AN-NUUR  Na.174 Rajab 1419, Novemba 6 - 12, 1998 
 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Madrasatul Maamury Islamiya
 

MADRASATUL Maamury Islamiya ipo nyumbani kwa mlezi wa madrasa hiyo marehemu Abdurahmani Mkambi, Sinza madukani mkoa wa Dar es Salaam. 

Madrasa hii ilianzishwa na Maustaadh watano lakini wawili ndio ambao wamepatikana mmoja aitwaye Ramadhani Khamisi (Kwangaya) mwalimu mkuu na Habibu Kidodi msaidizi. 

Madrasa hii ilianzishwa mnamo mwaka 1994 ikiwa na wanafunzi 23 wavulana kwa wasichana kwa kipindi hicho walimu walifanya kazi kubwa ya kuwafundisha wanafunzi na wakawa wanaongezeka siku hadi siku. 

Mpaka hivi sasa wapo wanafunzi 86, wasichana kwa wavulana, masomo yanayotolewa madrasani hapo ni Tawhiid, Sira, Lugha ya Kiarabu, Akhlaq, Fiqh na Qur’an na tafsiri yake. 

Kwa sasa madrasa hii imesajliwa na Jumuiya ya Walimu wanaosomesha Qur’an Tanzania (JUAKUTA) na inafuata silabasi zao. 

Mpaka sasa madrasa ina walimu kumi na wameanzisha kitendo cha chekechea ikiwa ni miongoni mwa masomo yanayofundishwa madrasani hapo. 

Madrasa hii imebahatika kuwapata viongozi wa madrasa ukiachilia mbali walimu waliotajwa hapo awali, viongozi hao ni Mama Rashidi ambaye ni mama wa madrasa, Ihsani Ramadhani Mwenyekiti na Chande Ibrahim Katibu. 

Hata hivyo, walimu hao wamelalamika sana mahudhurio kwa wanafunzi wakiwa wakubwa wanaamua kuacha chuo bila ya sababu maalumu. 

Matarajio yao wanataka kujenga chuo ili kiwe cha kujitegemea kwa sababu mpaka hivi sasa chuo bado kipo hapo hapo kilipokuwa awali. 

Hivyo, wito umetolewa kwa Waislamu wote na makampuni mbalimbali wajitokeze kwa wingi kutoa misaada yao ya hali na mali ili kufanikisha mikakati hiyo. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI  
Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha 

Serikali yakumbushwa kujiunga OIC 
Na Mwandishi wetu 

Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi 

Wafungwa waomba Futari na Vikoi 

Macho ya shutuma 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Hoja pofu 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Tafuteni ufalme wa kisiasa 

Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 

'Vichupi' vya nini Kimiti? 
Na. Said Rajab 

Mjadala wa Katiba na haki za Waislamu 
Na Masoud Mohammed Mbogo 

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 3 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Waliochukuliwa utumwa Uarabuni 
Na Hassan Omar 

Madrasatul Maamury Islamiya 

Teknologia: Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4) 
Na Hassan Omar 

Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito 

TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' 

Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa  

Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza 

Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga 

Mafunzo ya Qur'an  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa 

Barua za wasomaji  

Masomo ya dini ya Kiislam  

Chakula na lishe 

Mashairi 

Matangazo 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita