AN-NUUR 
Na.187 Shawwal 1419, Februari 5 - 11 , 1999 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Matokeo ya mitihani darasa la saba serikali ieleze:
 
Je, Waislamu ni taahira au kuna agenda ya siri
 
  • Waliotahiniwa Waislamu 71% Wakristo 29%
  • Waliochaguliwa Waislamu 21% Wakristo 79%
SERIKALI imetakiwa ieleze ni sababu zipi zinazopelekea watoto wa Kiislamu wanaochaguliwa kwenda kidato cha kwanza wawe wachache sana ikilinganishwa na idadi ya watahiniwa. 

Akizungumza Bungeni Februari 2, 1999 Mbunge wa Kigamboni Mh. Kitwana Kondo alisema kwamba kwa mwaka 1998 watoto Waislamu waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mkoa wa Dar es Salaam walikuwa asilimia sabini na moja (71%) wakati Wakristo walikuwa 29% ya watahiniwa wote. 

Hata hivyo, akasema kwamba waliokuja kuchaguliwa kwenda 

sekondari Waislamu walikuwa asilimia ishirini na moja (21%) wakati Wakristo waliochaguliwa walikuwa asilimia sabini na tisa (79%). 

Kutokana na kielelezo hicho, Mh. Kitwana Kondo alihoji: "ama Waislamu ni wajinga, ama akili zao hazifanyi kazi " ama mtu akiwa Muislamu basi wewe huna kitu au kuna kitu". Kwa hiyo, akaitaka serikali itoe maelezo. 

Katika utangulizi wake, akiielezea nukta hii Mh. Kitwana Kondo alikariri ahadi ya Mh. Rais ya kuyashughulikia matatizo ya kielimu ya Waislamu ambapo pia alishauri wafadhili wajenge shule zaidi badala ya Misikiti, lakini akamtaka Waziri wa Elimu atoe ufafanuzi juu ya jambo hili. 

Kwamba je, watoto wa Kiislamu kutochaguliwa kwenda kidato cha kwanza ni kwamba Waislamu kwa asili yao wanazaliwa wajinga au zipo juhudi za kuwakandamiza. 

Wakati huo huo, Mh. Kitwana Kondo ameliambia Bunge kwamba yapo mambo ambayo yanapangwa na serikali ambayo yanaweza kuleta mfarakano katika jamii yetu, jambo ambalo Mh. Rais amelikemea. 

Akitoa vielelezo alitaja suala la siku ya Ijumaa ambapo katika baadhi ya maofisi na mashule ratiba za kazi hazizingatii haki ya Waislamu kwenda kuswali. 

Ameiomba serikali itoe agizo kwamba shughuli zote za kazi na masomo zisimame saa sita na kama ni kuendelea ziendelee baada ya saa nane. 

Mfano mwingine aliotoa Mh. Kondo ni tabia ya serikali kuchelewesha usajili wa taasisi za Kiislamu bila sababu zozote za msingi. Alieleza kwamba taasisi moja ya Kiislamu ijulikanayo kama Baraza la Maimamu toka iombe kusajiliwa ni miaka mitatu bado haijasajiliwa. 

Aidha, alisema kwamba wakati mwingine Waislamu hudaiwa walete kibali cha Bakwata wanapoomba kusajiliwa, akahoji je, hiyo ni sheria ya serikali au matakwa tu ya wakubwa. 

Suala lingine aliloligusia kama kielelezo cha Waislamu kutokutendewa haki na hivyo kuhatarisha amani ya nchi, ni tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali na hasa katika taasisi za elimu kuwazuia mabinti Waislamu kuvaa hijab. Amesema hiyo ni amri ya Qur’an (33:30-31)na ni lazima iheshimiwe. 

Akizungumzia suala la mitihani ya kidato cha nne kufanyika mwezi wa Ramadhani, Mh. Kitwana Kondo alisema kwamba hiyo ni moja ya chehe za kuleta mfarakano. Hata hivyo akasema kwamba baada ya manung’uniko Waziri wa Elimu alitoa maelezo ambayo yaliwaridhisha Waislamu. 

Hata hivyo, akashangazwa na kuhoji dhamira ya wale wakubwa waliosema kwa jeuri na takabari kwamba watoto wa Kiislamu wakitaka kufanya mtihani wafanye na wasipotaka basi. Hakufafanua ni mkubwa gani huyo. 

Mh. Kitwana Kondo alisisitiza kwamba hao wasiojali hisia za Waislamu na wanaotoa kauli hizo za jeuri ndio wasio itakia kheri nchi yetu. 

Ila kwa upande wake na wengine wanaokuja na kusema hadharani ndio waitakiao mema nchi. 

Aliwaomba viongozi wa serikali na hasa Mawaziri kumsaidia Mh. Rais Mkapa kutekeleza dhamira na ahadi yake ya kuyashughulikia malalamiko ya Waislamu. 

Mh. Kitwana Kondo alipata fursa ya kuyasema yote hayo katika kipindi cha kujadili hotuba ya Mh. Rais Mkapa aliyoitoa Bungeni mwaka jana. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Mauaji ya Mwembechai; Mh. Rais apewe kanda

Matokeo ya mitihani darasa la saba serikali ieleze: Je, Waislamu ni taahira au kuna agenda ya siri

Hijab ivaliwe shuleni

Wenye siasa za kikaburu wasimyumbishe Rais

Hatuko tayari kuruhusu viwanja viporwe  -   Manyema

Maoni yetu
Kauli ya Waziri Mkuu Bungeni: Tumsikilize nani?

DONDOO ZA KISAIKOLOJIA: PEDOPHILIA

Mjue Usama bin Ladin -3

Uislamu na Mazingira katika Umoja wa Mataifa
Na Dk.  Wahid

Barua ya wazi kwa Rais Mkapa

Barua za Mtume (s.a.w.) za Jihad katika Internet
Na. Zituzzaman Hoque

Kutoka magazeti ya zamzni

Rais Mkapa atekeleze hadi yake kwa hadhari
J.R. Msuya, Moshi

Mashirika ya Dini yaelekeze misaada vijijini
Na KAWELE  SAIDI 

Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma

Ni serikali ipi anayoiwakilisha Sumaye
Na Abu Salim

Sehemu ya maelezo ya Waziri Mkuu bw. Frederick Sumaye bungeni

Zanzibar ni nchi au mkoa?.
Na SALUM ALI 

Sheikh Bafadhil aamuru kusimamishwa shughuli za African Muslim Agency Moro

Vijana Arusha njooni mnione - Alhaj Mollel

Waislamu Korelo wazama kwenye ushirikina

Waislamu Hanang’ wajenga Msikiti

Sayansi na Teknolojia 
[Jifunze ‘Kubana’ Majalada] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Chakula na Lishe 
[Ni hatari kuwaambia wananchi wasichague chakula] 

Kumbukumbu ya mauaji Mwembechai
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita