AN-NUUR 
Na.179 Shaaban  1419, Desemba 11 - 17, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Akina mama Muheza waungana kufanya Daawa
Na B. Mwakangwale

WANAWAKE Waislamu wilayani Muheza wameunganisha juhudi zao kwa lengo la kuimarisha harakati za Kiislamu wilayani hapo halikadhalika kujiletea maendeleo ya kiuchumi. 

Habari zaidi zimeeleza kwamba akina mama hao Waislamu wa Muheza mjini wamefanikiwa kuwaunganisha akinamama kutoka Misikiti mbalimbali pamoja na wale walioko mitaani wanaofanya biashara ndogondogo. 

Katika kuimarisha mtandao wao, wanawake hao wameshavitembelea vijiji vya Mkuzi, Kwamhosi, Tingeni, Ubembe, Magila, Tanganyika, Kisiwani na Mkumbi. 

Zaidi ya kuwaunganisha akina mama Waislamu kwa lengo la kuwapa elimu; mafanikio mengine yaliyopatikana kutokana na juhudi hizi mpya ni pamoja na kuwaita wengine katika Uislamu. 

Tayari wanawake hao wameshawasilimisha wanawake saba ambao walikuwa Wakristo. 

Jingine ambalo laweza kutajwa kama ni mafanikio ni moyo wa kujitolea ambapo wanapoandaa semina zao hawangoji mfadhili. Bali huja na vyakula vyao toka majumbani na kujigharamia mahitajio mengine. 



Wanafunzi Waislamu Mbeya wapata uongozi 
 
  • TAMSA Mbeya yazinduliwa rasmi
Na B. Mwakangwale

WANAFUNZI wa Kiislamu wanaosoma katika shule za sekondari na vyuo mbalimbali mkoani Mbeya wamefanya uchaguzi wa viongozi upya na wakati huo huo wamezindua rasmi Jumuiya mpya ya wanafunzi wa Kiislamu mkoani humo imefahamika. 

Jumuiya hiyo inayojulikana kama TAMSA tawi la Mbeya, inaundwa na taasisi zipatazo kumi na tisa ikijumuisha sekondari na vyuo vilivyopo katika Manispaa ya Mbeya na baadhi yake viko katika wilaya. 

Baadhi ya vyuo na shule hizo ni shule ya sekondari Iyunga, Loleza, Sangu, Meta, Mbeya, Mbalizi,Ivumwe, Itende, Meta shule ya ufundi, pamoja na vyuo vilivyomo ni Jakaranda chuo cha ufundi, Chuo cha Uganga - Mbeya M.M.T.C., Chuo cha Kilimo Uyole. 

Vingine ni Chuo cha Uhasibu DSA, Chuo cha Ufundi Mbeya M.T.C. 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni, mwanafunzi muhitimu katika Chuo cha Ufundi Mbeya Hamisi Mikidadi alizitaja baadhi ya taasisi na shule zilizo wilayani kuwa ni Chuo cha Ualimu Tukuyu, sekondari ya Kipoke, Ndembele, Lutungano pamoja na sekondari ya Mwakalelinzi. 

Aliongeza kusema zoezi la kusajili shule na vyuo vingine bado linaendelea. 

Aidha, muhitimu huyo alisema, zito zaidi ni ukosefu wa vijana wa Kiislamu katika shule na vyuo mkoani humo hii ilitambulika muda mchache baada ya kufanyika kikao kikuu cha viongozi wote mashuleni na vyuoni hapo Oktoba 10, mwaka huu katika chuo cha ufundi Mbeya M.T.C. 

Kabla ya tawi la TAMSA Mbeya, zamani ilitambulika kama MUWAKI - Mbeya, yaani Muungano wa Wanafunzi wa Kiislamu Mbeya. 

Akieleza kwa ufupi MUWAKI ilivyoanzishwa mwaka 1986. Wazo la kuanzishwa lilitolewa na mwanafunzi Ramadhani Sanze wa M.T.C. 

Jumuiya zilizounda MUWAKI kipindi hicho zilikuwa ni MTC Loleza pamoja na Uyole. 

Alipohojiwa zaidi na mwandishi wa habari hizi ni sababu zipi zilizopelekea kubadilisha MUWAKI na kuwa TAMSA, alisema kuwa MUWAKI ilikuwa haina katiba na wakati wa likizo MUWAKI , haina matamko rasmi, kutokamilisha majukumu yake, pia ilikuwa haitambuliki nje ya mkoa pamoja na wilayani. 

Vile vile uongozi wa TAMSA - Mbeya ulikubaliana pawe na uongozi wa kudumu, kwa kufanya hivyo itasadia endapo wanafunzi wamalizapo shule na vyuo, TAMSA isiweze kuyumba kwa kukosa kumbukumbu. 

Pia TAMSA tawi la Mbeya ina mlezi wake ambaye ni Msafiri Njelambala, katika kamati ya Da’awah wapo Ustaadh Sudi, Ally Hashim, Fundi pamoja na Abdulrahamani. 

Akielezea matatizo ya TAMSA Mbeya alisema ofisi ya muda iliyoko M.T.C pindi chuo kinapofungwa kumbukumbu hupelekwa kwa Katibu Mtendaji ambaye ni mfanyakazi wa TAMSA - Mbeya, haina miradi na kuwa michango ya wanafunzi haitoshelezi mahitaji muhimu. Mfano kuzitembelea taasisi zilizopo nje ya mji pamoja na upungufu wa vitabu vya elimu ya dini pamoja na misahafu. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Maoni
Waislamu tunakusudiwa kufanywa watumwa wa nani?

Wananchi waingiwa na hofu kuhusu silaha

Serikali yagwaya kwa wafugaji nguruwe 
Na Muhibu Said

Hakuna njama za kupindua Bakwata - Sheikh Yahya

MARADHI YA KISAIKOLOJIA:: VOYEURISM
Na. Abu Halima Sachangwa

Tathmini: Miaka 37 ya uhuru wa Tanganyika
Na Maalim Mwalimu

Adabu katika swala

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo: Batendi hakumuelewa Mkomidachi
Na Ally Said

Muhammad (s.a.w.) katika Unabii wa Isaya  (a.s.)
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa, Korogwe

Ijue SUA Madrasa Moro
Na Mussa Ally, Morogoro

Kiteto wakosa darsa kwa kupinga Ramli

Ustadh ayeyuka na saruji ya Msikiti mjini Arusha

Akina mama Muheza waungana kufanya Daawa
Na B. Mwakangwale

Wanafunzi Waislamu Mbeya wapata uongozi
Na B.  Mwakangwale

Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 2
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu

Njia ya uzima ni nyembamba,  waionao ni wachache - 2
Na Yasin Valerian Massawe

Waandishi andikeni ukweli - Kamati
Na Mwandishi Wetu

Sheikh Jongo  aichachamalia Uwawaru
Na Badru Kimwaga

Waamriwa kurejesha Mali ya Mirathi
Na Njuki  A.

Waislamu Mlimba Moro mashakani
Na Q. Mataita

Sayansi na Teknolojia 
[Ielewe Modem yako] 
 
Mafundisho ya Quran

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Futari ya Tende] 
 
Tangazo
Vitabu na Mihutasari ya Maarifa ya Uislamu
 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita