AN-NUUR 
Na.179 Shaaban  1419, Desemba 11 - 17, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Dondoo za Saikolojia 

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: 
 

VOYEURISM 

Na. Abu Halima Sachangwa 

KATIKA makala zangu zilizopita, nilikuwa nikizungumzia matatizo ya kisaikolojia kuhusu uoni wa watu katika masuala mbalimbali. Leo nitaanza kuangalia maradhi ya kisaikolojia ambayo yameivamia jamii yetu na yanaendelea kuwaathiri watu kwa kasi ya ajabu, hasa wanapokuwa nje ya kanuni na maadili ya Kiislamu. 

Maradhi haya hujulikana kama Paraphilia ambapo mtu anakuwa na tabia za ajabu na mbaya,kama tutakavyoziona. Paraphilia zote hukithiri katika jamii ambayo watu wake wamezama kwenye zinaa. Zinaa siku hizi katika jamii yetu imekuwa sio dhambi, na imekuwa ni jambo la kawaida lisilo hata na kificho. Matokeo yake watu wengi wamekuwa na maradhi haya ya kisaikolojia ya Paraphilia . Baadhi ya Paraphilia nitakazozingumzia katika makala zangu ni hizi zifuatazo. 

1. Voyeurism. 

2. Sexual sadism. 

3. Frotteurism. 

4. Exhibitionism. 

5. Fetishism. 

6. Transvexualism. 

7. Transvestism. 

8. Pedophilia. 

9. Sexual Mosochism. 

10. Homosexualism/Lesbianism. 

Usitishike na majina hayo kwa lugha ya kigeni. Kila kimoja tutajitahidi kukielezea kwa ufasaha wake katika lugha ya Kiswahili. 

Voyeurism: Tukianza na maradhi ya kwanza, Voyeurism ni maradhi ya kisaikolojia ambapo mwenye maradhi haya anakuwa na tabia ya kupenda kuangalia watu wasio na nguo. Mtu mwenye maradhi haya huitwa kitaalamu Voyeur (inasomwa vouya). Kwa Kiingereza cha kawaida, mtu huyu huitwa Peeping Tom, Waswahili humwita kozimeni. 

Mara nyingi Voyeur huwa na tabia ya kuchungulia watu walio kwenye faragha, na yeye roho yake hufurahi kuwaona watu walio wazi bila nguo, na furaha yake hufikia kilele kama atawaona mke na mume wako katika kitendo cha ndoa. 

Katika jamii yetu leo, maradhi haya yameingia kwa kasi. Tunao watu wengi waliozama hapa, na iko haja ya kupambana na maradhi haya, na hakuna anayeweza kupambana nayo bali Waislamu. Siku hizi, wenye maradhi haya huwezi kuwakuta wanachungulia madirishani au sehemu nyingine, kwa sababu wanaweza kushikwa na kuchomwa moto. Kuna mbinu mpya za kukidhi haja ya wenye maradhi haya. Zamani kulikuwa na senema za X. Siku hizi kuna kanda za video, hawa akina Peeping Toms hujifungia ndani na kuanglia kanda hizi. Hawa ni wagonjwa mahututi. 

Kuna wagonjwa wengine ambao sio mahututi, lakini nao pia ni ma Voyeur. Kwa mfano, binti wa Kiislamu anaweza akaomba avae hijabu shuleni, lakini wapo watu hawakubali binti huyu afunike viungo vyake. Utamkuta mwalimu anakuwa mkali kabisa, kwani na yeye ni miongoni mwa watu ambao roho zao haziridhiki mtu, hasa mwanamke anapojihifadhi. Hawa ndio wale wale ambao huandaa kile kinachoitwa "mashindano ya uzuri" na kuwapitisha mabinti waliovaa "vichupi" mbele ya kadamnasi, na mwisho huwapa zawadi. Kwa bahati mbaya sana, wenye maradhi hawa ni pamoja na viongozi wa nchi. Wao hufungua na kushiriki katika mambo haya ya kukodolea macho watu walio uchi. 

Mtume amesema: "Jinsi mlivyo, ndivyo mtakavyotawaliwa", kwa hivyo, kama viongozi wetu ni ma Peeping Tom na ma Voyeur, au Makozimeni, je wanaoongozwa. 

Kiboko ya maradhi haya hakuna zaidi ya Uislamu kwani ndio unaotekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu yasemayo: "Wala msiikurubie zinaa hakika hiyo ni uchafu na njia mbaya kabisa". (Qur. 17:32) 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Maoni
Waislamu tunakusudiwa kufanywa watumwa wa nani?

Wananchi waingiwa na hofu kuhusu silaha

Serikali yagwaya kwa wafugaji nguruwe 
Na Muhibu Said

Hakuna njama za kupindua Bakwata - Sheikh Yahya

MARADHI YA KISAIKOLOJIA:: VOYEURISM
Na. Abu Halima Sachangwa

Tathmini: Miaka 37 ya uhuru wa Tanganyika
Na Maalim Mwalimu

Adabu katika swala

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo: Batendi hakumuelewa Mkomidachi
Na Ally Said

Muhammad (s.a.w.) katika Unabii wa Isaya  (a.s.)
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa, Korogwe

Ijue SUA Madrasa Moro
Na Mussa Ally, Morogoro

Kiteto wakosa darsa kwa kupinga Ramli

Ustadh ayeyuka na saruji ya Msikiti mjini Arusha

Akina mama Muheza waungana kufanya Daawa
Na B. Mwakangwale

Wanafunzi Waislamu Mbeya wapata uongozi
Na B.  Mwakangwale

Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 2
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu

Njia ya uzima ni nyembamba,  waionao ni wachache - 2
Na Yasin Valerian Massawe

Waandishi andikeni ukweli - Kamati
Na Mwandishi Wetu

Sheikh Jongo  aichachamalia Uwawaru
Na Badru Kimwaga

Waamriwa kurejesha Mali ya Mirathi
Na Njuki  A.

Waislamu Mlimba Moro mashakani
Na Q. Mataita

Sayansi na Teknolojia 
[Ielewe Modem yako] 
 
Mafundisho ya Quran

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Futari ya Tende] 
 
Tangazo
Vitabu na Mihutasari ya Maarifa ya Uislamu
 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita