|
|
|
Katika sehemu ya pili, wiki iliyopita, tulichapisha mahojiano ya Bw. Usaama bin Ladin yaliyochapishwa katika gazeti la Nida’ul Islam, Toleo la 15, Oktoba - Novemba 1996 (http://www.islam.org.au). Katika mahojiano hayo, Bin Ladin aliishutmu vikali serikali ya Saud Arabia kwa kung’ang’ania madaraka, kuwabana wanazuoni waadilifu na pia wananchi kwa ujumla. Aidha mwanaharakati huyu alizichambua siasa za Saudia kuhusiana na ulimwengu wa Kiislamu. Leo, alhamdulillah, tunaendelea na sehemu ya tatu ya mahojiano hayo ambapo Bw. Usama anaubainisha ubabe wa Marekani dhidi ya Waislamu na, kisha, anatoa wito kwa Waislamu ulimwenguni kote kuukumbuka wajibu wao wa kidini unaowataka kuunganisha nguvu zao kumkabili dhalimu huyu, Marekani. Mwisho wa mahojiano tumetoa mambo matano ambayo tumeyapata (yatokanayo) katika mahojiano haya na tunadhani ni vizuri Waislamu tukayatia katika nyoyo zetu. Sasa endelea ... [Unafikiri] ni nini wajibu wa Waislamu ulimwenguni kote kuhusiana na hizi kampeni za kimataifa kuupiga vita Uislamu? Jambo ambalo halina shaka katika hizi kampeni za pamoja kati ya Wayahudi na Wakristo dhidi ya Waislamu ulimengini kote, kampeni ambazo mfano wake haujawahi kupatikana, ni kwamba lazima Waislamu kukusanya nguvu zote ili kumshinda adui kijeshi, kiuchumi, kiitikadi na pia katika nyanja zingine zote. Ni muhimu kwa [Waislamu ulimwenguni kote] kuwa ni wenye subira na kushirikaina katika mambo mema na ucha-Mungu na [pia] kuongeza kuujua zaidi ukweli kuwa kilicho muhimu zaidi baada ya sisi kuamini ni kumg’oa adui ambaye anaivuruga dini na ulimwengu kwa ujumla. Ni muhimu kuepuka kugombana wenyewe kwa wenyewe katika mambo yasiyo ya msingi ili tuunganishe juhudi zetu tupate kuung’oa ukafiri uliokithiri. Ni lazima wayaweke maneno haya ya Allah, Aliye Mtukufu, katika vitendo: "hakika huu umma wako ni umma mmoja, na Mimi ni Mola wako, hivyo niabudu Mimi", na wala wasiwe kama wale ambao Allah amewelezea kwa maneno Yake haya: "hakika wale walioigawanya dini yao na kuwa vikundi vikundi, wewe si katika wao". Ipo haja ya kujitolea na wala sio kuzozana katika mambo madogo madogo, na [wala] Muislamu asiyabeze matendo mema [ ya mwenzie] kwa namna yoyote ile. Mtume (s.a.w.) alisema: "Yeyote anayemwamini Allah na Siku ya Mwisho basi aseme maneno mazuri au akae kimya". Pia wazingatie maneno ya Mtume (s.a.w.), "wafahamisheni [wenzenu] wala msiyaharibu [mema waliyoyafanya] wafanyieni wepesi wala msiwafanyie ugumu". Tunamuomba Allah kuujalia umma huu uongofu, kuwainua daraja watu wenye kumtii Yeye[s.w.t.] na kuwadhalilisha wale wote wenye kumuasi, na atupe utawala ambamo wema unaarishwa na uovu unazuiliwa. Ee Mola mpe Rehma Zako Muhammad, [ambaye ni] mja Wako na Mjumbe Wako, na familia yake, na masahaba zake na uwape amani .... Shukurani zote zinamstahiki Allah, Mola wa ulimwengu. Yatokanayo 1. Tawala nyingi zipo madarakani si kwa maslahi ya wananchi, bali kwa maslahi ya watawala. 2. Utakapokuta katika nchi fulani ambapo utawala wake si kwa mujibu wa sheria za Allah lakini utawala huo ukawa na mahusiano mazuri na viongozi wa kidini, basi uwezekano ni kuwa viongozi hao wa kidini hawatendi kama alivyoamrisha Mwenyezi Mungu. 3. Katika jamii ni muhmu liwepo kundi, hususani la wanazuoni, japo wachache,ambalo litakuwa likifanya tathmini ya mwenendo wa serikali na mamlaka za kidini zilizoidhinishwa na serikali. Kundi hili litazikosoa mamlaka hizo mbili na kisha kuonesha Njia Sahihi ingawa litapata misukosuko ndani na nje ya nchi hiyo. 4. Adui anayetukabili Waislamu amepania kwelikweli. Kumshinda adui huyu tunahitaji juhudi za pamoja na kufuata Qur’an na Sunnah. Leo hii hapa Tanzania Waislamu tumegawanyika makundi makundi; mbaya zaidi ni kuwa Waislamu wa kundi moja wanakuwa ni vipenzi zaidi wa makafiri kundi la Waislamu wenzi wao! 5. Mwenyezi Mungu aliyetuamrisha kufunga saumu ya Ramadhani ndiye huyo huyo ametuarisha kupigana kwa ajili Yake kuondoa dhuluma na pia kulipiza kisasi. Yote haya yamo ndani ya Qur’an na hatuna budi kutii ikiwa sisi ni wenye kuamini. Allah ndiye Mjuzi zaidi |
YALIYOMO
Tahari
Matokeo ya mitihani darasa la saba serikali ieleze: Je, Waislamu ni taahira au kuna agenda ya siri Wenye siasa za kikaburu wasimyumbishe Rais Hatuko tayari kuruhusu viwanja viporwe - Manyema Maoni yetu
DONDOO ZA KISAIKOLOJIA: PEDOPHILIA Uislamu na Mazingira katika
Umoja wa Mataifa
Barua za Mtume (s.a.w.) za Jihad katika
Internet
Rais Mkapa atekeleze hadi yake
kwa hadhari
Mashirika ya Dini yaelekeze
misaada vijijini
Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma Ni serikali ipi anayoiwakilisha
Sumaye
Sehemu ya maelezo ya Waziri Mkuu bw. Frederick Sumaye bungeni Zanzibar ni nchi au mkoa?.
Sheikh Bafadhil aamuru kusimamishwa shughuli za African Muslim Agency Moro Vijana Arusha njooni mnione - Alhaj Mollel Waislamu Korelo wazama kwenye ushirikina Waislamu Hanang’ wajenga Msikiti Sayansi na Teknolojia
Chakula na Lishe
|