AN-NUUR 
Na.182 Ramadhan 1419, Januari 1 - 7, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Jicho la Uzalendo
Na. Sompo wa Kahambwe
Bhabhoo! Muungwana huyoo!

Miaka ya nyuma mpaka kufikia mwishoni mwa miaka ya sitini, baadhi ya makabila hapa nchini yalijijengea utamaduni wa kutoa mafunzo ya kitabia kwa vijana waliofikia balegh, chini ya hapo kidogo au zaidi kiumri. 

Mafunzo hayo yaliyoendeshwa porini kwa masiku kadhaa, yalifahamika kama Jando au Jandoni kwa upande wa wavulana na unyago kwa mabinti (wana wari). 

Jandoni, wavulana walitahiriwa na kupewa mafunzo mbali mbali ya tabia na ukakamavu katika kipindi chote cha mauguzo.haya yalifanyika katika utaratibu maalum uliowekwa na wahenga wa kabila. 

vijana walilelewa hivyo kwa kipindi chote, lengo likiwa kudumisha mila na desturi za kabila, athari ya mafunzo hayo ilionekana katika maisha ya vijana. Wale ambao hawakupata fursa ya kupita "kambi" hizo walijulikana. Ndio tukajasikia maonyo na makaripio dhidi ya tabia mbovu kwamba wahusika hawakwenda jandoni kwa maana hawakupata mafunzo maalum au hawakupita katika tanuri la tabia, yaani si waungwana. Kwani Muungwana ni yule anayejiepusha na kila lenye kuudhi wengine. Hujitahidi kutenda yafaayo kisha watu wakamsifu kwayo. 

Yule mwenye tabia ya kujisifusifu si muungwana. Yule mwenye kiburi si muungwana. Mwenye kauli za kuudhi si muungwana, asiye na huruma kwa wengine si muungwana. Mwenye majivuno si muungwana, na kadhalika. 

Hayo ni mambo ya zamani jandoni, kama yapo mazuri yaliwanufaisha baadhi ya watu na kinyume. 

Katika toleo lililopita la gazeti hili ukurasa wa mbele nilisoma habari iliyohusu ziara ya Alhaji Ali Hasaan Mwinyi mkoa wa Mwanza. Kwa mujibu wa ripoti hiyo Wananchi wa mkoa huo, wenyeji kwa wageni walimlaki kwa shangwe na hoi hoi Rais huyo mstaafu wa awamu ya pili. 

Swali lililokuja mara tu baada ya kusoma habari hiyo ni kwa nini imekuwa ni kawaida kwa Rais huyo mstaafu kushangiliwa kila anapopita. Hapana shaka kuna mengi mazuri aliyoyafanya wakati wa kipindi chake cha uongozi kwa hiyo kutokana na hayo wananchi hushindwa kujizuia kila wamuonapo. Na huenda pia mashangilizi haya huwa na ujumbe wa namna fulani unaofikishwa na wananchi hao kwa watawala waliopo ambao inasemekana hawajafanya lolote tangu washike madaraka. Ndipo nikakumbuka kuwa Mzee Mwinyi anastahili hayo kwa sababu ni muungwana yeye aliyewalisha na kuwavika vizuri Watanzania baada ya kuwakuta hoi, fii na taabani chini ya kinyamkera cha "ujamaa na kujitegemea" cha awamu iliyomtangulia. Ni muungwana yeye aliyewatoa ngomeni Watanzania chini ya zidumu fikra sahihi za mtu fulani. 

Ni muungwana huyu aliyefungua demokrasia ya upashanaji wa habari ambayo awali ilitungikwa kitanzini chini ya jinamizi la Glanost! Ni muungwana yeye aliyesimamia kikamilifu mageuzi ya kisiasa yanayoonekana kupingwa na wahafidhina wenye kujali maslahi yao zaidi. 

Nchi chini ya uongozi wa Muungwana huyu na washauri wake wa karibu iling’ara kinyume na kabla yake halikadhalika baada yake. Kwa uungwana wa kwetu mgeni wa aina hii hustahili heshima ya pekee na tunakawaida ya kumkaribisha kwa "bhabhooooo" katika mji wetu uliojaa mapagala (vidunda) ya tangu uhuru! 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 

Tahariri 
Kingunge, kweli upo uonevu na dhulma

Wananchi wahoji kuhusu polisi aliyeua Arusha

Matokeo ya Darasa la Saba yacheleweshwa kusherehekea sikukuu ya Krismasi: Wananchi wahoji je, nchi hii ina dini moja tu?

Njaa yaikumba Kilwa

Dondoo za Saikolojia
Na. Abu Halima Sachangwa

Kona ya Wacha Mungu
Mavuno yangu yasiwe...

Jicho la Uzalendo: Bhabhoo! Muungwana huyoo!
Na Sompo wa Kahambwe

Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897)

Mafunzo kuhusu funga ya Ramadhani
Imetayarishwa na Africa Muslims Agency

Marekani ni mtetezi au adui wa haki?: Umoja wa Mataifa upo upande gani?
Na Abu Salim

Dawa ya ukimwi ni mwenendo mwema
Na Habiba Swedi, Arusha

Mwalimu Maif: Mwanamke aliyetumia maisha yake kufundisha Qur'an

Ijue  Madrasa Hudaa Arusha

Wazazi waaswa kutoshabikia maovu

Mzee maarufu afariki Moro

Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? (jibu) 
Na Ally Said

Mapinduzi, Muungano kwa manufaa ya nani?

Fufueni EAMWS - Sheikh Amana
Na Habiba Swedi

Msiitupie lawama serikali - Dk. Omar

Baada ya kuvunjiwa nyumba, kuchomewa vyakula na Serikali: Nzasa sasa wafuturu Maembe
Na Q. Mtaita

Acheni mifumo mibovu, fuateni Qur'an - Sheikh Kilemile

Sayansi na Teknolojia 
[Kuunganisha Kompyuta kwa Kutumia Modem

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Saumu na lishe ya mama anayenyonyesha] 
  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita