AN-NUUR 
Na.179 Shaaban  1419, Desemba 11 - 17, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Mashairi

Chuki kafukuzwa 

Bismillah muhimu, kwa wingi wa ukarimu, 
Asaalam aleykumu, ama baada ya salamu, 
Ndugu zangu Islamu, ni letu hili jukumu, 
Kufukuzwa kwake Chuki, tujaribu tafakari. 

Kaletwa hospitali, matibabu akapewa, 
Imefikia mahali, ikanenwa wamtowe, 
Hiyo kweli ni kauli, halali atamkiwe? 
Kufukuzwa kwake Chuki, tutafute muafaka. 

Waislamu tukae, mawazo tukapeane, 
Fikra zetu tutoe, vifua tusivibane, 
Mikakati tuandae, itujenge tupambane, 
Kufukuzwa kwake Chuki, tutafute muafaka. 

Huo jama mtihani, katuletea Manani, 
Hapa hapa duniani, ni Yeye alotupeni, 
Ili atutathimini, atakaye kufu nani, 
Kufukuzwa kwa Chuki, dhamira hasa ni nini? 

Ndugu yetu kaka yetu, ni ndani ya yetu dini, 
Mabinti nusra yetu, tena wanne jamani, 
Wasiwasi ndani yetu, la kufanya hatuoni, 
Kufukuzwa kwake Chuki, tunayo mengi majonzi. 

Wabillah Tawfiq, mbele sitaendelea, 
Natusiwe wanafiki, madhalimu kuwalea, 
Kamwe nyuma hatubaki, mbele tutaendelea, 
Kwa wetu mshikamano, Inshallah tutafuzu. 
 

Aula Tinda, 
S.L.P. 1573, 
DAR ES SALAAM. 


Mtukufu Ramadhani 

Bismillahi naanza, kwa jina lake muweza, 
Nilo nayo kueleza, mupate kuyasikia, 
Ya muhimu kuwajuza, na ya kheri kuyajua, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Mtukufu Ramadhani, sasa kishatufikia, 
Tumjue kwa makini, kuwa ni kujizuia, 
Kutia kitu kinywani, na maasi yote pia, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Tufunge kwa lengo lake, ucha Mungu kufikia, 
Pia umuhimu wake, tupate kuutambua, 
Tuzipate radhi zake, kwa kutekeleza Twaa, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Mwezi huu Qur'an, ndio imetushukia, 
Kafaradhisha Manani, kwa watu kujifungia, 
Nguzo zake kwa yakini, nia na kujizuia, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Nia kila Isilamu, moyoni kukusudia, 
Kujizuia muhimu, alfajiri sawia, 
Hadi jioni kutimu, bila ya kuingilia, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Katika yaliyo Sunna, ni kufuturu mapema, 
Na daku usiku sana, na Qur'an kusoma, 
Na kuwa karibu sana, na kwa swala kusimama, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Kufanya mema muhimu, na miezi ilosalia, 
Kwa kutafuta elimu, na swala kujiswalia, 
Zaka na hija kutimu, kila ovu kuondoa, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Kama unalazimika, mwezi ukiusikia, 
Ufunge bila mashaka, hadi siku kutimia, 
Viwanjani kufurika, Iddi kwenda jiswalia, 
Karibu mgeni wetu, mtukufu Ramadhani. 

Juma M. Bwanakheri, 
(Ustaadh), 
S.L.P. 45245, 
DAR ES SALAAM. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Maoni
Waislamu tunakusudiwa kufanywa watumwa wa nani?

Wananchi waingiwa na hofu kuhusu silaha

Serikali yagwaya kwa wafugaji nguruwe 
Na Muhibu Said

Hakuna njama za kupindua Bakwata - Sheikh Yahya

MARADHI YA KISAIKOLOJIA:: VOYEURISM
Na. Abu Halima Sachangwa

Tathmini: Miaka 37 ya uhuru wa Tanganyika
Na Maalim Mwalimu

Adabu katika swala

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo: Batendi hakumuelewa Mkomidachi
Na Ally Said

Muhammad (s.a.w.) katika Unabii wa Isaya  (a.s.)
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa, Korogwe

Ijue SUA Madrasa Moro
Na Mussa Ally, Morogoro

Kiteto wakosa darsa kwa kupinga Ramli

Ustadh ayeyuka na saruji ya Msikiti mjini Arusha

Akina mama Muheza waungana kufanya Daawa
Na B. Mwakangwale

Wanafunzi Waislamu Mbeya wapata uongozi
Na B.  Mwakangwale

Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 2
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu

Njia ya uzima ni nyembamba,  waionao ni wachache - 2
Na Yasin Valerian Massawe

Waandishi andikeni ukweli - Kamati
Na Mwandishi Wetu

Sheikh Jongo  aichachamalia Uwawaru
Na Badru Kimwaga

Waamriwa kurejesha Mali ya Mirathi
Na Njuki  A.

Waislamu Mlimba Moro mashakani
Na Q. Mataita

Sayansi na Teknolojia 
[Ielewe Modem yako] 
 
Mafundisho ya Quran

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Futari ya Tende] 
 
Tangazo
Vitabu na Mihutasari ya Maarifa ya Uislamu
 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita