|
|
|
Chifu Masanja katoka Tanu kaingia Congress CHIFU Francis Masanja wa Bukwimba na pia mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria, nchini Tanganyika alitangaza jana kwamba amejiuzulu katika TANU na kuingia chama cha Congress. Chifu Masanja ambae aliingia katika Baraza la Kutunga Sheria kwa tikiti ya TANU, amesema kwamba amechukua hatua hii baada ya kuona kile alichokiita mengine ya TANU sio ya faida kwa watu wa Tanganyika. Katika taarifa yake magazetini Masanja anasema: Sasa nimeingia Congress, nami nitatoa siasa yake katika Baraza la Kutunga Sheria kwa sababu nimeshawishiwa kabisa kwamba ndio chama cha pekee ambacho bila woga au upendeleo, kinachunga haki za binadamu na kutoa maoni ya kweli ya watu wa nchi hii. Sio Demokrasia Alisema pia kwamba mara nyingi alisikia malalamiko kutoka kwa wanachama wa Wilaya yake na nyingine juu ya mambo yasiyo ya kidemokrasia yanayoendeshwa na wakuu wengine wa TANU. "Kuna mambo mengine ambayo wakuu wa TANU waliwasumbua baba kabwela, bila ya kujali haki zao", alisema. Chifu Masanja pia anasema kwamba TANU, kwa kutaka kura za watu, ilitoa ahadi nyingi kwa watu katika uchaguzi uliopita, lakini imeshndwa kabisa kutimiza ahadi hizo. Akasema wapiga kura hawaridhiki. Hakuna Uhuru Taarifa hiyo pia imesema kwamba ikiwa hali hii itaendelea nchi itachafuka na hakutakuwa na uhuru, na hasa uhuru wa kusema. Alipoulizwa na mwandishi wetu kama amejiuzulu kwa sababu Uchifu umeondolewa, Masanja akajibu kwamba hiyo sivyo, na pia kwamba hana cheo chochote katika Congress bali ni mwanachama wa kawaida tu. Msemaji wa TANU alipoulizwa kutoa maoni yoyote alisema kuwa hakuwa na maoni. BAADA ya bendera ya Congress kutundikwa katika ofisi yao mpya huko Tanga, asubuhi mti wa bendera hiyo ukaonekana umekatwa na kuangushwa chini. Hivi majuzi mjini Tanga ilifanyika sherehe ndogo ya kufungua ofisi kuu ya Jimbo ya chama cha African National Congress mtaa wa Ngamiani, barabara ya 15. Katika sherehe hiyo, bendera nyekundu yenye alama nyeusi ya ‘T’ katikati ilitundikwa kama kawaida nje ya ofisi. Baada ya kupepea kwa kutwa moja siku ya pili ikaonekana kwamba mti wa bendera umekatwa na kuangushwa chini. Wakuu wa ofisi bado
hawajatoa tamshi lolote na wala haijulikani kitendo hicho kimefanywa na
nani, lakini polisi imearifiwa nayo inafanya uchunguzi.
|
YALIYOMO
Tahari
Kupokelewa kwa malalamiko ya Waislamu: Masheikh wasubiri ukweli wa Mkapa Afariki baada ya kutokwa damu nyingi: Yadaiwa hakuwa na sh. 4,000 Nyumba ya Wakfu iliyoporwa yarejeshwa Kamanda Gewe atakiwa amkamate Daniel Sheikh awasambaratisha walevi Liwale Msikiti wavamiwa na kuvunjwa milango, madirisha Msikiti wa Mwinyimkuu wafanya sensa Njaa hakuna, tunategemea kula silaha Mabaraza yawatetee Waislamu - Sheikh Bafadhil Hali ya Uislamu Lukulunge, Kongwa inatisha Waislamu Kondoa waagizwa kuyatunza magazeti ya ANNUUR Sabato ni ya Waisraeli, Mungu alikwishaiondoa
Tume ya kubadili Katiba Kenya: Waislamu kuwakilishwa Waislamu Msonge waomba wanusuriwe Sayansi na Teknolojia
Chakula na Lishe
|