AN-NUUR 
Na.184 Ramadhan 1419, Januari 15 - 21, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
MSADAT yazidi kutia moyo Tanga

WAKATI mfuko wa sadaka Tanga ukiingia mwaka wake wa nne, zimetolewa habari zenye kuzidi kutia moyo. 

Katika taarifa yake ya mwaka ambayo hutolewa kila mwezi wa Ramadhani, inaonyesha kuwa jumla ya shilingi 263,720 zilikusanywa kutokana na visanduku vinavyoning’inizwa sehemu za biashara za Waislamu. 

Taarifa hiyo iliyosainiwa na mdhamini wake mkuu, Sheikh Nassor Rashid, inaonyehs pia kuwa shilingi 60,000 zilipatikana kama zaka za mali kutoka Waislamu waliovutiwa na taarifa ya mwaka jana. 

Zaidi ya fedha hizo kutumiwa kuwalipa walimu wa Maarifa ya Kiislamu wa shule za msingi ya Mwanzange, pia shilingi 33,000 zilitolewa mkopo kwa mwalimu mmoja anayejitolea kufundisha somo hilo kwenye shule za sekondari ili zimsaidie kuendeleza mradi wake. 

Akizingumza na mwandishi wa habari hizi kufuatia kutolewa kwa taarifa hiyo, Sheikh Nassor alionyesha kukasirishwa na baadhi ya watu wenye kupinga sadaka za aina hii, hasa kwenye jiji la Dar es Salaam. 

Badala yake alitoa wito kwa Waislamu kuwa madhubuti kwa suala hili, na akapendekeza kwa kila Muislamu kuwa na sehemu ya kukusanyia sadaka kwenye biashara yake pamoja na zaka zenye kuwawajibikia. 

Akifafanua juu ya namna bora ya utekelezaji, alisema kila mmoja anaweza kutengeneza sehemu hiyo kulingana na nafasi yake, inaweza kuwa cha kuning’inia au kwa kutoboa kwenye kuta. 

Alisema mara sadaka ya kutosha ya fedha itakapopatikana, mfnyabiashara mwenyewe achukue jukumu la kuzipeleka sehemu maalum ya kukusanyia itakayokuwa na jukumu la kutatua matatizo mbalimbali ya Waislamu wa eneo hilo. 

Kwa uzoefu wake alisema, ukusanyaji wa aina hiyo hutumika katika nchi za Ghuba, na sehemu kubwa kupelekwa kwenye nchi maskini za Kiislamu kama yetu. 

Kutokana na ufinyu wa bajeti, taarifa ya mwaka huu haikuweza kupelekwa kwa kila mkusanyaji na wameombwa radhi kwa hilo. 

Wale wote wenye maombi na maswali juu ya namna ya kutekeleza mradi huu wanaweza kutumia anuani ifuatayo: 

Katibu, MSADAT, S.L.P. 6082, Tanga. 
 



Mjue Usama bin Ladin 

VYOMBO vya habari vya nchi za Magharibi vimekuwa vikimtangaza kama ni gaidi wa Kimataifa na serikali za nchi hizo Marekani ikiwa mbele, zinamsaka kwa udi na uvumba kwa madai ya vitendo kadhaa vya kigaidi.  

Je, umepata kumsikia bin Ladin mwenyewe akijieleza? Je bin Ladin anapambana na nani na kwa maslahi ya nani? 

Basi kuyajua hayo na mengineyo mengi, usikose toleo lijalo. Insha-Allah. 

  
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa 

Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd 

Ubungo yakumbwa na ukame 

Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 

Dondoo za saikolojia 
Na. Abu Halima Sa Changwa 

Waislamu turejee kwa Allah 

MSADAT yazidi kutia moyo Tanga 

Mjue Usama bin Ladin 

MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI 

Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu 

Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii 

Hakuna Magharibi wala Mashariki: Uislamu ni ubinaadamu 
Na Abubakari S. Marwillo 

Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma mjini 
Na Abu Zuberi, Dodoma 

Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat - Tabata Kimanga 
Na B. Mwakangwale 

Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui 

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana 

Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake 

Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma 

Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti 

Mnyororo wa imani-2 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Kutoka magazeti ya zamani: 
Wanaoshitakiwa kwa uhaini kortini leo 

Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa Kanisa la Walokole 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Masjid Nurania yaswaliwa Ijumaa 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Jabal Hira kutoa mafunzo ya Kompyuta Morogoro 
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Internet ni nini?] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Thamani ya mlo wa Uyoga] 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita