AN-NUUR 
Na.185 Shawwal 1419, Januari 29 - Februari 4 , 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Kutoka magazeti ya zamani

Chifu Masanja katoka Tanu kaingia Congress 

Mwafrika No. 828, Jumanne Septemba 25, 1962

CHIFU Francis Masanja wa Bukwimba na pia mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria, nchini Tanganyika alitangaza jana kwamba amejiuzulu katika TANU na kuingia chama cha Congress. 

Chifu Masanja ambae aliingia katika Baraza la Kutunga Sheria kwa tikiti ya TANU, amesema kwamba amechukua hatua hii baada ya kuona kile alichokiita mengine ya TANU sio ya faida kwa watu wa Tanganyika. 

Katika taarifa yake magazetini Masanja anasema: Sasa nimeingia Congress, nami nitatoa siasa yake katika Baraza la Kutunga Sheria kwa sababu nimeshawishiwa kabisa kwamba ndio chama cha pekee ambacho bila woga au upendeleo, kinachunga haki za binadamu na kutoa maoni ya kweli ya watu wa nchi hii. 

Sio Demokrasia 

Alisema pia kwamba mara nyingi alisikia malalamiko kutoka kwa wanachama wa Wilaya yake na nyingine juu ya mambo yasiyo ya kidemokrasia yanayoendeshwa na wakuu wengine wa TANU. 

"Kuna mambo mengine ambayo wakuu wa TANU waliwasumbua baba kabwela, bila ya kujali haki zao", alisema. 

Chifu Masanja pia anasema kwamba TANU, kwa kutaka kura za watu, ilitoa ahadi nyingi kwa watu katika uchaguzi uliopita, lakini imeshndwa kabisa kutimiza ahadi hizo. Akasema wapiga kura hawaridhiki. 

Hakuna Uhuru 

Taarifa hiyo pia imesema kwamba ikiwa hali hii itaendelea nchi itachafuka na hakutakuwa na uhuru, na hasa uhuru wa kusema. 

Alipoulizwa na mwandishi wetu kama amejiuzulu kwa sababu Uchifu umeondolewa, Masanja akajibu kwamba hiyo sivyo, na pia kwamba hana cheo chochote katika Congress bali ni mwanachama wa kawaida tu. 

Msemaji wa TANU alipoulizwa kutoa maoni yoyote alisema kuwa hakuwa na maoni. 


Bendera ya Congress imeangushwa
Mwafrika No. 828, Jumanne Septemba 25, 1962

BAADA ya bendera ya Congress kutundikwa katika ofisi yao mpya huko Tanga, asubuhi mti wa bendera hiyo ukaonekana umekatwa na kuangushwa chini. 

Hivi majuzi mjini Tanga ilifanyika sherehe ndogo ya kufungua ofisi kuu ya Jimbo ya chama cha African National Congress mtaa wa Ngamiani, barabara ya 15. 

Katika sherehe hiyo, bendera nyekundu yenye alama nyeusi ya ‘T’ katikati ilitundikwa kama kawaida nje ya ofisi. 

Baada ya kupepea kwa kutwa moja siku ya pili ikaonekana kwamba mti wa bendera umekatwa na kuangushwa chini. 

Wakuu wa ofisi bado hawajatoa tamshi lolote na wala haijulikani kitendo hicho kimefanywa na nani, lakini polisi imearifiwa nayo inafanya uchunguzi. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Kama hakuna haki watu watachukua sheria mkononi 

Kupokelewa kwa malalamiko ya Waislamu: Masheikh wasubiri ukweli wa Mkapa 

Afariki baada ya kutokwa damu nyingi: Yadaiwa hakuwa na sh. 4,000 

Nyumba ya Wakfu iliyoporwa yarejeshwa 

Kamanda Gewe atakiwa amkamate Daniel 

Sheikh awasambaratisha walevi Liwale 

Msikiti wavamiwa na kuvunjwa milango, madirisha 

Mjue Usama bin Ladin -2 

Msikiti wa Mwinyimkuu wafanya sensa 

Njaa hakuna, tunategemea kula silaha 

Parole kwa mbinde! 

Mabaraza yawatetee Waislamu - Sheikh Bafadhil 

Hali ya Uislamu Lukulunge, Kongwa inatisha 

Waislamu Kondoa waagizwa kuyatunza magazeti ya ANNUUR 

I.P.C yatakiwa kujitangaza 

Kutoka magazeti ya zamani 

Sabato ni ya Waisraeli, Mungu alikwishaiondoa 
Na Muhibu Said 

Waislamu wachoma moto nguruwe 

Tume ya kubadili Katiba Kenya: Waislamu kuwakilishwa 

Waislamu Msonge waomba wanusuriwe 

Sayansi na Teknolojia 
[PELEKA FAX NCHI ZA NG’AMBO BURE! – (2)] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na Lishe 
[Mwongozo wa mlo wa kila siku] 
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita