AN-NUUR
Na.156 Rabi' Awal 1419, Julai 4 - 9, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
TAMTA yaadhimisha miaka 36

Na Masoud Mohamed Said, Tanga

TAASISI ya TAMTA Almadrasat Shamsiyah mwaka huu (1998) imetimiza umri wa miaka 36 tangu kuasisiwa kwake mwaka 1963 na Almarhum Sheikh Muhammad Ayoub.

Maadhimisho ya mwaka huu ambayo yameachana kwa siku chache na siku ya maadhimisho ya Maulid ya Nabii Muhammad (s.a.w) ndiyo ya mwanzo kufanyika bila kuwepo muasisi wake huyo.

Shamrashamra za sherehe hii maarufu kwa jina la "TAMTA Day" zilianza Jumamosi ya Juni 27.

Wananchi waliokuwa bado hawajayasoma matangazo ya sherehe hizi, walielewa wakati vijana na wazee walipokuwa wakirejea kutoka Manyanjani kwa maandamano ya baiskeli na pikipiki huku wakiwa wameshika na kuchomeka kwenye vilemba matawi ya miti ya Pwani ambayo pia iliyoenea katika mitaa yote, kuanzia barabara ya 14 mpaka Msambweni yaliko Makao Makuu ya TAMTA. Wengi walidhani ni askari wakiwa kwenye operesheni fulani za kijeshi.

Siku mbili zilizofuata zilikuwa ni za maonyesho ya kielimu ya wanafunzi wa zamani wa kike na kiume.

Mnamo siku ya kilele Juni 30, ilikuwa ni zamu ya maandamano ya magari. Yakipishana kwa vitambo vifupi na yalionekana yakiingia mjini kutoka kila pembe ya mji, tangu mapema asubuhi.

Wakati wa usiku, wawakilishi wa baadhi ya matawi 80 ya TAMTA walionyesha taaluma zao na kufuatiwa na Samai.

Mudiir mpya Sheikh Muhammad Bakar baadaye alisimama kusoma historia ya marehemu Sheikh Muhammad Ayoub kwa njia ya mashairi ya Kiarabu ambayo yalitafsiriwa pia kwa Kiswahili.

Akifunga sherehe saa 5.30 usiku, mlezi wa TAMTA, Sheikh Abdallah bin Ayoub alitoa shukrani nyingi kwa ushirikiano mkubwa uliopatikana kwa jina la Uislamu. Alisifu ushujaa na ukakamavu wa Mudiir mpya Sheikh Muhammad Bakar ambaye pamoja na mambo mengine imeelezwa kuwa alifanikisha sherehe za mwaka huu.

Mwisho, alitoa wito kwa Waislamu popote walipo wasitoe njia kwa Shetani kukaribia ibada na mambo yao.
 

Juu 
 

YALIYOMO
 
TAHARIRI 

Maoni yetu:Tusianze kuulizana tena shida yenu nini 

Agizo la Rais Mkapa lapuuzwa:Wazee wa miaka 80 wateseka Gerezani

Wanawake wasema hawatarudi nyuma mpaka dhulma iondoke

Serikali kuzuia mahubiri ya Waislamu, kuvamia Msikiti, kukamata, kudhalilisha na kuua Wananchi ni kuvunja Katiba na Sheria za Nchi

Kujua lugha ya Kiarabu sio kuujua Mwongozo wa Allah
Na Sadick M. Sadick"

Serikali isidhani kuwa Waislamu wa Tanzania wamelala usingizi

Intifada ndio jibu (2)
Na Sheikh Pandukizi Dilunga

Kusema ukweli ni sehemu ya uadilifu
A.S. Chachika

Mafumbo ya imani yabakie ndani ya Makanisa
Na J. Hussein

Majibu kwa Kamara Kusupa

Tamko la Wanawake wa Kiislamu mkoa wa Morogoro kuhusu kadhia ya Mwembechai

Asiye na elimu kwa mujibu wa Biblia
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

TAMTA yaadhimisha miaka 36
Na Masoud Mohamed Said, Tanga

Muumini aliyeachiwa aeleza jinsi Waislamu wanavyoteswa Segerea
Na Muhibu Said

Wakwama kujenga msikiti kwa miaka 30

Habari za Madrasa

Barua 

Mashairi 

Lishe : Mtoto anyonye maziwa ya mama miaka miwili 
Na Dk. Ali. A. Mzige
  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita