AN-NUUR  Na.174 Rajab 1419, Novemba 6 - 12, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Mafundisho ya Quran 
  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa
 

Aya ya 268 na 269 

  

Shetani anakuogopesha ufukara na anakuamrisheni ubakhili; na Allah anakuahidini msamaha utokao kwake na ihsani. Na Allah ni Mwenye wasaa mkubwa na Mwenye kujua. 

Humpa hekima amtakaye na anayepewa hikima bila shaka amepewa kheri nyingi. Na hawakumbuki ila wenye akili. 

Mtiririko tuliokuwa tunaendelea nao hapo juu kwenye aya zilizotangulia ilikuwa umejikita na suala la kutoa. Bado aya hii na inayofuatia ziko kwenye maudhui hiyo hiyo ya kutoa ingawa kwa namna njia tu. 

Hapa Allah anakwenda kwenye chimbuko la watu kuwa wagumu wa kutoa mali zao kwenye njia ya Allah au kufanya jambo jengine ambalo kwa uoni wake halimpatii mapato au tija ya haraka haraka inayoweza kufanyiwa hisabu ya faida na hasara. 

Ni katika maumbile ya binadamu kukimbia kila anachokihisi kuwa kitakuwa ni chimbuko la hasara au matatizo kwake. Kwa mtu anayeona dunia mwisho wake ni kifo na hakuna maisha baada ya haya kutoa bila ya kuingiza kwake hakuna tofauti na kujitia kwenye ufakiri au umasikini wa kujitakia. 

Ukweli wa mambo ni kuwa anayetoa ni Allah na anayenyima au kumpokonya aliyempa ni Yeye na siyo binadamu yeyote. Hata hivyo hii ni daraja ya imani hivyo kwa wengi bado wasiwasi wa kufilisika upo wakati wa kutoa isipokuwa tu akiona yapo manufaa ama ya dhahiri au yaliyofichikana. 

Mpangilio wa Allah ni kila mtu anaptoa ndipo anapojiongezea hivyo hapana haja ya wasiwasi wa kufilisika. Kujiongezea huko kuna maana zote mbili – kuongeza kwa mali hapa hapa duniani au kukuta malipo huko akhera ambayo yatakuwa mengi mno kama tulivyokwisha sema au kuelezea huko nyuma. 

Utaratibu wa Allah ni kulipa kumi kwa kila jema moja; jambo hili limethibitishwa katika maisha ya binadamu wa zama tofauti. 

Kutokana na sababu ya kuogopa kufilisika ni katika mbinu ya shetani ya kuwazuilia binadamu kufanya mema. Mbinu za shetani ni nyingi na miongoni mwao ni hii na nyingine ni zile alizozielezea Allah katika Suratul Nisaa (aya ya 117 hadi 119): 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI  
Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha 

Serikali yakumbushwa kujiunga OIC 
Na Mwandishi wetu 

Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi 

Wafungwa waomba Futari na Vikoi 

Macho ya shutuma 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Hoja pofu 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Tafuteni ufalme wa kisiasa 

Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 

'Vichupi' vya nini Kimiti? 
Na. Said Rajab 

Mjadala wa Katiba na haki za Waislamu 
Na Masoud Mohammed Mbogo 

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 3 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Waliochukuliwa utumwa Uarabuni 
Na Hassan Omar 

Madrasatul Maamury Islamiya 

Teknologia: Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4) 
Na Hassan Omar 

Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito 

TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' 

Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa  

Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza 

Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga 

Mafunzo ya Qur'an  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa 

Barua za wasomaji  

Masomo ya dini ya Kiislam  

Chakula na lishe 

Mashairi 

Matangazo 
 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita