|
|
Hakuna
njama za kupindua Bakwata - Sheikh Yahya
Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake mtaa wa Kagera Mwembechai Jijini Dar es Salaam, kiongozi huyo wa Bakwata amesema kuwa tuhuma hizo si za kweli na kwamba zimelenga kujenga hofu isiyo na msingi. Sheikh Yahya amezihusha tuhuma hizo na mtafaruku uliomo Bakwata hivi sasa baina ya viongozi wake na kusema kwamba huenda ni baadhi ya viongozi wa baraza hilo walioneza uzushi huo. "Hizi ni njama zimefanywa na baadhi ya uongozi wa Bakwata ili kuleta hofu kwa Mufti na akubaliane na uongozi huo juu ya ubaya wa wale wasiotakiwa", amesema Sheikh huyo. Aliongeza kusema kuwa hakuna njama hizo na kama zingalikuwepo yeye angelifahamu mapema. Hata hivyo, alikiri kupigiwa simu na mtu ambaye hakumfahamu kutoka mahali alipokuita "nyeti" akieleza kuhusu njama hizo. Aidha alisema, Waislamu wanaelewa wazi njia ya kuichukua Bakwata si kuivamia bali kuitikia wito wa Mufti Hemed bin Juma wa kujiunga na Bakwata na kushiriki uchaguzi. Alituhumu kuwepo kwa njama zinazopangwa na baadhi ya viongozi wakuu wa baraza kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wakubwa serikalini dhidi yake na Mufti. Wiki iliyopita gazeti hili liliripoti kuhojiwa kwa baadhi ya Masheikh jijini kuhusiana na tuhuma zilizodaiwa kuwepo polisi juu ya mpango wa kupindua uongozi wa Bakwata makao makuu. Hata hivyo, haikuweza kufahamika tuhuma hizi zilifikaje polisi na kwa vipi Masheikh waliotajwa walihusika na mpango huo. ndani ya Bakwata |
YALIYOMO
Maoni
Wananchi waingiwa na hofu kuhusu silaha Serikali yagwaya kwa wafugaji
nguruwe
Hakuna njama za kupindua Bakwata - Sheikh Yahya MARADHI YA KISAIKOLOJIA:: VOYEURISM
Tathmini: Miaka 37 ya uhuru wa Tanganyika
Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo:
Batendi hakumuelewa Mkomidachi
Muhammad (s.a.w.) katika
Unabii wa Isaya (a.s.)
Ijue SUA Madrasa Moro
Kiteto wakosa darsa kwa kupinga Ramli Ustadh ayeyuka na saruji ya Msikiti mjini Arusha Akina mama Muheza waungana kufanya
Daawa
Wanafunzi Waislamu Mbeya wapata
uongozi
Je, hivi tuendelee kushika amri
za Mungu tena? - 2
Njia ya uzima ni nyembamba,
waionao ni wachache - 2
Waandishi andikeni ukweli - Kamati
Sheikh Jongo aichachamalia
Uwawaru
Waamriwa kurejesha Mali ya
Mirathi
Waislamu Mlimba Moro mashakani
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|