AN-NUUR 
Na.169 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 2 - 8, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Maoni yetu 

Masheikh tupeni Fatwa 
  

MTU akifa amali zake zote zimekatika ila Swadaqatul-Jaaria, Masheikh wanatwambia. Swadaqa hii huendelea kumpatia thawabu maiti muda wa kudumu swadaqa ile. 

Maana yake ni kwamba kama mtu amechimba kisima kadri watu watakavyoendelea kunufaika na maji ya kisima hicho naye hupata thawabu, ila tu kitakapokuja kukauka. Hivyo kama mtu alijenga nyumba akaiweka Wakfu isaidie yatima au kulipa mshahara wa Mwalimu wa Madrasa, ataendelea kupata thawabu mpaka hapo nyumba hiyo itakapoanguka. 

Lakini je, kama mtu amechimba kisima akatokea mtu kwa sababu zisizoeleweka akaelekeza mtaro wa maji machafu ndani ya kisima hicho ili watu wasifaidike na maji hayo; je nini hukumu ya mtu huyu; na je, yule marehemu ataendelea kupata thawabu zake? 

Watu wengi kwa kuzingatia mafundisho ya Uislamu na kwa kuzingatia nasaha za Masheikh wao, wamekuwa wakitoa Sadaqatul-Jaaria kwa kujenga Misikiti, Madrasa na kuweka nyumba zao Wakfu. 

Kodi inayopatikana kutokana na nyumba hizo hulipa gharama za kuendesha Msikiti, mishahara ya walimu wa madrasa, Maimamu n.k. 

Kwanza tungependa Masheikh wetu watukufu watueleze nini jukumu lao katika kuilinda mali hii ya Wakfu. Nini jukumu la Taasisi, Jumuiya na Mabaraza ya Kiislamu katika kudumisha ‘amana’ hii iliyoachwa na Waislamu wema. 

Na nini jukumu la Waislamu wote kwa ujumla kuzitunza Sadaqa hizi ambazo ni za thamani kubwa kuliko chochote katika hii dunia kwa waliotangulia mbele za haki. 

Pili nyumba ya Wakfu inapogeuzwa Baa bado ni Wakfu? Masheikh tupeni jibu. Na nini hukumu ya yule aliyeitoa kama Sadaqatul-jaaria mbele ya Allah. Bado ataendelea kupata thawabu wakati badala ya nyumba hiyo kuunufaisha Msikiti na Uislamu imegeuzwa danguro na kilabu ya kangara na ‘taska’! 

Nini hukumu ya Allah kwa wale wanaoingia Misikitini wakaswali wakatumia mali zao na nguvu zao kupigania viwanja vyao vinapoporwa lakini wakawa hawafanyi lolote amana za Allah (sw) zinapohujumiwa. 

Masheikh wetu watukufu tunaomba Fatwa juu ya jambo hili. Kitabu cha Allah (sw) na Sunnah ya Mtume (saw) inasemaje. 

Fatwa hii ni muhimu kwa sababu haitakuwa na maana Masheikh kutuhimiza tuwekeze katika swadaqatul-jaariah wakati sadaqa hiyo inakoma mara tu tuingizwapo katika mwanandani. 

Jaalia waliokwenda mbele za haki na kuacha nyumba zao Wakfu wanafufuka na kukuta zimeuzwa na kugeuzwa madanguro na vilabu ya ‘dengelua’ la Kizungu na gongo, vipi wangejihisi. 

Leo ni nyumba ya Bint Omar kesho itakuwa ya Mwinshehe. Tunadhani ni muhimu Masheikh watupe Fatwa juu ya suala hili kabla ya kuendelea kutuhamasisha kuweka mali zetu Wakfu. Ni bora tuziuze wenyewe tukiwa hai tule na kunywa vya halali kwa wasaa kuliko kuziacha Wakfu zije kuwa vilabu vya ulanzi.MTU akifa amali zake zote zimekatika ila Swadaqatul-Jaaria, Masheikh wanatwambia. Swadaqa hii huendelea kumpatia thawabu maiti muda wa kudumu swadaqa ile. 

Maana yake ni kwamba kama mtu amechimba kisima kadri watu watakavyoendelea kunufaika na maji ya kisima hicho naye hupata thawabu, ila tu kitakapokuja kukauka. Hivyo kama mtu alijenga nyumba akaiweka Wakfu isaidie yatima au kulipa mshahara wa Mwalimu wa Madrasa, ataendelea kupata thawabu mpaka hapo nyumba hiyo itakapoanguka. 

Lakini je, kama mtu amechimba kisima akatokea mtu kwa sababu zisizoeleweka akaelekeza mtaro wa maji machafu ndani ya kisima hicho ili watu wasifaidike na maji hayo; je nini hukumu ya mtu huyu; na je, yule marehemu ataendelea kupata thawabu zake? 

Watu wengi kwa kuzingatia mafundisho ya Uislamu na kwa kuzingatia nasaha za Masheikh wao, wamekuwa wakitoa Sadaqatul-Jaaria kwa kujenga Misikiti, Madrasa na kuweka nyumba zao Wakfu. 

Kodi inayopatikana kutokana na nyumba hizo hulipa gharama za kuendesha Msikiti, mishahara ya walimu wa madrasa, Maimamu n.k. 

Kwanza tungependa Masheikh wetu watukufu watueleze nini jukumu lao katika kuilinda mali hii ya Wakfu. Nini jukumu la Taasisi, Jumuiya na Mabaraza ya Kiislamu katika kudumisha ‘amana’ hii iliyoachwa na Waislamu wema. 

Na nini jukumu la Waislamu wote kwa ujumla kuzitunza Sadaqa hizi ambazo ni za thamani kubwa kuliko chochote katika hii dunia kwa waliotangulia mbele za haki. 

Pili nyumba ya Wakfu inapogeuzwa Baa bado ni Wakfu? Masheikh tupeni jibu. Na nini hukumu ya yule aliyeitoa kama Sadaqatul-jaaria mbele ya Allah. Bado ataendelea kupata thawabu wakati badala ya nyumba hiyo kuunufaisha Msikiti na Uislamu imegeuzwa danguro na kilabu ya kangara na ‘taska’! 

Nini hukumu ya Allah kwa wale wanaoingia Misikitini wakaswali wakatumia mali zao na nguvu zao kupigania viwanja vyao vinapoporwa lakini wakawa hawafanyi lolote amana za Allah (sw) zinapohujumiwa. 

Masheikh wetu watukufu tunaomba Fatwa juu ya jambo hili. Kitabu cha Allah (sw) na Sunnah ya Mtume (saw) inasemaje. 

Fatwa hii ni muhimu kwa sababu haitakuwa na maana Masheikh kutuhimiza tuwekeze katika swadaqatul-jaariah wakati sadaqa hiyo inakoma mara tu tuingizwapo katika mwanandani. 

Jaalia waliokwenda mbele za haki na kuacha nyumba zao Wakfu wanafufuka na kukuta zimeuzwa na kugeuzwa madanguro na vilabu ya ‘dengelua’ la Kizungu na gongo, vipi wangejihisi. 

Leo ni nyumba ya Bint Omar kesho itakuwa ya Mwinshehe. Tunadhani ni muhimu Masheikh watupe Fatwa juu ya suala hili kabla ya kuendelea kutuhamasisha kuweka mali zetu Wakfu. Ni bora tuziuze wenyewe tukiwa hai tule na kunywa vya halali kwa wasaa kuliko kuziacha Wakfu zije kuwa vilabu vya ulanzi. 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI 
Majeshi ya nje kupelekwa Lesotho: Je, ni sera za Nguvumali? 

Nyumba ya Wakfu yageuzwa  Baa Dar 
Na Mwandishi Wetu 

‘VAT’ yaingia Bakwata Same 
 Na Mwandishi Wetu 

Mchungaji asema hakuna mihadhara ya kashfa 
 Na Muhibu Saidi 

Maoni yetu: Masheikh tupeni Fatwa 

Safari yangu Ufini 
Ustaadh Ka-Batembo 

Unyanyasaji wa kidini mashuleni, vyuoni ukomeshwe 
Na Abuu Afahah 

Wanaume toeni haki za wanawake 
Na Zabibu Iddi Ng’onda Box 78, Mwadui 

MAONI: Yesu ni yule yule Isa 
Na Saleh Ngoi 

Hatuna uwezo wa kuwapinga manabii 
Na Elia Batendi, S.L.P. 538, DSM 

Ukoloni mwingine unaingizwa nchini? 
Sheikh Thabit H. Mbago,S.L.P. 21486,DSM 

Khatamy ni ‘Gorbacheiv’ mwingine? 
Na Athman Rajab 

Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo kwa maneno 
Mwandishi: Maalim Ali Bassaleh 

AN-NUUR  lina chuki na Wakristo 
Na Charles Kamuhabwa, DSA Mtwara 

Msiiparamie ovyo Biblia 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Yaliyosemwa na viongozi wa dini juu ya idadi ya watu 1989 
Na Rajab Rajab 

Uislamu ulivyoingia Zanzibar -2 

Waislamu Moro watakiwa kutoyumba 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Wanawake Masasi wawataka Masheikh kutangaza sheria za Allah 
Na Muhibu Saidi, Masasi 

Ugaidi na Uislamu siyo kitu kimoja – Sheikh Jongo 
Na Bakari Musa 

Sheikh Abbas awataka wananchi Dodoma waepuke upuuzi 
Na Abu Zubair, Dodoma 

Vijana watakiwa kujiepusha na ‘vijiwe’ 
Na Badru Kimwaga 

Mafundisho ya Quran 
Kutoa katika njia ya Allah: Al-Baqarah aya   261-263 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Magonjwa yanayoathiri lishe 
  

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita