|
Na. 042 Jumatano Aprili 5 - 11, 2000 |
|
|
|
|
|
Wasomi mnatakiwa kukomesha dhuluma Na Mwandishi Wetu VIJANA wasomi wa Kiislamu nchini wametakiwa kujitokeza na kusimama imara kukomesha dhuluma iliyoelezwa imeshamiri katika jamii na hivyo kuhatarisha mustakabali wa taifa hili. Wito huo umetolewa na Amir wa Shura ya Maimamu nchini Sheikh Juma Mbukuzi , alipozungumza na wanafunzi wa Kiislamu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumapili iliyopita. "Nyie vijana wa chuo kikuu lazima muwe wacha-Mungu ili (muweze) kuupiga kumbo udhalimu katika dunia ..." alisema Sheikh Mbukuzi alipoongea na wanafunzi hao katika msikiti wa Chuo Kikuu hicho. Aliwambia wasomi hao kuwa dhuluma katika jamii ni lazima iondolewe kwa gharama yoyote na kwamba "wanaodhulumu wasiungwe mkono". Amir huyo wa Shura ya Maimamu aliwaambia wanafunzi hao kwamba kwa mujibu wa dini yao ya Kiislamu kuubadilisha utawala usio na uadilifu ni suala la wajibu. "Kuubadilisha utawala ulio dhalimu ni wajibu katika dini yetu ya Kiislamu ... Hadith nyingi za Mtume (s.a.w.) zinafundisha kuondoa dhuluma kwa gharama yoyote" alisema Sheikh Mbukuzi. Akionesha haja ya kuleta mabadiliko nchini, Amir Mbukuzi alisema jamii ya Watanzania imegubikwa na madhila mengi ikiwemo hali mbaya ya uchumi na ukiukwaji wa haki za raia. "... na anayechafua mazangira tunamjua, hivyo Oktoba dhalimu aondolewe ..." alisema Amir huyo na kisha akaonya kwamba iwapo mabadiliko hayataletwa basi hali hiyo mbaya itazidi. Hata hivyo Amir huyo wa Shura ya maimamu alilitia moyo kundi hilo la wasomi kuwa dhuluma huwa haidumu. "Hakuna dhuluma inayodumu", alisema Amir Mbukuzi Mwezi Oktoba mwaka huu Tanzania itafanya uchaguzi mkuu wa madiwani, Rais na wabunge ambao ni wa pili katika mfumo wa vyama vingi vya siasa. Uchaguzi wa kwanza wa aina hiyo ulifanyika mwaka 1995 ambapo mgombea wa CCM, Bw. Benjamin William Mkapa, alishinda kiti cha urais. |
YALIYOMO
Tahariri
Mbukuzi
anguruma Chuo Kikuu:
Kuelekea
uchaguzi mkuu 2000:
Maalim Seif afunguliwa mashitaka ‘Tume ya Keenja’ haikufanya ilichoagizwa - Wananchi MPASHO NASAHA
Ushauri Nasaha
MAKALA
WAZO LA WIKI
MAKALA
Kalamu ya Mwandishi
Makala
MAKALA
Riwaya
Lishe
Madadi azionya timu za Ligi Kuu |
|
|
|
|