AN-NUUR  Na.174 Rajab 1419, Novemba 6 - 12, 1998 
 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Lishe na kansa ya titi
 
Na Mujahid Mwinyimvua

KATIKA makala yetu ya chakula na lishe ya wiki iliyopita tulijifunza kwa ujumla kwamba chakula ni silaha inayoweza kumsaidia mtu kupunguza kama sio kuondoa kabisa uwezekano wa kupata ugonjwa wa kansa. Kwa maneno mepesi anaweza kusema kuwa tukifuata kanuni na taratibu za chakula na lishe tunaweza kwa kiasi kikubwa kuepuka ugonjwa wa kansa. Makala yetu ya wiki hii ni mwendelezo wa somo la wiki iliyopita. Kansa ya titi (Breast Cancer) ambayo tutajifunza wiki hii ni moja ya aina ya ugonjwa wa kansa. 

Ugonjwa huo ni tatizo linalowasumbua mamilioni ya watu hasa wanawake katika nchi mbalimbali hapa ulimwenguni. 

Kwa upande wa wanawake, ugonjwa wa kansa ya titi unachangiwa na sababu kadhaa, baadhi yake ni zile ambazo hatuwezi kuzidhibiti. Kwa mfano historia ya wazazi (ukoo) kama walikuwa na ugonjwa huo, kuanzia siku za mwezi (Menstruation) katika umri mdogo na kutokuzaa. 

Sababu nyingine (ambayo tunaweza kuidhibiti) ya titi ni aina ya vyakula tunavyokula na matokeo ya vyakula hivyo. Kwa mfano vyakula vyenye mafuta (Cholesterol) ni kichocheo kikubwa cha kansa ya titi. 

Vile vile kuwa na uzito mkubwa (matokeo ya vyakula) ni kichocheo cha kansa ya titi. Makala zetu za nyuma zilieleza kwa kina sababu na njia za kudhibiti uzito wa miili yetu, hivyo basi katika makala hii sitarudia maelezo hayo. 

Baada ya utangulizi huo, ni vyema sasa tukapata ushauri nasaha wa lishe juu ya njia za kupunguza uwezekano wa kupata kansa ya titi. 

Kwanza watu wajitahidi kupunguza kula vyakula vyenye mafuta. Kama vile mayai ni chanzo kikubwa cha mafuta yajulikanayo kama "Cholesterol" ambayo ni kichocheo kikubwa cha kansa na magonjwa mengine kama yale ya moyo, ni vyema pia watu wakapunguza kiwango cha kuyala. 

Baadhi ya watafiti wanashauri katika kukabiliana na kansa, mtu ale yai moja au mayai mawili kwa wiki. 

Pili, watu waongeze kula vyakula vyenye vitamini A na C. Wataalamu wanasema kuwa wanawake wenye virutubisho hivyo mwilini wana uwezekano mdogo wa kupata ugonjwa wa kansa ya titi. 

Tatu, watu wale vyakula vyenye madini joto (Iodine) na madini ya selenium. Utafiti umeonyesha kwamba upungufu wa madini hasa ya madini joto unazifanya chembe chembe hai (cells) za kwenye matiti zikuwe vibaya na hivyo kuleta ugonjwa wa kansa ya titi. Madini joto na yale ya Selenium yanapatikana kwa wingi katika vyakula vinavyotoka baharini (samaki, dagaa, n.k.) na vyakula vya punje punje (mahindi, mchele, n.k.) 

Nne, watu wale zaidi maharage badala ya nyama. Maharage yana vitu vinavyoitwa "Proteanse inhibitors" ambavyo vinazuia kutokea kwa kansa. 

Tano, watu wajiepushe na vyakula na vinywaji kama vile kahawa, chai, cola na chocolate. Vyakula hivyo vina vitu vinavyoitwa ‘methylxanthines’ ambavyo vinahusishwa na ugonjwa wa ‘Fibrocystic’. 

Zaidi ya hayo, watu hasa wanawake wanashauriwa kwamba: Kila siku japo mara moja wakae faragha na wajichunguze matiti yao kama yana dalili za kansa ya titi. Baadhi ya dalili hizo ni kama vile kutokwa damu, usaha, maji maji n.k. katika matiti. 

Pia kujisikia maumivu au dalili yoyote ile katika matiti ambayo unaiyona siyo ya kawaida kama umegundua hali yoyote ile mfano wa maelezo ya hapo juu au nje ya hayo, haraka wahi hospitalini kwa ushauri nasaha au tiba. Ukichelewa tatizo litakuwa kubwa kwa hiyo si rahisi kupata ufumbuzi wake. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI  
Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha 

Serikali yakumbushwa kujiunga OIC 
Na Mwandishi wetu 

Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi 

Wafungwa waomba Futari na Vikoi 

Macho ya shutuma 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Hoja pofu 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Tafuteni ufalme wa kisiasa 

Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 

'Vichupi' vya nini Kimiti? 
Na. Said Rajab 

Mjadala wa Katiba na haki za Waislamu 
Na Masoud Mohammed Mbogo 

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 3 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Waliochukuliwa utumwa Uarabuni 
Na Hassan Omar 

Madrasatul Maamury Islamiya 

Teknologia: Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4) 
Na Hassan Omar 

Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito 

TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' 

Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa  

Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza 

Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga 

Mafunzo ya Qur'an  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa 

Barua za wasomaji  

Masomo ya dini ya Kiislam  

Chakula na lishe 

Mashairi 

Matangazo 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita