NASAHA
Na. 036 Jumatano Februari 23 - 29, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Habari za ndani
 
 

NCCR-Mageuzi wamkataa Msimamizi wa Uchaguzi

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha upinzani cha NCCR-Mageuzi Wilaya ya Nzega mkoani Tabora kimewakataa wasimamizi wa uchaguzi mkuu ujao katika wilaya hiyo kutokana na madai kadhaa, likiwemo la kushindwa kusimamia uchaguzi wa serikali za vijiji na hivyo kufanya uchaguzi kutokuwa wa haki na huru.

Katika barua ya Februari 8, yenye kumbukumbu nambari NCCR/NCG/Vol. I/975 ambayo chama hicho kimemwandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kusainiwa na Katibu wa Wilaya ya Nzega, Bw. Katoro Ramadhani, ambayo NASAHA ina nakala yake, chama hicho kimetaja majina ya wasimamizi hao kuwa ni Ndugu Jamari Gazembe ambye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega na Ndugu Masili ambaye ni Katibu Tawala katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Nzega. 

"Mkurugenzi Mtendaji wilaya ameshindwa kabisa kusimamia uchaguzi wa serikali za vijiji, hivyo kufanya uchaguzi kuwa na migogoro mingi na kufanya kuwa sio HURU NA HAKI. Hii inatokana na kwa yeye kutoa maamuzi kwa shinikizo la chama tawala... Mfano hai ni kitongoji cha Nyasa Mpya kata ya Nzega mjini na katika kijiji cha Ifumba kata ya Lusu ambapo wapinzani tulishinda lakini yeye kwa shinikizo alibatilisha matokeo", kinasomeka kifungu A(1) cha barua hiyo. 

Aidha, kifungu B(1) kinasomeka, "Katibu tawala wilaya ya Nzega yeye kama Mwenyekiti wa Kamati ya rufaa ya wilaya amekuwa akishirikiana na Mkurugenzi kutoa maamuzi yao kwa kuegemea chama tawala". Kifungu B(2) nacho kinasomeka, "Maamuzi mengi aliyokuwa akiyatoa yeye na kamati yake yalikuwa ya jazba, hayakufuata sheria, taratibu na maelekezo. Hii imejionesha katika rufaa nyingi zilizopelekwa mbele yao kam avile rufaa ya Nyasa Mpya na kijiji cha Nzega Mashariki, Ifumba na vingine vingi". 

Pamoja na mambo mengine yaliyoorodheshwa katika barua hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Nzega, pia barua hiyo inamtaka Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua hatua mapema ili kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Oktoba wasihusishwe kama wasimamizi. 

Wakati huo huo ule mkutano Mkuu wa Taifa wa uchaguzi wa Chama cha NCCR-Mageuzi uliokuwa ufanyike siku ya Jumatatu Februari 21, umeahirishwa mpaka Machi 4, kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Vijana wa chama hicho, Bw. Joseph Selasini alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu katika ofisi za chama hicho zilizopo Ilala hapa jijini. 

Sababu zilizotolewa za kuahirishwa kwa mkutano huo ni kutokana na mikoa mitano kati ya ishirini kushindwa kuhudhuria mkutano huo kulikosababishwa na kushindwa kumaliza chaguzi ndani ya mikoa hiyo.

Sababu nyingine ni chama makao makuu kukosa pesa za kuendesha mkutano huo wa uchaguzi, japokuwa haikuelezwa wazi kwanini wajumbe waliitwa huku ikiwa inajulikana wazi kuwa fedha hakuna. 

Baadhi ya wajumbe wa mkutano huo walioongea na mwandishi wetu walisema kuwa wameridhishwa na sababu iliyotolewa na uongozi wa juu ya kuahirishwa kwa mkutano. 

"Sababu ni za msingi, kumbuka kuwa kuna watu ambao kwa nafasi ya ushiriki ni wagombea nafasi za ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ambao wako kwenye mikoa hiyo, hivyo kuwanyima nafasi ni kuvuruga demokrasia", alisema Bwana Ahmed Khalid ambaye ni mjumbe kutoka mkoa wa Tabora. 

Juu

YALIYOMO
 

Tahariri:
Katiba ya Zanzibar ni ya Wazanzibari

‘CUF tumejiandaa kuchukua serikali'

Suala la Mwembechai lazua mtafaruku

Mabadiliko ya katiba ya Zanzibar: CCM Z'bar ina nafasi ya ushindi

MPASHO NASAHA
Ulimbukeni wa siku ya Valentino

Habari za ndani
NCCR-Mageuzi wamkataa Msimamizi wa Uchaguzi

Ushauri Nasaha
Nafasi ya familia katika makuzi ya mtoto

MAKALA
CCM imepindua nini?

WAZO  LA  WIKI
Vitisho vya kikachero visihamishiwe mashuleni

Makala ya Kimataifa
Mtazamo wa maadui wa Uislamu juu ya Uislamu

Kalamu ya Mwandishi
Katiba irekebishwe, lakini kwa maslahi ya wananchi

MAKALA
MAREKEBISHO YA 13 YA KATIBA YA  JAMHURI YA MUUNGANO -2
Vita dhidi ya demokra

HABARI ZA KIMATAIFA

  • Clinton kusaidia  amani Burundi
  • Nigeria yaazimia kuwa taifa la Kiislamu
  • n.k

  • Riwaya 
    Ndoto ya mafanikio - 2

    LISHE
    Madhara ya mafuta mwilini

    Barua/Maoni

    MASHAIRI

    MICHEZO

  • Makoye, Mapunda wateta Dar 
  • Tino, Katolila, Omar 'wautwaa' ukocha 
  • Tuna mashaka na Shungu - Yanga

  •  

     

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com


    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita