|
|
|
ZANZIBAR imeundwa kwa visiwa viwili ambavyo ni Unguja na Pemba. Nchi ya Tanzania ni muunganiko wa nchi mbili tofauti ambazo ni Tanganyika na Zanzibar, ambapo Zanzi bar ina mikoa mitano na Tanganyika ina mikoa ishirini, kwa pamoja inafanya Tanzania kuwa na jumla ya mikoa ishirini na tano. Salum Ali wa Zanzibar anaelezea zaidi. Dhana ya kujiuliza endapo Zanzibar ni nchi au mkoa ndani ya Tanganyika inakuja baada ya kufuatilia mambo kadhaa ya msingi ya kiutendaji katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uwezo wa Zanzibar kama nchi unaelekea kuondoka kabisa baada ya kubanwa kiuchumi na serikali ya Muungano. Sisi kama Wazanzibari tunapaswa kujiuliza huu Muungano wetu ni muungano gani wa kiuchumi kati ya "The Free Trade Area" au "The Customs Union" au "The Common Market" au "The Economic Union? Mifano hii ya miungano ya kiuchumi haina ubaguzi wakati baina ya nchi husika na "terms" zake za mikataba zipo wazi kwa pande zote mbili na inafaidisha pande zote husika bila pande moja kuona na kuhisi inabaguliwa. Inawezekana kabisa Muungano wa Zanzibar na Tanganyika ni muungano wa pumbazo la kisiasa la kuharibu na kunyonya upande mmoja ambao ni Zanzibar. Maana Zanzibar haina tofauti sana na mikao ya Pwani, Tabora, Mtwara, Lindi, Kigoma na Tanga n.k. Kwa sababu mikoa hii huishi Waislamu wengi angalau kama Zanzibar. Wazanzibari hatuna budi kuhisi hivyo kwa jinsi tunavyotendewa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zanzibar ni nchi yenye asilimia 99% ya Waislamu kati ya wananchi wote wa Zanzibar. Cha kushangaza serikali ya Jamhuri ya Muungano imeizuia Zanzibar kujiunga na umoja wa nchi za Kiislamu (OIC) kwa sababu zisizoeleweka. Kinyume chake Wakristo wa Tanzania hupata misaada mbalimbali kutoka kwenye nchi za Kikristo kwa manufaa ya Wakristo. Kwa mfano sasa hivi vyuo vikuu vingi vimejengwa vya Kikristo kwa misaada kutoka nje, Je, Waislamu sisi hatma yetu nini baadaye? Hali hii inaonyesha upendeleo wa kidini ndio ulio tawala katika serikali ya Jamhuri ya Muungano. Zanzibar inashindwa kutetea nguvu za umeme wa kutumia taka kutoka Malaysia ambao ilitarajiwa kuwekeza hapa Zanzibar. Hii ni kutokana na serikali ya Jamhuri ya Muungano kutounga mkono na shinikizo toka nje. Zanzibar tunategemea umeme kutoka bara, hii ni kutufanya tuwe tegemezi katika nyanja muhimu ili tutawaliwe kisiasa na kiuchumi na ndivyo ilivyo. Sababu mojawapo ya kuzuia uwekezaji ule wa umeme wa taka ni kwmba eti TANESCO itakosa mapato kutoka Zanzibar. Hii ni sababu dhaifu sana na ni ya kidini kwa sababu zipo Missions za Kikristo kama vile Peramiho - Songea, Nambele - Songea n.k. zina umeme wa kutumia maji kwa ajili ya matumizi yao binafsi na vijiji vya jirani mbona serikali ya Jamhuri ya Muungano haisemi kama TANESCO itakosa mapato kwa Missions hizo kuwa na umeme wao? Huko kukosa mapato kupo Zanzibar tu? Kama siyo udini ni nini? Tuelezwe. Zanzibar tunataka kuanzisha kampuni ya simu (ZANTEL) ambayo itatoa huduma Zanzibar bado nayo tunatiliwa ngumu eti TTCL itakosa mapato. TTCL itakosa mapato kwa Zanzibar tu kuanzisha kampuni yake ya simu? Mbona kuanzishwa kwa TRITEL na MOBITEL haiwi kukosesha mapato TTCL ila Zantel itakosesha mapato. Hii inaonyesha jinsi gani Zanzibar inavyokabwa katika kujiendeleza. Suala lolote linaloonekana ni mali na manufaa kwa Zanzibar halikubaliki, kwa nini? Hii ni jitihada ile ile ya kudhoofisha kiuchumi maeneo yenye Waislamu wengi Tanzania kama vile Mtwara, Lindi, Kigoma, Pwani na Tanga n.k. Kama kweli Tanzania ni muungano wa nchi mbili zenye Marais yaani Zanzibar na Tanganyika, mbona mgawanyo wa taasisi na vyuo vya elimu haupo sawa? Tanzania bara kwa mfano kuna vyuo vya biashara kama vile College of Business Education (CBE), DSA, Vyuo vya Ufundi, SIDO n.k. ambavyo vimetapakaa karibu mikoa yote ya bara na hakuna hata kimoja Zanzibar. Sisi kama Watanzania Wazanzibari tuelewe vipi, ikiwa tuna haki ya kupatiwa na sisi ujenzi wa vyuo hivyo Zanzibar? Sasa hivi tuna msuguano mwingine wa Zanzibar kuwa "Free Port" bado tunatiliwa ngumu na serikali ya Jamhuri eti serikali itakosa mapato, mapato gani hayo? Kama kweli Muungano wetu ni wa kheri kwanini tuvutane au tuwekeane ngumu kwa kuona wivu kuwa Zanzibar itanufaika. Mlioliona kwa serikali ya Jamhuri kukosa mapato ni kwa Zanzibar kuwa "Free Port" tu? Vipi ndege za Kikristo zinaingia na kutoka Tanzania kwenye viwanja vyao bila kupekuliwa hamuoni kama serikali inakosa mapato? Mali inayoingizwa au kutolewa kwenye "Air Strips" za Wakristo kusiko na polisi wala Afisa "Custom" kwa ndege za Kikristo mnazijua? Ila Zanzibar tu kuwa "Free Port" huu ni udini ulio dhahiri. Ili kujinasua na hali hii serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Wazanzibari
wote kwa ujumla bila kujali tofauti za kisiasa tushikamane ili tuweze kujitegemea
katika njia zote kuu za uchumi na ulinzi. La sivyo, tukubali Zanzibari
kuwa mkoa na siyo nchi yenye Rais.
|
YALIYOMO
Tahari
Matokeo ya mitihani darasa la saba serikali ieleze: Je, Waislamu ni taahira au kuna agenda ya siri Wenye siasa za kikaburu wasimyumbishe Rais Hatuko tayari kuruhusu viwanja viporwe - Manyema Maoni yetu
DONDOO ZA KISAIKOLOJIA: PEDOPHILIA Uislamu na Mazingira katika
Umoja wa Mataifa
Barua za Mtume (s.a.w.) za Jihad katika
Internet
Rais Mkapa atekeleze hadi yake
kwa hadhari
Mashirika ya Dini yaelekeze
misaada vijijini
Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma Ni serikali ipi anayoiwakilisha
Sumaye
Sehemu ya maelezo ya Waziri Mkuu bw. Frederick Sumaye bungeni Zanzibar ni nchi au mkoa?.
Sheikh Bafadhil aamuru kusimamishwa shughuli za African Muslim Agency Moro Vijana Arusha njooni mnione - Alhaj Mollel Waislamu Korelo wazama kwenye ushirikina Waislamu Hanang’ wajenga Msikiti Sayansi na Teknolojia
Chakula na Lishe
|