|
|
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekumbushwa kutekeleza ahadi iliyoitoa huko nyuma ya kujiunga na Shirika la OIC. Akiwasilisha taarifa ya Baraza Kuu katika kongamano la Waislamu lililofanyika Jumapili Novemba 1, 1998, Katibu Mkuu wa Baraza hilo Sheikh Abas Kilima alisema kwamba ni muda mrefu sasa tangu Serikali iahidi kujiunga na OIC kwa hiyo kwa niaba ya Baraza lake angeikumbusha Serikali kutekeleza ahadi hiyo. Sheikh Kilima alisema haoni sababu ya Serikali kuendelea kusita kujiunga na shirika hilo kwani tofauti na ilivyokuwa ikiripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, malengo ya shirika hilo yako bayana kwa Serikali hivi sasa. Akikumbusha yaliyopelekea Zanzibar kutojiunga na shirika hilo, Sheikh Kilima alisema kwamba hapakuwa na sababu za kidini kwa Zanzibar kuzuiwa kujiunga na jumuiya hiyo. "Lakini Bunge, Serikali na hasa Mwalimu Nyerere, waliipinga kweli kweli, Mwalimu Nyerere kwa mikutano ya hadhara na ya waandishi wa habari alipinga hatua ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano kujiunga na Shirika la O.I.C.", alieleza Sheikh Kilima. Mwaka 1992 Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilitaka kuwa mwanachama wa O.I.C.ili ijikwamue kiuchumi kutokana na misaada na mikopo isiyo na riba inayotolewa na jumuiya hiyo ya Waislamu. Hatua hiyo ya Serikali ya Mapinduzi ilizua mtafaruku ndani ya Bunge, CCM, Serikali na katika vyombo vya habari, kwamba ililenga kuiingiza Zanzibar katika Sharia za Kiislamu na hatimaye kuisilimisha Jamhuri ya Muungano. Sheikh Kilima alilieleza kongamano hilo kwamba O.I.C. haina malengo ya kusilimisha bali kusaidia nchi wanachama wake kuboresha hali za kijamii. "Ni kweli hili ni shirika la dini lakini malengo yake ni kuwajengea huduma za maendeleo, elimu na afya nchi wanachama wake wenye raia Waislamu", alisema katibu huyo wa Baraza Kuu. Wakati huo huo, Waislamu nchini wametakiwa kuwa waangalifu katika chaguzi mbali mbali ili kujiepusha na wale wote wenye mawazo ya kuwafanya ngazi ya kufikia malengo yao kisha kuwapuuzilia mbali mara baada ya uchaguzi. Akizungumza katika kongamano hilo katibu wa jumuiya ya wazazi nchini Bwana Shaaban Kakinga aliwataka Waislamu waanzishe utaratibu wa kupiga kura ya maslahi badala ya kujitumbukiza kwenye chaguzi bila ya malengo ambako kumechangia kuwafanya Waislamu wasiwe na sauti katika sera za nchi. "Kura inayozingatia maslahi yetu kama Waislamu hapa nchini ndiyo liwe azimio letu", aliongea kwa msisitizo katibu huyo wa Wazazi. Waislamu nchini mara kwa mara wamekuwa wakiishutumu Serikali kwamba haiwatendei haki, hata hivyo malalamiko yao yamekuwa yakipuuzwa na vyombo mbali mbali. |
YALIYOMO
TAHARIRI Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha Serikali
yakumbushwa kujiunga OIC
Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi Wafungwa waomba Futari na Vikoi Macho
ya shutuma
Hoja
pofu
Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 'Vichupi'
vya nini Kimiti?
Mjadala
wa Katiba na haki za Waislamu
Mdahalo
kati ya Waislamu na Wakristo- 3
Waliochukuliwa
utumwa Uarabuni
Teknologia:
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4)
Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga Mafunzo
ya Qur'an
|