AN-NUUR 
Na.173 Rajab 1419, Oktoba 30 - Novemba 6, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Akina mama watakiwa kushikamana na dini yao 

AKINA mama Waislamu wametakiwa kushikamana na dini yao kama njia pekee ya kujikomboa. Hayo yamesemwa na wahadhiri mbalimbali kwenye kongamano la siku moja lililofanyika Oktoba 24, katika Msikiti wa Ijumaa Kigogo CCM Jijini Dar es Salaam. 

Kongamano hilo lililohudhuriwa na akina mama wa Kiislamu wapatao 1500 lilianza saa mbili asubuhi kwa Qur’an tukufu, na kufuatiwa na mada ya elimu iliyotolewa na Amirah wa akinamama - Wilaya ya Kinondoni, Bi. Zaituni Ahmad ambaye alisisitiza kuwa elimu haina faida kama haitekelezwi. La muhimu ni kufanyia kazi yale yote tulioyasoma, alisema na akawataka akina mama wote ambao mpaka leo bado hawajajiunga na darsa za akina mama haraka sana wajiunge. Alisema Uislamu hautaki watu wajinga, na huwezi kuwa na uchungu na Uislamu ikiwa huufahamu. 

Mada ya pili ilikuwa ni harakati za Kiislamu iliyotolewa na Ummu Hamza kubwa zaidi aliloliongelea ni kuusimamisha Uislamu katika maisha ya kila siku na kwamba Uislamu ndio mkombozi pekee wa kweli wa matatizo ya akina mama. 

Aidha, alisema kwamba Qur’an ndio dira na mwongozo wa Waislamu na wala haitakiwi kutekeleza baadhi ya Aya bali Aya zote. 

Bi Fatuma Lazaro, Katibu wa Kamati ya Kutetea Haki za Akinamama (T), alielezea kuwa tatizo kubwa kwa Waislamu ni kutokuishi Kiislamu katika maisha yao ya kila siku, na dawa pekee ya huku kunyanyaswa na kudhalilishwa ni kuuteleza Uislamu vilivyo, kwani nusra haiji kwa kutamani tu basi, bali huja baada ya kuchukua sababu za nusra na Allah habadilishi hali za watu mpaka wajibadilishie wao wenyewe kwanza. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Wakipewa fursa watainusuru nchi

Wasomi watetea haki ya wananchi kumiliki ardhi

Serikali izungumze na wananchi–Mzee Gonga

Akina mama watakiwa kushikamana na dini yao

Maoni
Serikali inaWhite Paper:  Wananchi mna nini?

Dondoo za Saikolojia: Hoja kengeza
Na Abu Halima Sa Changwa

Makala ya mtangazaji
Khatamy sio Gorbacheiv!!!

Makala
Malipo ya fadhila
Na Mohamed Saleh

Tanzania tuna sera gani kuhusu kanda
Na Abu Abdullah, Tanga

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 2
Na Nandenga wa Mkomidachi

Teknologia
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (3)
Na Hassan Omar

Makala na habari
'Usiiparamie ovyo Theolojia'
Na Charles Kamuhabwa, DSA Mtwara

Mwinyimkuu kufanya sensa ya waumini Magomeni
Na Jamillah Nassoro

Same tusilimu upya

Wazazi Mwanza wahimizwa kuwashonea watoto wao Hijab
Na Idd Katimba, Mwanza

Tuwaige Wangazija, 'tutafanikiwa'
Mwandishi: Maalim Bassalah

Serikali imeweka rekodi ya kutisha – Sheikh Salim
Na Mwandishi Wetu

Muhadhara waunguruma Geita
Na Hussein Abdallah, Geita

Fuateni Sharia ya Allah - Sheikh
Na Badru Kimwaga

Wanawake wa Kiislamu Mburahati wahimizwa kutafuta elimu

Mafunzo ya Qur'an
Vijana wa pangoni

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na lishe
Chakula ni silaha ya kukabiliana na changamoto ya kansa
Na Mujahid Mwinyimvua

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita