AN-NUUR  Na.174 Rajab 1419, Novemba 6 - 12, 1998 
 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi

IMAM wa Msikiti Mujahidiin uliopo Mburahati Jijini, Sheikh Juma Mbukuzi amesema kabla ya kukamatwa usiku wa manane Jumanne wiki iliyopita aliamriwa kutoka nje ya nyumba yake ambako askari polisi walitanda kuzunguka nyumba hiyo.

Sheikh Mbukuzi alieleza hayo katika kongamano la Waislamu lililoandaliwa na baraza kuu la jumuiya na taasisi za kiislamu ambalo lilifanyika Temeke Jumapili iliyopita.

"Niligongewa usiku wa manane, nilipochungulia dirishani niliwaona askari wakiwa wametanda, alieleza kwa ufasaha Sheikh Mbukuzi huku akisikilizwa kwa makini na Waislamu waliofurika katika kongamano hilo.

Sheikh huyo maarufu Jijini, aliendelea kusema kwamba walichukuliwa yeye na mwenzie kisha wakapelekwa kituo cha polisi cha jirani ambako waliamriwa kuvua viatu na kuswekwa ndani hadi kulipopambazuka. 

Sheikh Mbukuzi alisema kutoka kituo hicho walipelekwa kituo kikuu cha Polisi (Central Police) ambako walielezwa sababu za kukamatwa kwamba wanatuhumiwa kuhusika na kutishia maisha ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Luteni Yusuf Makamba.

Alisema alipohoji ni kwa vipi ahusishwe na tishio hilo, alionyeshwa "barua" inayodaiwa kuwa na tishio hilo aliyoandikiwa bw.Makamba na watu wasiojulikana.

Aidha Polisi walimtaka yeye binafsi afikirie ni kwa vipi ahusishwe na jambo hilo.

"Niliwaeleza labda kwa vile nilikamatwa kuhusiana na kadhia ya Mwembechai", alisema Sheikh Mbukuzi.

Hata hivyo alisema polisi hao waliikana sababu hiyo na kumtaka afikirie sababunyingine.

Aliwaambia kwamba huenda amefitiniwa na baadhi ya watu wa eneo lake ambao hawakufurahishwa na yeye kushinda uchaguzi uliofanyika eneo hilo.

"Niliombwa na vijana pamoja na akinamama wa pale mtaani nigombee Uenyekiti wa NGO moja ya eneo letu nikakubali, ulipofanyika uchaguzi mimi niliibuka mshindi kwa kura nyingi, alieleza Sheikh Juma.

Kwa hiyo alieleza Imam huyo kuwa huenda kutokana na ushindi huo baadhi ya watu wamejenga chuki dhidi yake.

"Nadhani ni kutokana na chuki hii baadhi ya watu wameamua kunifitini, ni demokrasia gani hii? Alieleza na kuhoji Sheikh Mbukuzi.

Kwa mujibu wa maelezo yake shauri hilo bado liko polisi hivi sasa na yeye yuko nje kwa dhamana. 

Jitihada za kumpata msemaji wa polisi kuhusiana na suala hili hadi gazeti hili linakwenda mitamboni hazikuweza kufanikiwa. 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI  
Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha 

Serikali yakumbushwa kujiunga OIC 
Na Mwandishi wetu 

Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi 

Wafungwa waomba Futari na Vikoi 

Macho ya shutuma 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Hoja pofu 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Tafuteni ufalme wa kisiasa 

Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 

'Vichupi' vya nini Kimiti? 
Na. Said Rajab 

Mjadala wa Katiba na haki za Waislamu 
Na Masoud Mohammed Mbogo 

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 3 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Waliochukuliwa utumwa Uarabuni 
Na Hassan Omar 

Madrasatul Maamury Islamiya 

Teknologia: Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4) 
Na Hassan Omar 

Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito 

TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' 

Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa  

Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza 

Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga 

Mafunzo ya Qur'an  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa 

Barua za wasomaji  

Masomo ya dini ya Kiislam  

Chakula na lishe 

Mashairi 

Matangazo 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita