|
|
Wamesema taarifa hiyo iliyotolewa na baadhi ya vyombo vya habari imewaacha wananchi hao wakijiuliza maswali mengi kuliko majibu. Katikati ya wiki hii msemaji wa Wizara ya Elimu wakati akielezea moja ya sababu za kuahirishwa kutolewa matokeo ya mitihani ya darasa la saba mwaka huu mbele ya waandishi wa habari, alisema kama matokeo hayo yangetolewa kabla ya Krismasi watoto wa Wakristo ambao hawakuchaguliwa wasingesherehekea sikukuu ya Krismasi kwa furaha. Bw. Abeid Juma akiongea na gazeti hili alisema kwamba kauli hii inawakilisha dhana iliyojengeka miongoni mwa watendaji wa serikali kamba wanafunzi wote ni Wakristo tena basi wakusherehekea Krismasi. Kufuatia mawasiliano na wananchi waliotaka ufafanuzi wa maelezo ya Wizara, AN-NUUR iliwasiliana na Wizara ya Elimu kutaka kujua ukweli wa madai haya. Baada ya kumkosa Mh. Waziri na Katibu wake Mkuu, Msemaji mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake alikiri kwamba Katibu Mkuu wa Wizara alitoa sababu hiyo lakini akadai kuwa hiyo haikuwa sababu pekee. Hata hivyo hakutoa ufafanuzi zaidi. Kilichowafurahisha wananchi walioongea na gazeti hili ni kuona jinsi Wizara ilivyo makini na inavyojali na kuthamini hisia za kidini za wanafunzi katika utendaji wake. Hata hivyo, wamehoji je, nchi hii ina dini moja tu. Taarifa hizi za kucheleweshwa kutolewa
matokeo ya darasa la saba ili kuwawezesha watoto Wakristo kusherehekea
vizuri Krismasi zimekuja wiki moja tu baada ya gazeti hili kuripoti kuwa
wanafunzi Waislamu watalazimika kufanya mitihani ya kidato cha nne ndani
ya Ramadhani na pengine kuikosa Id el Fitr.
|
YALIYOMO
Tahariri Kingunge, kweli upo uonevu na dhulma Wananchi wahoji kuhusu polisi aliyeua Arusha Dondoo za Saikolojia
Kona ya Wacha Mungu
Jicho la Uzalendo: Bhabhoo! Muungwana
huyoo!
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) Mafunzo kuhusu funga ya Ramadhani
Marekani ni mtetezi au adui wa haki?:
Umoja wa Mataifa upo upande gani?
Dawa ya ukimwi ni mwenendo mwema
Mwalimu Maif: Mwanamke aliyetumia maisha yake kufundisha Qur'an Wazazi waaswa kutoshabikia maovu Je, hivi tuendelee kushika amri za
Mungu tena? (jibu)
Mapinduzi, Muungano kwa manufaa ya nani? Fufueni EAMWS - Sheikh Amana
Msiitupie lawama serikali - Dk. Omar Baada ya kuvunjiwa nyumba,
kuchomewa vyakula na Serikali: Nzasa sasa wafuturu Maembe
Acheni mifumo mibovu, fuateni Qur'an - Sheikh Kilemile Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|