AN-NUUR 
Na.185 Shawwal 1419, Januari 29 - Februari 4 , 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Kamanda Gewe atakiwa amkamate Daniel

WAISLAMU Jijini Dar es Salaam wamemtaka Kamanda Gewe amkamate Bw. Daniel Zakaria kwa kosa la kughushi hati za nyumba na kutaka kuzipora. 

Wito huo umetolewa kufuatia ushahidi mpya uliopatikana kuelezea jinsi Bw. Daniel alivyokuwa amefanya jaribio la kupora nyumba za Hajat Aziza Bint Omar toka akiwa hai. 

Ushahidi huo unaonyesha kwamba mwaka 1986 Bw. Daniel alighushi hati za nyumba na kuandika jina lake la Daniel Zakaria. Taarifa zilipelekwa kituo cha Polisi Msimbazi ambapo ilitolewa hati ya kusakwa Bw. Daniel. Hata hivyo Bw. Danile hakuonekana hadi alipofariki Hajat Aziza. 

(Marehemu) Hajat Aziza alipewa barua na Polisi akapewa hati mpya na jina la Daniel Zakaria likafutwa kwenye vitabu vya ofisi ya kodi ya mapato. 

Katika hali isiyoeleweka Bw. Daniel kupitia mahakama ya Kisutu alipewa kibali cha usimamizi wa nyumba hizo. 

Kufuatia shauku ya Waislamu kutaka kujua ni kwanini Bw. Daniel hajakamatwa, ANNUUR iliwasiliana na Kamanda wa polisi mkoa wa Dar es Salaam Bw. Alfred Gewe.  

Hata hivyo, Kamanda Gewe alipoombwa aeleze ni kwa nini Bw. Daniel hajakamatwa na hati ya polisi ya kukamatwa mtuhumiwa humaliza uhalali wake baada ya muda gani, hakutaka kusema lolote akidai kwamba suala hilo lishahukumiwa mahakamani. 


Sheikh awasambaratisha walevi Liwale
 

SHEIKH Yasin Mpako wa Liwale amepongezwa na waumini kwa hatua yake ya kuwasambaratisha walevi ambao walikuwa wamevamia eneo karibu na Msikiti. 

Walevi hao walikuwa wakinywa pombe na kucheza ngoma jirani kabisa na Msikiti wa Mtaa wa Soko; hali iliyofanya watu wanaoswali wasisikilizane. 

Wakati mmoja ndani ya mwezi wa Ramadhani walevi hao wlaianza ngoma yao wakati swala ya Dhuhri ikikimiwa. 

Sheikh Mpako alitoa dakika 15 kwa walevi hao kusambaa lakini wakakaidi wakidai kwamba pombe ni yao na wana kibali cha serikali. 

Kufuatia ukaidi huo, Sheikh Yasin Mpako alichukua bendera yake na kuanza kuuzunguka uwanja huo kwa Tahlil na Takbir, waumini walifurika eneo hilo kumhami Sheikh wao jambo lililowafanya walevi watimke. 

Kufuatia hatua hiyo, Waislamu wa Liwale hasa waumini wa Msikiti wa Mtaa wa Sokoni wamekuwa wakimpa pongezi Sheikh Mpako kwa kuwaondolea kero ya walevi hao. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Kama hakuna haki watu watachukua sheria mkononi 

Kupokelewa kwa malalamiko ya Waislamu: Masheikh wasubiri ukweli wa Mkapa 

Afariki baada ya kutokwa damu nyingi: Yadaiwa hakuwa na sh. 4,000 

Nyumba ya Wakfu iliyoporwa yarejeshwa 

Kamanda Gewe atakiwa amkamate Daniel 

Sheikh awasambaratisha walevi Liwale 

Msikiti wavamiwa na kuvunjwa milango, madirisha 

Mjue Usama bin Ladin -2 

Msikiti wa Mwinyimkuu wafanya sensa 

Njaa hakuna, tunategemea kula silaha 

Parole kwa mbinde! 

Mabaraza yawatetee Waislamu - Sheikh Bafadhil 

Hali ya Uislamu Lukulunge, Kongwa inatisha 

Waislamu Kondoa waagizwa kuyatunza magazeti ya ANNUUR 

I.P.C yatakiwa kujitangaza 

Kutoka magazeti ya zamani 

Sabato ni ya Waisraeli, Mungu alikwishaiondoa 
Na Muhibu Said 

Waislamu wachoma moto nguruwe 

Tume ya kubadili Katiba Kenya: Waislamu kuwakilishwa 

Waislamu Msonge waomba wanusuriwe 

Sayansi na Teknolojia 
[PELEKA FAX NCHI ZA NG’AMBO BURE! – (2)] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na Lishe 
[Mwongozo wa mlo wa kila siku] 
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita