|
|
| Barua
za Mtume (s.a.w.) za Jihad katika Internet
Barua adimu zenye chapa (seal) ya Mtume Muhammad (s.a.w.) hivi karibuni zitaanza kuonekana, Insha’Allah, katika mtandao wa kompyuta ulimwenguni, Internet, gazeti la serikali nchini Misri, Al-Akhbar, lilitangaza. Barua hizo ambazo zilipatikana kutoka katika jumba la makumbusho la Topkapi huko Instanbul [Uturuki] zilikuwa zimetumwa kwa watawala wa Uhabeshi (Ethiopia), Persia (Iraq) na Misri. Mtume (s.a.w.) alipeleka barua nyingi kwa wafalme walioishi katika ukanda unaozunguka Peninsula ya Uarabuni akiwataka watawala hao kusilimu, alisema Mkurugenzi wa mradi huo, Hamed Abdur-Rahim. Mradi huo uliotayarishwa na Kituo cha Urithi wa Kisayansi cha Chuo Kikuu cha Cairo, umekusudiwa kuthibitisha kuwa Uislamu ulianza ukiwa ni dini imara na utaendelea kuwa imara. Barua hizi si tu kwamba ni vitu vya kihistoria. [bali] zilikuwa ni sehemu muhimu katika mpango wa Mtume (s.a.w) kuieneza dini. Allah (s.w.t.) alisema: Na tumekupeleka wewe kama mletaji wa biashara njema na muonyaji kwa watu wote. (Qur’an 34:28) Hii ilimaanisha kuwa Uislamu (kama mfumo wa maisha ya jamii) ndio unaostahiki kuwa kigezo kwa wanaadamu wote. Hivyo sera (siasa) za Dola ya Kiislamu kuhusiana na masuala ya nchi za nje ni kuyafanya mataifa yote yafuate amri za Allah (s.w.t.). Na kwa sababu hiyo, Mtume (s.a.w.) aliwatuma mabalozi wakiwa na barua hizi, kwenda kwa watawala wa mataifa makubwa wakati huo. Mataifa hayo ni pamoja na taifa lililokuwa kubwa katika kanda ya Uarabuni mfano Yemen, na pia mataifa makubwa ulimwenguni kwa wakati ule, Warumi na Wapersia (Wairaq). Kwa kweli Uislamu ulianza ukiwa imara. Sera hii ya masuala ya nchi za nje ilileta mafaniko makubwa muda wote ambao ilitekelezwa na viongozi wa Dola ya Kiislamu walioshika madaraka baada ya Mtume (s.a.w.). Watu waliingia Uislamu makundi kwa makundi. Wengi walislimu na walikubali kuishi chini ya utawala wa dola ya Kiislamu. Wengine hawakusilimu lakini waliishi katika Dola hiyo na walilindwa (ahl udh-dhimmah). Wale walioyakanusha wazi wazi maamrisho ya Allah (s.w.t.) walijikuta wakipigana vita na Waislamu, vita ambayo hatimaye iliwaacha [makafiri hao] chini ya utawala wa Dola ya Kiislamu. Kwa njia hii Uhabeshi, Persia na Misri zikawa sehemu ya dola ya Kiislamu. Mataifa hayo yaliunganishwa katika Dola ya Kiislamu mpaka ikawa hakuna dalili kuwa mataifa hayo yalikuwa tofauti. Hakika, Uislamu ulianza ukiwa imara na ulindelea kuwa imara. Leo hii kilichobaki kama ushahidi wa sera hiyo ya dola ya Kiislamu juu ya masuala ya nchi za nje ni hizi barua na umma huu wa Waislamu. Hakuna utawala wa Kiislamu. Nafasi yake imechukuliwa na serikali za ki-secular (zisizofuata maamrisho ya Allah bali matashi ya mwanadamu) kama zilivyo serikali za Misri na Iran. Matokeo yake ni kuwa hivi sasa hakuna kabisa sera hiyo ambayo Mtume wa Allah (s.a.w.) aliileta. Badala yake kumekuwepo na sera ambazo zinaufanya u-secular kuwa ndio kigezo kikuu cha mfumo wa maisha ya mwanadamu. Nchi zote leo hii ni wanachama wa Umoja wa Mataifa na kwa maana hiyo zimeitelekeza Jihad zikichelea kuwa kupanuka kwa tawala za Kiislamu kutaonekana kuwa ni kukiuka sheria za kimataifa. Badala ya [mataifa ya kiislamu] kutuma mabalozi [katika nchi zisizo za Kiislamu] ili kuwafikishia neno la Allah (s.w.t.) [wapate kusilimu] zinabaki kuwanyenyekea Clinton na wenzake na kuyafuata kwa unyenyekevu yale Clinton anayowaeleza. Hakika Uislamu ulianza imara na utaendelea kuwa imara. [Lakini] Ili hili liwezekane inahitajika kuwepo tena kwa utawala wa Kiislamu ili Uislamu upate kuenezwa ulimwenguini kote. Muhammad (s.a.w.) alisema, "Jihad ni jambo lenye kuendelea tangu kuteuliwa kwangu (kuwa Mtume) mpaka [mtu] wa mwisho katika umma wangu atakapombana na Dajjal". Khilafah Magazine
|
YALIYOMO
Tahari
Matokeo ya mitihani darasa la saba serikali ieleze: Je, Waislamu ni taahira au kuna agenda ya siri Wenye siasa za kikaburu wasimyumbishe Rais Hatuko tayari kuruhusu viwanja viporwe - Manyema Maoni yetu
DONDOO ZA KISAIKOLOJIA: PEDOPHILIA Uislamu na Mazingira katika
Umoja wa Mataifa
Barua za Mtume (s.a.w.) za Jihad katika
Internet
Rais Mkapa atekeleze hadi yake
kwa hadhari
Mashirika ya Dini yaelekeze
misaada vijijini
Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma Ni serikali ipi anayoiwakilisha
Sumaye
Sehemu ya maelezo ya Waziri Mkuu bw. Frederick Sumaye bungeni Zanzibar ni nchi au mkoa?.
Sheikh Bafadhil aamuru kusimamishwa shughuli za African Muslim Agency Moro Vijana Arusha njooni mnione - Alhaj Mollel Waislamu Korelo wazama kwenye ushirikina Waislamu Hanang’ wajenga Msikiti Sayansi na Teknolojia
Chakula na Lishe
|