AN-NUUR 
Na.187 Shawwal 1419, Februari 5 - 11 , 1999 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Fatwa Masheikh kususia mazishi 

Ndugu Mhariri 

NAPENDA kuchukua fursa hii katika gazeti lako ili niweze kumsaidia ndugu yangu Muislamu ambaye alitoa maoni yake kuhusu habari iliyoandikwa katika gazeti hili toleo nambari 181 iliyokuwa na kichwa cha habari "Maiti ya Muislamu yasusiwa". 

Ndugu huyu aliomba Masheikh watoe Fatwa kuhusu kususia mazishi. Katika barua yake ambayo imechapishwa katika gazeti hili toleo nambari 183 iliyokuwa na kichwa cha habari "kususia mazishi Masheikh tupeni Fatwa". 

Naomba nimsaidie kwa kurejea aya ifuatayo katika Qur’an (9:84) "Wala usimswalie kamwe mmoja wao yeyote yule akifa wala usisimame kaburini kwake (kumuombea dua). Hakika hao wamemkataa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakafa na hali ni wenye kuvunja amri za (Mwenyezi Mungu)". 

Habari zilizotolewa kwenye gazeti hili ni kwamba maiti ya Muislamu huyo ilisusiwa kwa kuwa alikuwa tarkuswalat. Kwa hiyo moja kwa moja inaonyesha kuwa alikuwa anakwenda kinyume na maamrisho ya Allah (s.w.) na mwenendo (mafundisho) ya Mtume (s.a.w.). Maana yake ni kwamba hakuwa anatekeleza lengo la kuumbwa kwake ambalo ni kumuabudu Allah (s.w.). 

Kutokana na aya hiyo hapo juu namuomba ndugu yangu atoe shaka na hofu kwa kitendo cha Masheikh kususia mazishi ya Waislamu ambao wanakwenda kinyume na maamrisho ya Allah (s.w.) na mwenendo wa Mtume (s.a.w.). Insha-Allah. 

Sharifa Yusuf, 
Mudio Islamic Seminary, 
P.O. Box 8387, 
Moshi. 


Nampongeza Sheikh Yahya Mohammed

Ndugu Mhariri 

KWA mara yangu ya kwanza napenda kuwapongeza Waislamu wa Makole kata ya kwa Fungo tarafa ya Mbwembwera wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga wakiongozwa na Sheikh Yahya Mohammed Kiduo. 

Kwa kuwa na msimamo wa kweli mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.) na hivyo ndivyo Waislamu wa ulimwengu tunatakiwa tufuate. Hiyo ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w.) pia ni kauli ya Mtume Muhammad (s.a.w.). 

Nawaoma Masheikh wote na Waislamu tufuate amri zote za Mwenyezi Mungu (s.w.) na Mtume wake. Cha kushangaza amri hii inafumbiwa macho nawaomba Masheikh watukumbushe Waislamu wote kupitia ANNUUR pia kupitia katika radio kuhusu msimamo huu wa kutozika wala kuswalia maiti ya namna hiyo kwa kufuata amri ya Mwenyezi Mungu na Sunnah za Mtume (s.a.w.). Tunawaomba waweke wazi jambo hilo ili lifuatwe na wacha Mungu wote Insha-Allah. 

Pia namuomba Sheikh ambaye alikuwa akitufunza Dawa za miti ajitahidi kutoa mafunzo kila makala ili tupate faida. Ninamuomba arudie somo la dawa ya Mkomamanga na aendelee na miti mingine pamoja na dawa zote. Mfano Zamda n.k. naomba anuani yake ili tuweze kumtumia barua. Mola wetu twakuomba tuzidishie elimu na utuzidishie ufahamu. 

Awadh Salim, 
Box Arusha. 


Waislamu tujikomboe
 

Ndugu Mhariri 

ALHAMDULILLAH tumemaliza Ramadhani yetu katika kuisherehekea hatuna budi kupongeza wale wote waliofanya maandalizi ya Baraza la Idd ambayo imetufanya kusisimkwa na kujengwa hisia mpya za kuingia mwaka mpya wa Kiislamu. 

Hivyo basi, Waislamu popote tulipo tafadhali tuingie katika harakati za kudai ukombozi. Tudai mashule ya msingi yote yaliyotaifishwa ili tuweze kuendeleza kizazi kipya kwa misingi ya dini kuanzia chekechea hadi Chuo Kikuu. 

Kama Wakristo wameweza kurudishiwa shule zao za misheni kwa nini sisi kuwepo kigugumizi cha kurudishiwa? 

Tunatoa pongezi kwa IPC kutuandalia muhtasari wa kufundishia na hivyo kutuwezesha kuujua Uislamu wetu vilivyo dhidi ya makafiri. 

Wakati huo tuwe katika maandalizi ya kufanya kumbukumbu za mashujaa wetu waliokufa shahidi Mwembechai. 

Mswadiku, 
Singida. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Mauaji ya Mwembechai; Mh. Rais apewe kanda

Matokeo ya mitihani darasa la saba serikali ieleze: Je, Waislamu ni taahira au kuna agenda ya siri

Hijab ivaliwe shuleni

Wenye siasa za kikaburu wasimyumbishe Rais

Hatuko tayari kuruhusu viwanja viporwe  -   Manyema

Maoni yetu
Kauli ya Waziri Mkuu Bungeni: Tumsikilize nani?

DONDOO ZA KISAIKOLOJIA: PEDOPHILIA

Mjue Usama bin Ladin -3

Uislamu na Mazingira katika Umoja wa Mataifa
Na Dk.  Wahid

Barua ya wazi kwa Rais Mkapa

Barua za Mtume (s.a.w.) za Jihad katika Internet
Na. Zituzzaman Hoque

Kutoka magazeti ya zamzni

Rais Mkapa atekeleze hadi yake kwa hadhari
J.R. Msuya, Moshi

Mashirika ya Dini yaelekeze misaada vijijini
Na KAWELE  SAIDI 

Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma

Ni serikali ipi anayoiwakilisha Sumaye
Na Abu Salim

Sehemu ya maelezo ya Waziri Mkuu bw. Frederick Sumaye bungeni

Zanzibar ni nchi au mkoa?.
Na SALUM ALI 

Sheikh Bafadhil aamuru kusimamishwa shughuli za African Muslim Agency Moro

Vijana Arusha njooni mnione - Alhaj Mollel

Waislamu Korelo wazama kwenye ushirikina

Waislamu Hanang’ wajenga Msikiti

Sayansi na Teknolojia 
[Jifunze ‘Kubana’ Majalada] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Chakula na Lishe 
[Ni hatari kuwaambia wananchi wasichague chakula] 

Kumbukumbu ya mauaji Mwembechai
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita