|
|
| Mchungaji
asema hakuna mihadhara ya kashfa
Asema Imani ya Waislamu haiwezi kuwa kashfa Adai haiwezi kuleta machafuko Na Muhibu Saidi MCHUNGAJI wa Kanisa la Kilutheri Temeke Bw. Msafiri Chabulilo amesema kwamba imani za Waislamu na Wakristo kamwe haziwezi kuitwa kashfa wala kuleta machafuko nchini. Pamoja na kuibuliwa propaganda ya mihadhara ya kashfa; Mchungaji Chabulilo amesema hajaona mabadiliko yoyote katika ushirikiano wa mambo mbalimbali kati ya Waislamu na Wakristo uliokuwepo toka zamani. Ameyasema hayo kufuatia onyo la Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mh. John Chiligati (Capt.) kwamba serikali itapambana na wanaoendesha mihadhara inayokashifu dini nyingine. Katika kikao chake na viongozi wa kidini Septemba 28 ofisini kwake, Kapteni Chiligati alidai kwamba watu wanaoendesha mihadhara hiyo ni watu wachache ambao alidai kuwa wanafanya hivyo kutokana na kusumbuliwa na njaa. Kapteni Chiligati alisisitiza kuwa iwapo watu hao wataachwa waendelee na mihadhara hiyo watasababisha mapigano kama yale yanayoendelea katika Jamhuri ya Congo ambapo alisema hali hiyo itasababisha pia Misikiti na Makanisa kutokuswaliwa. Akizungumzia suala la kuchanganya dini na siasa, Kapteni Chiligati alishutumu kitendo cha Misikiti na Makanisa kutumika kama viwanja vya siasa, jambo ambalo alisema ni hatari tupu inayoweza kuiletea nchi matatizo. "Makanisa na Misikiti ni mahali pa swala tu. Inashangaza kuona watu wanaacha vyama wanatumia Misikiti na Makanisa. Hali imefikia leo watu hao wanatangaza kwamba mwaka 2000 Rais awe Muislamu au Mkristo, tuwe macho na hili litatuharibia", alisema Mh. Chiligati na kuongeza kuwa anashukuru sana kuona mambo hayo hayapo katika wilaya yake. Alidai kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Luteni Yusufu Makamba alikwisha wahi kuwatahadharisha wakuu wake wa wilaya kuhusiana na kitendo cha Msikiti mmoja uliopo Konondoni cha kugawa kadi za chama cha CUF ndani ya Msikiti. Hata hivyo Mh. Chiligati hakuutaja Msikiti huo. Mapema akitoa mchango wake katika mkutano huo, mmoja wa wadhamini wa ALMALLID, Mzee Amani Mushi alimwambia Mkuu wa Wilaya kwamba suala la mihadhara inayoitwa ya "kashfa" limekwisha wahi kuzungumzwa Ikulu baina ya Masheikh na Maaskofu chini ya Uenyekiti wa Rais mstaafu wa pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, lakini halikupatiwa ufumbuzi kwa kashfa hizo kuwekwa bayana. Mzee Mushi aliongeza kuwa pia kikao kingine kama hicho kimewahi kufanyika katika Hoteli ya Forodhani, Jijini chini ya Waziri wa Mambo ya Ndani wa zamani Mh. Ernest Nyanda na hivi karibuni, kilifanyika kikao kama hicho katika ukumbi wa Karimjee chini ya Uenyekiti wa Waziri wa sasa wa Mambo ya Ndani, Mh. Ali Ameir Mohamed ambapo Wakristo na Waislamu walikubaliana kwa kauli moja kuvumiliana katika imani zao za msingi. Aidha, Mzee Mushi alisema wakati huo huo serikali ilikwisha sema kupitia kwa Makamu wa Rais, Dk. Omar Ali Juma kuwa haitangilia tena mambo ya dini badala yake itawaachia wana dini wenyewe. "Leo tunashangaa kuona tunaitwa na Mkuu wa Wilaya kurudia suala lile lile", alishangaa Mzee Mushi. Akizungumza katika kikao hicho, Sheikh Omar Matata alisema kwamba mahali popote ambapo haki haitendeki basi hakuna amani na akatahadharisha kwamba kama serikali itawadhulumu na kuwaonea Waislamu basi ijue amani haitakuwepo. Aidha, Sheikh Matata amesisitiza kwamba Waislamu hawako tayari kumtii kiumbe yeyote kwa kuacha kuhubiri mafundisho ya Uislamu kwamba Yesu si Mungu, na kwamba hakufa msalabani wala kufufuka. Alisema kufanya hivyo itakuwa ni kumuasi Mwenyezi Mungu. Akijibu madai ya Mkuu huyo wa Wilaya ya Temeke kwamba baadhi ya waliotoka
rumande wanatamba kuendeleza mihadhara ya kashfa na kwamba serikali itawakamata,
Sheikh Matata alisema pamoja na kuwepo mkakati huo, lakini hakuna hata
kesi moja ya watuhumiwa hao imekwishafika mwisho wake zaidi ya usumbufu
na uonevu.
|
YALIYOMO
TAHARIRI Majeshi ya nje kupelekwa Lesotho: Je, ni sera za Nguvumali? Nyumba ya Wakfu yageuzwa Baa
Dar
‘VAT’ yaingia Bakwata Same
Mchungaji asema hakuna mihadhara ya
kashfa
Maoni yetu: Masheikh tupeni Fatwa Safari yangu Ufini
Unyanyasaji wa kidini mashuleni, vyuoni
ukomeshwe
Wanaume toeni haki za wanawake
MAONI: Yesu ni yule yule Isa
Hatuna uwezo wa kuwapinga manabii
Ukoloni mwingine unaingizwa
nchini?
Khatamy ni ‘Gorbacheiv’ mwingine?
Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo
kwa maneno
AN-NUUR lina chuki na
Wakristo
Msiiparamie ovyo Biblia
Yaliyosemwa na viongozi wa dini juu
ya idadi ya watu 1989
Uislamu ulivyoingia Zanzibar -2 Waislamu Moro watakiwa kutoyumba
Wanawake Masasi wawataka Masheikh
kutangaza sheria za Allah
Ugaidi na Uislamu siyo kitu
kimoja – Sheikh Jongo
Sheikh Abbas awataka wananchi
Dodoma waepuke upuuzi
Vijana watakiwa kujiepusha
na ‘vijiwe’
Mafundisho ya Quran
Chakula na Lishe
|