polisi kuvamia na kuunajisi msikiti, kuwapiga na kuwatesa Waislamu na raia wengine kinyume na taratibu za kisheria Sisi wanawake wa Kiislamu wa Morogoro tunaunga mkono kwa dhati tamko na maazimio ya mkutano wa Wanawake wa Kiislamu wa tarehe 7/6/98, Masjid Nur-Sinza, Dar es Salaam na tunaitaka serikali iyafanyie kazi kwa kuwa roho za Waislamu na heshima ya wanawake wa Kiislamu si vitu vya kuchezewa. Sisi wanawake wa Kiislamu wa Morogoro tunatamka ya kuwa tunaunga mkono juhudi za Kamati ya Kupigania Haki za Waislamu Tanzania (kamati ya Ponda) katika kusimamia na kufuatilia haki za wote walioathirika kutokana na kadhia hii Sisi wanawake wa Kiislamu wa Morogoro tunatamka ya kuwa tunaungana na akina Wanawake wenzetu wa Kiislamu kote nchini katika juhudi za kufuatilia haki za Waislamu kufuatia kadhia hii na tunatoa ahadi yakuwa hatutarudi nyuma wala hatutohofu mpaka haki ipatikane na wote waliohusika na mauaji ya Waislamu na waliowaadhiri Wanawake wa Kiislamu watakapochukulia hatua za kisheria. Sisi Wanawake wa kiislamu wa mkoa Morogoro tunaunga mkono Kauli na Hoja ya mbunge wa Kigamboni Mh. Kitwana Kondo alizozitoa mbele ya Waandishi wa Habari na kule Bungeni. Na tunaitaka Serikali ifanyie kazi Kauli hizo. Sisi Wanawake wa Kiislamu wa Morogoro tutakuwa nyuma ya Maimamu na Masheikh wetu watakaosimama kueleza dhulma dhidi ya Waislamu na upendeleo kwa Wakristo hasa wa kanisa Katoliki unaofanywa na Serikali ya nchi hii. Na tunamuunga mkono Sheikh mkuu wa Mkoa wa Morogoro Sheikh Omar Bafadhil kwa jitihada anayoifanya hivi sasa ya kutetea Haki za Waislamu. Wanawake wa kiislamu Mkoa Morogoro
|
TAHARIRI Maoni yetu:Tusianze kuulizana tena shida yenu nini Agizo la Rais Mkapa lapuuzwa:Wazee wa miaka 80 wateseka Gerezani Wanawake wasema hawatarudi nyuma mpaka dhulma iondoke Kujua
lugha ya Kiarabu sio kuujua Mwongozo wa Allah
Serikali isidhani kuwa Waislamu wa Tanzania wamelala usingizi Intifada
ndio jibu (2)
Kusema
ukweli ni sehemu ya uadilifu
Mafumbo
ya imani yabakie ndani ya Makanisa
Tamko la Wanawake wa Kiislamu mkoa wa Morogoro kuhusu kadhia ya Mwembechai Asiye
na elimu kwa mujibu wa Biblia
TAMTA
yaadhimisha miaka 36
Muumini
aliyeachiwa aeleza jinsi Waislamu wanavyoteswa Segerea
Wakwama kujenga msikiti kwa miaka 30 Lishe
: Mtoto anyonye maziwa ya mama miaka miwili
|